Geza Ulole
Platinum Member
- Oct 31, 2009
- 75,683
- 107,124
Mi naomba evidence akisema makabila makubwa ya Wachagga, Wahaya na Wanyakyusa yasitawale!Wakati Nyerere anaongea hatuwezi kujua alikuwa katika mood gani, au aliudhika nini na hawa watu.
Si maneno yake yote yanaweza kuwa sheria mengine aliongea ki ubinadamu ,ndio maana naye alisema kwenye utawala wake kuna vitu alikosea,akashauri vilivyokosewa tuviache na tuangalie yaliyo mema,utakuta hata hii kauli ni mojawapo ya aliyokosea.
Ila kwa kuwa huko tulishatoka tuyaache tuendelee mbele.
Alisema pia mtu asichaguliwe kuwa kiongozi kwasababu ya ukabila wake au asinyimwe kuwa kiongozi kwasababu ya ukabila wake ,isipokuwa achaguliwe kwa kuwa ana uwezo wa kuongoza.
Hii kauli watu wasiitumie kuwanyima wengine haki ya kuongoza nchi eti kisa Nyerere alishasema. Vitu vingine vitenguliwe kwa maslahi mapana ya nchi yetu.