The best 007
JF-Expert Member
- Oct 6, 2019
- 42,616
- 98,847
Shida inakuja moja kwamba Watz hatukuwahi kuona faida ya nyie kuongezwa mishahara, ila tuliona faida ya nyie wafanyakazi wa serikalini kutoongezwa mishahara na badala yake kujenga hospitali, zahanati, madaraja, barabara, bandari, airports, reli, etc.Labda sijui heshima manake nn,
Naona kuna mahali umenitaja na kusema suala la mishahara, Kuna mikataba ,sheria na utaratibu ambazo zipo na kitaalamu zinatambulika,suala la kuongeza mishahara halihusiani na ujenzi wa madaraja ama ujenzi wa aina yoyote ile...Sasa bad enough unapogusa maslahi ya watu usitegemee ueleweke watakuelewa wale ambao hawana direction na maisha yao tu.
Raisi ni mwanasiasa wako watu wanaofanya kazi lazima awathamini Jpm hakua anaheshimu wafanyakazi alikua anaamini yeye mwenyewe ndio anaweza kufanya kazi,Kitu ambacho sio kweli,Binafsi naweza sema alijitahidi kufanya kazi ila kipengele icho sijawahi kumkubali hata siku 1