Kwamba enzi za Magufuli kulikua na matumizi madogo kuliko hivi Sasa?, tunahitaji kupewa ushahidi katika Hilo. Kuna njia mbili ya serikali kuthibitisha,.
1)Kiwango cha uzalishaji umeme enzi za Magufuli na Sasa hivi
2)Kiwango cha umeme kilichokua kikitumika katika kipindi cha mwaka au mwezi kwa wakati ule na Sasa hivi/Makusanyo ya mapato yatokanayo na mauzo ya umeme yalinganishwe.
Serikali/Makamba na rais Samia wote wanalalamika kuhusu uchakavu wa miundombinu ya usambazaji umeme kuwa ndio chanzo, tunaweza kuamini juu ya Hilo, lakini swali la kujiuliza ni kwamba mbona kipindi cha Magufuli madhara ya uchakavu hayakuonekana Kama inavyoonekana Sasa hivi?.
Kama kweli hivi Sasa matumizi yameongezeka kutokana na uchumi kufunguka, tunaomba takwimu ili kweli tuamini, lakini kutoa majibu mepesi mepesi kwa Mambo ya msingi Kama haya haifai.
Jambo Moja ambalo viongozi wa Sasa hivi ni lazima wajifunze ni kwamba, Magufuli amewafungua macho watanzania kwamba Mambo yanawezekana Kama watumishi wa umma watafanya kazi zao vizuri, iwe kwa kupenda au kwa kushikiwa bakora, watu hawataki maneno na maelezo mengi, wanataka kuona vitu vinafanyika
Sent from my itel L5007 using
JamiiForums mobile app