Sasa ilipaswa huyo Simon ndio azungumze hayo kwasababu yeye yupo TANESCO Kama kweli anazo hizo data, wewe itakua vigumu kueleweka.
Kuhusu Makamba huko Bingeni tumemsikiliza, zaidi ya kuzungumzia matatizo ya kiufindi na kuchakaa kwa miundombinu ya umeme, hajazungumzia lolote kuhusu kuongezeka kwa uzalishaji, sio kazi ya TANESCO Wala hawezi kujua lolote kuhusu ongezeko la uzalishaji, wao wanachojua ni kuhusu ongezeko la matumizi tu.
Mkuu, mahitaji ya umeme Tanzania hadi Sasa ni 1400MW, na uzalishaji wa umeme ni 1700MW, maana yake tunazalisha umeme zaidi ya mahitaji yetu, kwahiyo hakuna peak demand inayozidi au kufikia 1700MW, kwahiyo tatizo lipo kwenye usambazaji hasa kutokana na TANESCO wenyewe kushindwa kugundua matatizo mapema katika njia za usambazaji na kuzirekebisha kabla tatizo halijatokea.
Magufuli alifanikiwa Sana kuwafanya wafanyakazi wa serikali kuwa "proactive" badala ya kuwa "reactive" katika utendaji wa kazi, ndio sababu umeme kipindi chake ulikua haukatiki mara kwa mara, wafanyakazi waliokua wanaogopa kushitakiwa kwa Magufuli kupitia safari zake za ghafla nchi nzima, hivi Sasa wafanyakazi wameanza tena kujisahau
Sent from my itel L5007 using
JamiiForums mobile app