Mkuu ni kipengele gani cha Katiba ya Sasa ambacho unadhani ni kibovu?. Je kikibadilishwa unadhani ni Mambo gani yatabadilika nchini?.
Tujifinze kutoka kwa majirani zetu ambao walibadili Katiba kwa shangwe na vigelegeke, Je wamefaidika nini?, Mbona matatizo na hali zao za kiuchumi, kisiasa na kijamii ndio zinazidi kuwa mbaya zaidi?
Me ninadhani tatizo siyo katiba. Viongozi wetu ndio wana mawazo mgando hawana spirit ya maendeleo, viwango vya utendaji ni hafifu sana, hata wale wanaonekana kufanya vizuri wanapigwa vita sana na majungu.
Kujenga masoko mapya nayo inahitaji katiba mpya? Dawa na vifaa tiba hospitalini napo kunahitajika katiba mpya kweli? Issue ya MSD ni aibu kwa taifa.
Tunahitaji visionary leaders na siyo hawa wachumia tumbo. Katiba mpya hata iwe nzuri kiasi gani kama viongozi hawana maono ni taifa mfu.
Nakuunga mkono mkuu katiba mpya haiwezi kufanya kazi kwa ufanisi yenyewe pasipo viongozi kubadilika na kuwa na maono. Watu ni wezi sana.
Yaani mtu hana mshipa wa aibu anaweza kuiba fedha zote za bajeti ya barabara km kadhaa na wananchi wakaendelea kuteseka asione shida as long as watoto wake wanaishi vizuri.
Viongozi wa Afrika hawana uchungu na wananchi wa chini wanajiangalia wao tu, katiba zetu zinaweza kufanya kazi vizuri sana kama ikitokea tukatawaliwa mara ya pili kwa mfumo ule ule wa miaka ya ukoloni na siyo huu wa mamboleo.
Mfano wazungu wawacharaze viboko hadharani wabunge wasionekana jimboni, wakuu wa mikoa na wilaya, wakurugenzi, mawaziri na makatibu wakuu, halafu uovu wao utangazwe hadharani, hapo watabadilika na kufanya kazi sawa sawa.
Afrika ina intelligent people lakini mifumo ya uongozi haiwapi nafasi kufanya vizuri ndio maana huko nje huwa wanafanya vizuri sana kwa vile wanapewa nafasi kuonyesha kile walichonacho.
Huku kwetu ukiwa na influence kidogo tu na watu aliyeko juu anahisi unataka kupindua meza, utatengezewa zengwe mpaka ukimbie mwenyewe.
Afrika wivu, uchoyo, ubinafsi, uchawi na ushirikina, wizi,ufisadi, uvivu,ukwepaji kodi,roho, mbaya n.k ndio kikwazo cha maendeleo. Katiba Mpya tunaisingizia tu.