Sawa kaka ngoja tuone after 6 yrs itakuwaje. Ila huko nyuma ulipokuwa ukienda ofisini unakaribishwa na kusikilizwa haraka tena ukikutwa umekaa kwenye bench unaulizwa umeshasikilizwa? So nidham ilikuwepo kama ilikuwa ya uoga ilisaidia kiasi kikubwa. Sasa hivi hiyo hali haipo.
Mimi simpingi mama ni Rais wetu , ni mama yetu lakini asiongoze kwa upole sana watendaji wakimjua udhaifu wake watamkwamisha mipango yake, nadhani watz unawajua wakishakusoma.
Kwahiyo hatupigi kelele kwamba tunampinga au kumkwamisha la hasha! Tunamzindua asiwachekee hawa,akishindwa yeye ni taifa zima tumeshindwa, akikwama yeye tumekwama sote.
Mtu anayekupenda na kukutakia mema huwa anakwambia udhaifu wako. Mama hawezi kujua yote kuna mahali watendaju wake wanamdanganya kwa maslahi yao binafsi. Hatumchukii tunampenda na tunataka afanikiwe na amalize salama kipindi chake cha uongozi.