Kenya ilishapoteza pambano na TZ Kati hili eneo la SGR, sababu kubwa ya mchina kukataa kutoa pesa kumalizia kipande hadi Malaba, alijua kwamba hakutokua na faida kibiashara kwasababu Uganda ilishakosa pesa ya kuifikisha Kampala.
Kama SGR haiwezi kuunganisha nchi zaidi ya tatu, haiwezi kuwa na faida, Kenya walitegemea Sana Uganda waifikishe Kampala, ili angalao Rwanda wangepata nguvu ya kuunganisha hadi Kigali, au japo DRC, Rwanda, na South Sudan wangeweza kuchukulia mizigo Yao Kampala.
Kitendo cha Uganda kushindwa kupata pesa, na ugomvi Kati ya Rwanda na Uganda, vilipigilia msumari wa mwisho kwa reli ya Kenya kushindana na Tanzania.
Kuhusu reli ya umeme kutumia "diesel engine locomotives", hiyo ni Kama kiwanda kuwa na "standby generator" iwapo umeme utakatika, kumbuka ni ghali Sana kutumia "diesel", hiyo ni miongoni mwa sababu kubwa kwanini hizi nchi zimeamua kuungana na Tanzania na kuachana na Kenya, kumbuka hata Uganda walisema kwamba hata kama wangejenga reli kuunganisha na Kenya, lakini wangejenga ya umeme.