Wacha porojo mingi, kupata Elimu au kutopata Elimu kwa raia wa nchi kunatokana na sera nzuri za Elimu za serikali/nchi husika, hatuzungumzi familia Moja Moja.
Tanzania Nyerere alilazimisha kwamba ni lazima kila mtoto kupata Elimu ya msingi(Primary Education), ili kufanikisha hilo aliifanya Elimu ya msingi kupatikana bure na ni lazima mzazi kumuandikisha mtoto wake shuleni, kushindwa kufanya hivyo lazima mzazi atashitakiwa na kutozwa faini.
Nyerere ndiye aliyeanzisha Sheria ya kukataza mtoto aliyepata mimba kuendelea na masomo (Formal education), badala yake akaanzisha mfumo wa "adult education" ambao utamuwezesha huyo mtoto kusoma hadi chuo Kikuu huku akiwa anaendelea na jukumu lake la kulea mtoto na akipenda kuolewa.
Ni mtu mpuuzi ambaye anaweza kupinga mfumo mzuri wa Nyerere ambao umempa nafasi huyo Binti kuendelea na masomo Kama mzazi wakati huo huo kupunguza athari za kisaikolojia ambazo zingeweza kusababishwa na yeye kwa wanafunzi wenzake au kwake kutoka kwa wanafunzi wenzake endapo angeendelea kusoma shule na darasa lile lile