Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Wakunya kazini
Screenshot_20211031-092247.jpg
 
Hiyo historia unayoongelea ni ya kuletwa kama tu hii yetu ya majengo ya Wazungu unayoibeza - hiyo ni ya majengo ya Waarabu wa Omani. Sasa kabla useme Kenya iko colonized, pia nawe uache kuiga Waarabu ujenge chako

Kilwa Ruins
kilwa.png


Zimbabwe Ruins
Zimbabwe.png



FYI Waomani walikuja 19th century, himaya ya Kilwa ilikuwepo toka 9th century. Sasa nioneshe magofu yoyote mliyojenga nyinyi kabla ya wageni kuja (usiniletee fort Jesus hapa).
 
Kwahiyo ni central bank au ni office tower.
Times Tower is 100% occupied by the KRA, kutoka floor ya kwanza hadi ya mwisho. It doesn't have any other tenant apart from the KRA. KRA and Central Bank are one and the same thing, ndio maana hata hizi buildings mbili (Times Tower and Central Bank) zinakaribiana
 
Nimesema jengo la BOT Pension tower kama sisi tulivyo na CBK Pension Tower nikakuelezea ni department ya CBK ukakana. Sasa nionyeshe hilo la BOT Pension Tower sio tu jumba lolote lililo na jina pension.
Mwambie tuko na pension houses nyingi hapa Kenya. Nyingine ndio hii hapa pale Loita Street, Nairobi
images (37).jpeg
images (29).jpeg
 
Kumbe hujui historia, pwani ya Africa mashariki ilikuwa aina ya majengo yake hata kabla ya wageni kuja. Ukiangalia kwa makini majengo ya zamani ya Dar, Tanga na Bagamoyo utaona yana utofauti na yale ya Zanzibar. Yale ya Zanzibar yanafanana na yale ya Omani wakati yale ya bara yanafanana na majengo ya zamani ya himaya za Kilwa na Mwenemutapa.

Wajerumani walipovamia pwani yetu walishangazwa na ujenzi huo wa pwani (kwa jinzi unavyo maintain humidity and temperature, ndani) na kuamua kuiga usanifu huo wa kiafrika. Ndiyo hayo maboma ya wajerumani, yako kila mahali Tanzania nzima.

Majengo waliyojenga wajerumani kwenye makoloni yao mengine kama kule Namibia ni tofauti na yale ya Tanganyika, kule walijenga kutumia usanifu wa kijerumani (Gothic), Dar bado in majengo machache ya kigothic mfano ni kanisa la Azania front. Kama hujui, usanifu huo wa kiswahili unatokana na kuiga usanifu wa siafu (ants) wanapojenga kichuguu (anthill). Jotoridi ndani ya kichuguu huwa halibadiliki sana kulinganisha na joto la nje.
Naona unajua historia vizuri
 
Back
Top Bottom