Mkuu, mtu kuwa kigeugeu (mafiki) na kile anachokisema ni Mambo mawili tofauti kabisa, Geza tunaweza kumuhukumu kwa hilo la kugeuka lakini sio kwa anayoyasema.
Hilo la kugeuka hata Mimi ninaliona na linanisikitisha, ninaamini Moja ya sababu ya kuwa hivyo ni (Counter reaction) baada ya watu kumzonga na kumshambulia Sana akaamua "Kama ni mbwai iwe mbwai", lakini kwa anayoyasema ni ukweli kwa kiasi kikubwa.
Mimi ninamkubali Sana Magufuli, Sana Sana, lakini hayo maeneo anayozungumzia Geza kuhusu Magufuli ni kweli Magufuli alikosea, Mimi ninayachukulia Kama ni sehemu ya mapungufu yake, ninayaweka pamoja na kuyalinganisha na mazuri yake mwisho ninagundua kwamba, mazuri yake yanazidi mabaya yake.
Kosa ninaloliona kwa Geza ni kwamba ameamua kushikilia Yale mabaya yake Kama silaha ya majibishano, lakini Kama tungeamua kutaja mazuri vs mabaya ya Magufuli, hapo ndio tungejua nani angeishiwa hoja mapema.