Mkuu, Mwinyi ameiva barabara. Anayo kila sifa kiongozi visionary anapaswa kuwa nayo. Mbali na maono, ni mtu anayejua namna ya kufanya teuzi.
Juzi hapo kwa mfano, kateua watu ambao kwa hizi elimu zetu za vyeti alikosolewa. Kwamba aliteua watu pasi na kuzingatia profession zao zikilinganishwa na taasisi watakazoongoza. Katoa jibu lililonikosha sana na kunipa imani kubwa sana kwake:
"Mimi sitafuti utaalam, natafuta uongozi". Period.
Rejea,
Ulimwengu wa wanazuoni ulikosoa teuzi/chaguzi zifuatazo;
1. Mkemia kuwa Rais.
2. Mhandisi kuwa Katibu mkuu kiongozi.
3. Mwanasheria kuwa waziri wa mambo ya nje.
4. Mwanasheria kuwa gavana wa benki kuu, nk
Lakini tazama matokeo yake. Chini ya uongozi wa hao watajwa hapo juu ndipo taasisi zao zimekuwa na ufanisi zaidi tangu uhuru wa nchi hii.