Kuna watu wanasikia raha masuala ya wizi na rushwa yanavokuwa ndio headlines, bila kujua kwamba kuna vitu vingi tunavikosa kwa huu wimbo, Nampongeza mama lkn wale wapinzani wanataka kutumia hii km mbinu kutuanzishia kutuaminisha kwamba utawala uliopita ulikuwa nao una ubadhirifu sana. Huu ndio wimbo unaoiua Africa yetu, cha msingi hapo kuna vitu huwa havihitaji hesabu za mbali sana ila ni hesabu simple tu, Mf, Hata umpe mtu hela akujengee nyumba hapa bado kuna jero atakunywa maji tu, sasa wapinzani wanataka tuuimbe wimbo wa rushwa wee mpaka miradi mingine wasite kuja kwasababu hiyo. Wakufanya nchi ionekane safi ni sisi na wakufanya ionekane chafu pia ni sasa, Hapa Nampongeza sana Mh. Magu maana mkumbuke hili,
ILI KUONDOA RUSHWA AU WIZI NA UVIVU WE ZUNGUMZIA KUCHAPA KAZI TU.
ILI KUONDOA UJINGA ZUNGUMZIA ELIMU,
ILI KUONDOA HOFU ZUNGUMZIA UJASIRI,
ILI KUONDOA UADUI ZUNGUMZIA WEMA,
Sasa mkitaka turudi kule kwenye Ufisadi na Ubadhirifu tunajikaanga sana, nazungumzia kwa Wapinzani naona shauku yao ndio hiyo sana.
Lkn kwa aliye kwenye dola huo kwake niutekezaji safi sana.