Umesoma na kuelewa nilichoandika!?
Hiyo ndiyo reality.
Watu wanamchagua mtu ambaye atawasemea shida zao. Halafu tunapoongelea demokrasia ni kuacha ubaguzi ambao hauana mantiki.
Baadae utaanza kuwabagua walemavu eti wasiweze kuchaguliwa kwa sababu ya ulemavu wao.
Kwa mawazo yako hayo huwezi ukawa kiongozi. Siasa ni jambo pana mno.
Hebu nikuulize jambo kati yako na Msukuma ni nani aliyeelimika!? Msukuma anajua issue za madini, yupo na mabasi. Kabla hata ya kuwa mbunge alikuwa anamilk Helkopita.
Kishimba mbunge wa kahama mjini ameishia darasa la saba. Anamilk viwanda, Dar free Market ni yake, Imalaseko Super market ni yake.
Wapo wabunge wengi tu weishia darasa la saba lakini wamefanya mabadiliko makubwa tu.
Laizer wa Melerani anamilk mgodi wa Tanzanite.
Usimdharau mtu.