Jana niliingia Dodoma nikasema ngoja ninyooshe kidogo miguu kutembea mjini (kutoka hotel niliyofikia) yaani kuna machinga kinoma.
Maeneo ya makao makuu ya ccm kuna machinga wa kutosha hadi ile barabara iliyoko karibu na Nmb Dodoma branch wameiziba yote.
Nikatokea maeneo ya Square pale asee kuna machinga kinoma hadi wamepewa barabara yote two lanes na sehemu za watembea kwa miguu yote wanamiliki machinga



mtaa mzima wanamikiki machinga.
Nikatokea tena kule karibu na soko asee machinga wametawala barabara hadi sehemu za watembea kwa miguu.
Nikapita tena usiku huwezi amini barabara zinavyo kuwa nzuri machinga wakiwa hawapo.