Nashukuru sana kwa kunielewa mkuu, ni kwamba hata Maraisi wetu tunapaswa kuwalipa mishahara mikubwa pengine kuliko hata marais wa mabeberu ili wawe wazalendo na mali zetu, unajua tatizo letu waafrika tumeharibiwa na hii elimu yetu ya darasani eti utakuta mtu msomi wa Phd anahubiri demokrasia wkt hata yeye mwenyewe haiwezi hyo demokrasia.
Hao walioianzisha tu hawaiwezi itakuwaje cc waafrika? Kwa jicho langu la mbali natamani ifike wakati WaTz tuamue kuwa na huyu rais kwa muda mrefu japo miaka 30 hv na tumlipe mshahara mkubwa zen atusafishie hii nchi cz haya mambo ya kupoteza zaidi ya bilioni 300 kila baada ya miaka 5 kwa kisingizio cha demokrasia ni upuuzi mtupu.
Angalia hzo pesa tulizopoteza kwa ajili ya uchaguzi wakati kila mtu alijua kwamba nn kitatokea je zingetengeneza barabara za urefu wa kilomita ngp? Km tungesema tununue dawa zingekuwa tani ngp? Je tungeokoa WaTz wangapi ambao wamekufa kwa kukosa dawa?
Tufungue macho waafrika tupambane na njaa kwnz km wao walivyopambana zen waliposhiba ndpo wakaingiza hyo demokrasia kwamba kila mtu ana haki ya kuwa raisi, but kuanza kuingiza demokrasia wkt tuna njaa haiwezekani narudia tena haiwezekani cz demokrasia haiwezi ku operate kwenye njaa.
Ni very tricky namna ya kuiweka hii..
Kwanza kuna shida ya matabaka... Walionacho na wasionacho. Hii imeangusha tawala nyingi na kubwa katika historia ya ulimwengu.
Demokrasia ni kilele kabisa cha tawala zilizofanikiwa zaidi... Dhana ya uhuru inakuja tu pale tunapotaka kutumia lakini unapokuja kwenye kutafuta hakuna demokrasia..maana utafutaji lazima uwe na elements za kujitoa.
Kutumia hakuna kipimo na ndio maana tunakuwa na uhuru.. ukiweka chapati mezani kunakuwa na uhuru wa kuchagua nile nusu, nile tano au tagawana moja moja kulingana na walengwa. Mtoto hawezi lazimishwa kula chapati tatu..sawa na mtu mzima.. ila kama ni watoto wote na hazitoshi tunaweza kuja na namna sahihi ya kugawana. Japo haya yote lazima kuwe na kuheshimu makubaliano kunakotoka ndani ya moyo. Uzalendo.
Kwenye Kutafuta inakuwa tofauti kidogo... Nature ya mwadamu inadhihirika kwa uwazi. Ubinafsi... Hakuna mwanadamu anapenda kuumia kwa ajili ya wengine.. na kwa sababu hii "Kafara ya Yesu Kristu" inakuwa na uzito kwetu.
Utafutaji ndio msingi wa mafanikio ya Taifa.. Nidhamu ya matumizi ndio kilele cha njia ya kuimarisha mafanikio.. hulka ya mwadamu ya kujipenda zaidi lazima ichungwe. Na hakuna njia ya kirafiki kwenye hilo.. kutakuwa na malengo na mnyapara wa kukunyoosheni kuyafikia.
Sisi tuna Rais Mkali (kiongozi haswa) Marekani wana mfumo mkali sote tunapata adha ile ile.. utofauti wetu na wao sisi kuna mwanya wa kuweka ubinadamu ndani ya mtu.. ila ni kazi kuufanya mfumo uwe wa kibinaadamu.
Hapa tulipo ni mahali sahihi... Tunachopaswa na kujenga Hybrid itakayojengwa juu ya uongozi wenye utu na ubinadamu na mifumo ya kitaasisi wezeshi.. ili kuupa tija zaidi mfumo wetu wa kujitawala... Na siku moja tuweze kuwapelekea ndugu zetu barani kote Afrika na ulimwenguni.
Kuwa na chaguzi ni muhimu... Ila nadhani ni bora tungekuwa na sera ya kitaifa ya maendeleo ya miaka 20/30&50 kisha vyama vikachuana juu ya namna bora ya kutekeleza... Implementation strategies.. uzuri wake sera zinaweza kuwa sehemu ya.mihula ili watu wazijue ndani nje.. na waweze kupima ni nani ana njia.bora ya kutekeleza. (Mawazo yangu binafsi)
Sent from my Infinix X650 using
JamiiForums mobile app