Mkuu nahisi kuna complication ya ujenzi ukiwa unaingia mza.
Kunaweza hitajika kupasua milima ambayo si kazi ya kitoto, nafikiri wengi wetu tunajua jiografia ya mza.
Mwanza na isaka kuna marshaling yards kama sikosei.
Ukiacha tabora, mwanza - isaka ina vituo vingi vikubwa, ambavyo ni mwanza na shinyanga, isaka na malampaka vinaweza kuwa vituo vya size ya kati ila si vidogo.
Uwezekano wa mza isaka kuchukua muda mrefu kwenye ujenzi kuliko makutupora isaka ni mkubwa.
Let assume mwaka kesho wakatangaza tender ya makutupora isaka Unaweza kuta ujenzi ukaisha sawa na wa mza isaka. kutakuwa hakuna utofauti sana na hata ukiwepo ni miezi sita or less.
Suala la mizigo kuanza kuchukuliwa na sgr si la hivi karibuni. Inavyoonyesha linasubiriwa daraja la pale gerezani liishe ndio ujenzi uanze kuelekea bandarini.