Muigai Jr
JF-Expert Member
- Jun 3, 2020
- 2,218
- 4,043
Budjet ya jeshi sio kigezo sana mkuu...kuna mambo mengi sana...mfano mzuri ni Kenya na Nguvu zake za kijeshi...Kikundi kidogo tuu Alshabab kina waenyeshaNdio sababu nikasema mkuu mbona sikuekewi?
1)Kwanza sijasema kwamba kuna Vita au kutatokea Vita, ila nimesema Egypt ana nguvu za kijeshi za kuweza kulivunjilia mbali hilo bwawa bila Vita kutokea.
Sasa mkuu unasema maneno mengi bila kuangalia Geography ya hizi nchi mbili, hizi nchi hazijapakana kama hizo Iran na Iraq, sasa hiyo vita itatokeaje wakati nchi moja inao uwezo wa kutuma silaha toka mbali na kulivunja wakati Ethiopia haina jinsi ya kufika Egypt kulipiza kisasi?.
Kuhusu uwezo wa majeshi kuwa ni kigezo cha kushinda Vita, ninashangaa sana kwa kupinga hilo, sasa kigezo cha kushinda Vita ni kipi kama sio uwezo wa jeshi?, unategemea Tanzania tushinde vita dhidi ya Urusi, China, USA, UK au India.
Angazia pia kuhusu Vita vya vinavyoendelea Yemen,Saudi Arabia Anajuta sana mpaka sasa..
