Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

😂😂😂😂 bakia kusema kwann US na japan wanamadeni wakat hzo hzo nchi zinawadai pesa kibao😂😂👇👇 na zinawapa msaada wa chakula kila mwaka


Ukiisikiliza serikali ya Magu inasema deni ni himilivu na wanatoa mifano kama hii wanayotoa wakenya kuhalalisha ukopaji na kuwashushua wanaotoa tahadhari,sasa kwa kasi ya ukopaji sitashangaa mika mingine 5 ya Magu nchi ikaingia kwenye hali hii kama ya Kenya maana tulikuwa tunaambiwa serikali inajenga kwa pesa zake ikajagundulika kumbe ni mikopo nadhani mnafahamu awamu ya 5 kwa mda mfupi imekopa kuliko awamu yoyote yeyote iliyopita ,kwa hiyo ni mapema sana kuwacheka na kuwa na akiba ya manene kama ilivyokuwa kwenye wimbo wa "tunajenga kwa pesa zetu"
 
Wabongo tufike mahala tubadilike,barabara za single lane zimepitwa na wakati kujengwa mijini na ni aibu zaidi kwa jiji kuu kama la Dar yaani hata Dodoma imeanza kuepukana na huu ushamba wakati haina traffic jam kama Dar sas hii inashangaza
 
Honestly, this thing looks ugly, kama factory flani hivi., is that a train station ama ni glass all round inawafurahisha., this thing looks ugly for real! Weka inside design nione, maybe it will save face.
Hata mimi nimewaambia wanabisha,hapo ili papendeze labda landscaping ifanyike vizuri maana design yake haifananii na station as if ni cultural site fulani inayohifadhi viboko maana hilo ni u bo la kiboko kama kainamii kwenye maji..sorry nitakaowaudhi ila huu ni ukweli..Pia airport ya dodoma wabadili mapema structural building
 
Yeah still some catch up to do...we are focused on various projects tho..tungekuwa hatuinvest sana Air Tz tungekuwa na cash flow kubwa kuweka hio sector
uwekezaji wa serikali unachekesha,ukisoma majumuisho ya hotuba ya wizara ya ujenzi kwa miaka 5 iliyopita imeongeza paved roads za trunk roads roughly 500km zimekamilika,nyingi ziko hatua mbali mbali za ujenzi but how comes pesa yote inaishia kwenye miradi isiyokuwa na impaccts kubwa kwenye uchumi kama ndege na reli na madaraja ya kukatisha ziwani na baharini wakati mikoa ambayo Jk aliiacha bado haijaunganishwa na lami? Serikali ingewekeza pesa za kutosha kwenye barabara ucchumi na maisha ya watu vingeimarika sana lakini kuongezea train speed kwa pesa ndefu sio dili kabisa
 
Wabongo tufike mahala tubadilike,barabara za single lane zimepitwa na wakati kujengwa mijini na ni aibu zaidi kwa jiji kuu kama la Dar yaani hata Dodoma imeanza kuepukana na huu ushamba wakati haina traffic jam kama Dar sas hii inashangaza

Barabara ni 4 lanes, Upande wa pili ndio unafumuliwa angalia picha Vizuri,napita hapa kila siku ndio maana nimeweka hiyo update. Hii barabara yenye lane mbili ni mpya kabisa haikuwepo, kwa hiyo magari yamehamia lane mpya kulia kupisha kujenga upya lane 2 za zamani. BTW ni mradi unaounganisha Daraja la Selander .
 
WAZIRI MHAGAMA APONGEZA MAFANIKIO YALIYOFIKIWA KATIKA UJENZI KIWANDA CHA BIDHAA ZA NGOZI CHA KARANGA
Matokeo ChanyA+ 1 day mda uliopita OFISI YA WAZIRI MKUU SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU, Waziri Mkuu Acha maoni 132 Imeonekana


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama ametoa pongenzi kwa Jeshi la Magereza na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwa hatua waliyofika katika ujenzi wa kiwanda cha bidhaa za Ngozi cha Karanga.

Akizungumza mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo wa ujenzi wa kiwanda hicho uliopo Moshi, Mkoani Kilimanjaro ambapo hatua za ujenzi umefikia asilimia 97 Waziri Mhagama alieleza kuwa mikakati ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kuendeleza uchumi wa Taifa kupitia Viwanda.
1-01-14.png

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (wa pili kutoka kulia) akiongozana na Wasimamizi wa mradi wa ujenzi wa Kiwanda cha bidhaa za Ngozi kilichopo katika Gereza la Karanga lililopo Moshi, Mkoani Kilimanjaro alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujezi wa kiwanda hicho.

“Mradi huu wa ujenzi wa Kiwanda cha kuzalisha bidhaa za Ngozi hapa Karanga ni mmoja ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati ambayo inatekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano na utakuwa mfano wa kuigwa na mataifa mengine utakapoanza uzalishaji wa bidhaa za Ngozi ambazo zitakuwa zinazalishwa hapa nchini,” alieleza Mhagama.

“Nimeridhika na kasi ya ujenzi wa mradi huu, na nitoe pongezi zangu kwa Jeshi la Magereza linalosimamia ujenzi wa mradi huu kwa kushirikiana na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (PSSSF) hatua mliyofikia kwa kweli ni nzuri,”
Alisema Mhagama Alifafanua kuwa, Kiwanda hicho kitakavyo kamilika mapema kitakuwa na manufaa makubwa kwa taifa ikiwemo kutoa fursa za ajira kwa Watanzania pamoja na kuongeza mapato ya Serikali kupitia bidhaa zitakazokuwa zinazalishwa na kiwanda hicho kuuzwa ndani na nje ya nchi.
2-01-15.png

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akikagua baadhi ya mishine za kuchakata bidhaa za Ngozi alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda hicho.
PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU) OWM-KVAU

Aliongeza kuwa kukamilika kwa majengo manne ya msingi katika kiwanda hicho ina ashiria kuwa hatua iliyobaki sasa ni kusimikwa mitambo ya uchakataji wa ngozi ili kiwanda hicho kiweze kuanza kazi ya uzalishaji haraka.

Aidha, Waziri Mhagama ametoa maagizo kwa Mkurugenzi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma kuhakikisha anasimamia kwa karibu matumizi ya fedha ya mradi huo.
“Ujenzi wa mradi huu umefikia asilimia 97 na matumizi ya fedha yanaridhisha ikionesha kwenye kumbukumbu zenu kuwa kuwa hadi sasa asilimia 63 ya malipo yamekishafanyika, hivyo suala la ‘Value for Money’ limeweza kutekelezwa katika mradi huu,” alisema Mhagama.
3-01-14.png

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akifurahia pamoja na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza muonekano wa majengo mapya ya Kiwanda cha Bidhaa za Ngozi cha Karanga alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo Mkoani Kilimanjaro. Wa pili kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bw. Hosea Kashimba.

Pia Mheshimiwa Mhagama alielezea namna alivyofurahishwa na utekelezaji wa mafunzo ya vitendo sehemu za kazi ambayo yamekuwa ni chachu ya kuwawezesha vijana kukuza ujuzi walionao.

“Katika mradi wa ujenzi wa kiwanda hiki nimefurahi kuona vijana ambao wanataaluma ya uhandisi wameweza kushiriki na kutoa mchango wao katika mradi huu wa muhimu kwa taifa ambao umewawezesha kupata ujuzi na wameonyesha namna walivyojitoa katika kujenga nchi yao,” alisema Mhagama.

Kwa Upande wake Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro, RPO Dkt. Miraji Katumbily alieleza kuwa ujenzi wa mradi huo umefikia asilimia 97 na hatua iliyobaki sasa ni pamoja na kusimikwa kwa mashine ya uchakataji, kuweka miundombinu ya umeme, vifaa vya TEHAMA na kukamilisha ofisi ili uzalishaji katika kiwanda hicho uanze rasmi.

Naye Mkurugenzi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bw. Hosea Kashimba alimuhakikishia Waziri huyo kuwa Ofisi yake kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza nchini kuwa watatekeleza maagizo yote yaliyotolewa ili kuhakikisha mradi huo unakamilika bila kuwa na kasoro zozote.

WAZIRI MHAGAMA APONGEZA MAFANIKIO YALIYOFIKIWA KATIKA UJENZI KIWANDA CHA BIDHAA ZA NGOZI CHA KARANGA - Matokeo ChanyA+
Hii tabia ya stste kufanya biashara haina afya huko baadae ilimshinda nyerer mashirika na viwanda vya umma vilikufa vyote labda wakikamilisha wakibifsishe ila wakisubili wakiendeshe kitakufa itakuwa hasara,biashara na gpa za darasani ni vitu viwili tofauti
 
Barabara ni 4 lanes, Upande wa pili ndio unafumuliwa angalia picha Vizuri,napita hapa kila siku ndio maana nimeweka hiyo update. Hii barabara yenye lane mbili ni mpya kabisa haikuwepo, kwa hiyo magari yamehamia lane mpya kulia kupisha kujenga upya lane 2 za zamani. BTW ni mradi unaounganisha Daraja la Selander .

mtu nchi sio yake ila anajikuta anaumia kuliko wenye nchi wenyewe
 
Hii tabia ya stste kufanya biashara haina afya huko baadae ilimshinda nyerer mashirika na viwanda vya umma vilikufa vyote labda wakikamilisha wakibifsishe ila wakisubili wakiendeshe kitakufa itakuwa hasara,biashara na gpa za darasani ni vitu viwili tofauti

ulitaka afanye nan?
hizi biashara/viwanda za viatu na products za ngozi zimejaa huko dunian.. hakuna ataekuja kujenga huku Africa vipya.. sisi tunajenga kwasababu materials zipo zimejaa tele za kutosha.. baada ya ethiopia sis tunaongoza kuwa na mifugo mingi africa
 
Hii tabia ya stste kufanya biashara haina afya huko baadae ilimshinda nyerer mashirika na viwanda vya umma vilikufa vyote labda wakikamilisha wakibifsishe ila wakisubili wakiendeshe kitakufa itakuwa hasara,biashara na gpa za darasani ni vitu viwili tofauti
Watu wengine km akili ni ziro sasa ww kizuri kwako ni kipi..au wanacho sema wa kenya....upumbavu mwingine bwana....
 
ulitaka afanye nan?
hizi biashara/viwanda za viatu na products za ngozi zimejaa huko dunian.. hakuna ataekuja kujenga huku Africa vipya.. sisi tunajenga kwasababu materials zipo zimejaa tele za kutosha.. baada ya ethiopia sis tunaongoza kuwa na mifugo mingi africa
kikifa kama vingine ndo utajua alitakiwa ajenge nanai uzuri past experience ipo kama hutaki kujifunza hilo suala jingine,wewe unachojua ni hizi simulizi tuu lakini biashara ina protokali zake
Jana nilikuwa naangalia tv mfanyabiashara dodoma analalamika serikali kuwalazimisha kuhamia soko la jipya la ndugai..alisema watu wa maofisini wanaamini sana kwenye maandishi na kompyuta zao sijui aliwaza nini yule jamaa
 
Barabara ni 4 lanes, Upande wa pili ndio unafumuliwa angalia picha Vizuri,napita hapa kila siku ndio maana nimeweka hiyo update. Hii barabara yenye lane mbili ni mpya kabisa haikuwepo, kwa hiyo magari yamehamia lane mpya kulia kupisha kujenga upya lane 2 za zamani. BTW ni mradi unaounganisha Daraja la Selander .
Wa kukurupuka utawajua tu
 
kikifa kama vingine ndo utajua alitakiwa ajenge nanai uzuri past experience ipo kama hutaki kujifunza hilo suala jingine,wewe unachojua ni hizi simulizi tuu lakini biashara ina protokali zake
Jana nilikuwa naangalia tv mfanyabiashara dodoma analalamika serikali kuwalazimisha kuhamia soko la jipya la ndugai..alisema watu wa maofisini wanaamini sana kwenye maandishi na kompyuta zao sijui aliwaza nini yule jamaa
Umeulizwa swali unatakiwa ujibu acha blaa blaa zako za siasa, umeulizwa unataka ajenge nani? Km hao wawekezaji wapo miaka yote na hawajajenga, mifugo imejaa mpk inamwagika, kwahyo tuambie hapa ulitaka ajenge nani usituletee hoja za kina Zitto humu
 
Wa kukurupuka utawajua tu
Achaneni naye huyu ni mfuasi wa ZZK
Ukiisikiliza serikali ya Magu inasema deni ni himilivu na wanatoa mifano kama hii wanayotoa wakenya kuhalalisha ukopaji na kuwashushua wanaotoa tahadhari,sasa kwa kasi ya ukopaji sitashangaa mika mingine 5 ya Magu nchi ikaingia kwenye hali hii kama ya Kenya maana tulikuwa tunaambiwa serikali inajenga kwa pesa zake ikajagundulika kumbe ni mikopo nadhani mnafahamu awamu ya 5 kwa mda mfupi imekopa kuliko awamu yoyote yeyote iliyopita ,kwa hiyo ni mapema sana kuwacheka na kuwa na akiba ya manene kama ilivyokuwa kwenye wimbo wa "tunajenga kwa pesa zetu"
 
uwekezaji wa serikali unachekesha,ukisoma majumuisho ya hotuba ya wizara ya ujenzi kwa miaka 5 iliyopita imeongeza paved roads za trunk roads roughly 500km zimekamilika,nyingi ziko hatua mbali mbali za ujenzi but how comes pesa yote inaishia kwenye miradi isiyokuwa na impaccts kubwa kwenye uchumi kama ndege na reli na madaraja ya kukatisha ziwani na baharini wakati mikoa ambayo Jk aliiacha bado haijaunganishwa na lami? Serikali ingewekeza pesa za kutosha kwenye barabara ucchumi na maisha ya watu vingeimarika sana lakini kuongezea train speed kwa pesa ndefu sio dili kabisa
Umesoma shule gn ww? Mbn unachekesha sn
 
Back
Top Bottom