Baada ya kauli ya Waziri Bashe na TBS kuhusu Mchele wa msaada toka Marekani, nini kinaendelea?

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
617
1,800
cHAKULA.png
Baada ya kuibuka kwa mjadala katika mitandao ya kijamii juu ya mchele ulioongezwa virutubisho ulioletwa Tanzania kutoka nchini Marekani, Hussein Bashe ambaye ni Waziri wa Kilimo alieleza kuwa waagizaji hawakupaswa kuleta mchele huo kwani Tanzania ina hazina ya mchele.

Hata hivyo, muda si mrefu baada ya kauli ya Bashe, Shirika la Viwango Tanzania (TBS) lilisema mchele, mafuta ya vilivyotolewa kama msaada na Marekani chini ya Mpango wa Pamoja Tuwalishe' ni salama kwa Walaji ambapo Taasisi ya Global Communities ikiwa ni sehemu ya Wadau waliohusika katika usambazaji

Swali ni: Je, Mchele huo utaendelea kusambwazwa kwenye shule au zoezi ndio limeishia hapo? Kwani inaonekana hakukuwa na muafaka wa nini kinachoendelea?

========== =============

JamiiForums imefanya jitihada za kupata ufafanuzi kutoka katika mamlaka kadhaa kuhusu hoja hii iliyoulizwa na member wa JamiiForums.com

Shirika la Viwango Tanzania (TBS)

Meneja Uhusiano na Masoko, Gladness Kaseka anasema “Hakuna maelezo mengine ya ziada, kila kitu kipo kwenye lile tamko letu la Machi 17, 2024”

Tamko lilieleza mchele, mafuta ya kupikia ya alizeti na maharage ambavyo vyote vimeongezwa Virutubishi vilivyotolewa na Wizara ya Kilimo ya Marekani kwa ushirikiano na Taasisi ya Jumuiya za Kimataifa (Global communities) kwa baadhi ya Shule za Dodoma, vyote ni salama kwa Walaji.

Alipoulizwa kwamba kwa tamko hilo inamaanisha wametoa ruhusa vyakula hivyo kuendelea kusambazwa shuleni na je, virutubisho vilivyoongezwa vilikuwa na nini vya ziada ambavyo hapa Nchini havipo? Amesema “Kila kitu kipo kwenye tamko letu la Machi 17 hakuna cha ziada”.

Wizara ya Elimu
Mkuu wa Mawasiliano Serikalini Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Sylvia Lupembe amesema “Shule zipo chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI, wao ndio waendeshaji Shule, sisi ni watunga sera, waulize wao.”

Wizara ya Kilimo
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Geofrey Mweli anasema “Vyakula vipo chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI, wao ndio wanaweza kutoa ufafanuzi, Waziri wa Kilimo (Hussein Bashe) anashughulikia usalama wa chakula alitoa ufafanuzi wa mambo mawili.

“Kwanza nchi ipo salama kwa chakula na pili alieleza tumeshawasiliana na Wafadhili kwamba wanapotaka kuleta chakula kwenye shule, wanaweza kufanya uwekaji wa virutubisho hapa nchini.

“Kuhusu Mkataba wa chakula usambazaji wa hiki chakula upo chini ya TAMISEMI.

“Kulikuwa na hoja nyingi mtandaoni ikiwepo madai kuwa chakula hicho kitaondoa nguvu kwa Watoto lakini tayari TBS walitoa ufafanuzi na kuweka sawa.”

TAMISEMI
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini TAMISEMI, Nteghenjwa Hossesh alipoulizwa alisema “Hilo suala ungewauliza wao Wizara ya Kilimo, sina majibu ya moja kwa moja, ngoja nifuatilie.”

Global communities
Alipotafutwa Afisa mmoja wa juu (jina linahifadhiwa) wa Shirika hilo lililohusika kugawa chakula alisema “Mimi sio msemaji wa Shirika, wewe watafute US Embassy ndio watakupa taarifa kwa wao wao ndio walipost, wao ndio wanatakiwa kusema kama wanaendelea kugawa chakula au wamesitisha.

“Mtafute Godfrey Matumu huyu ndiye atakusaidia kukupa majibu, yeye ndiye mtu sahihi wa kukupa majibu hayo.”

Alipotafutwa Godfrey Matumu ambaye ni mmoja wa watendaji wa kuu wa Global Communities, alipoelezwa kuhusu hoja ya Mdau akasema "Nipo kikaoni, nitakutafuta baadaye."

Screenshot 2024-03-25 100905.png


Pia soma:
Hussein Bashe, Waziri wa Kilimo: Waagizaji hawakupaswa kuleta mchele wa Msaada kutoka Marekani kwani Tanzania ina hazina ya mchele

TBS: Mchele, mafuta ya kupikia ya alizeti na maharage kutoka Marekani, ni Salama kwa Walaji
 
Baada ya kuibuka kwa mjadala katika mitandao ya kijamii juu ya mchele ulioongezwa virutubisho ulioletwa Tanzania kutoka nchini Marekani, Hussein Bashe ambaye ni Waziri wa Kilimo alieleza kuwa waagizaji hawakupaswa kuleta mchele huo kwani Tanzania ina hazina ya mchele.

Hata hivyo, muda si mrefu baada ya kauli ya Bashe Shirika la Viwango Tanzania (TBS) lilisema mchele, mafuta ya vilivyotolewa kama msaada na Marekani ni salama kwa Walaji.

Swali ni: Je, Mchele huo utagawiwa kwa wananchi au la?
MGONJWA AKIKATAA UJI HUWA TUNAFORCE ....... TBS wameshaupitisha......

Yaani mwaka 1982 mle mahindi ya msaada kipindi cha njaa mje kukutaaa mchelee leo


ARV zote tuwape mkatae mchele
Vyoo vya shule mara ngapi tumewachimbia leo mje kukaaa mchele hamna nguvu hivyo

Tanzania yatima .....na yatima yadeki .....
 
Baada ya kuibuka kwa mjadala katika mitandao ya kijamii juu ya mchele ulioongezwa virutubisho ulioletwa Tanzania kutoka nchini Marekani, Hussein Bashe ambaye ni Waziri wa Kilimo alieleza kuwa waagizaji hawakupaswa kuleta mchele huo kwani Tanzania ina hazina ya mchele.

Hata hivyo, muda si mrefu baada ya kauli ya Bashe Shirika la Viwango Tanzania (TBS) lilisema mchele, mafuta ya vilivyotolewa kama msaada na Marekani ni salama kwa Walaji.

Swali ni: Je, Mchele huo utagawiwa kwa wananchi au la?
Kwa nini usigawiwe? Kwani vitu haramu vingapi tayari tumeshagawiwa na tumevipokea?
 
Mambo mengine ni ya ajabu, mtu amekaa kasoma vitu mtandaoni anatoka kwenye press kulizungumzia as if yeye ndo board ya udhibiti wa hicho chakula.

Ukiwa kiongozi wa umma lazima uchunge sana kauli zako, hata kama ni mawazo jitahidi usiwaze kwa sauti, maana kuna watu watachukua kama ndo msimamo wa serikali
 
Baada ya kuibuka kwa mjadala katika mitandao ya kijamii juu ya mchele ulioongezwa virutubisho ulioletwa Tanzania kutoka nchini Marekani, Hussein Bashe ambaye ni Waziri wa Kilimo alieleza kuwa waagizaji hawakupaswa kuleta mchele huo kwani Tanzania ina hazina ya mchele.

Hata hivyo, muda si mrefu baada ya kauli ya Bashe Shirika la Viwango Tanzania (TBS) lilisema mchele, mafuta ya vilivyotolewa kama msaada na Marekani ni salama kwa Walaji.

Swali ni: Je, Mchele huo utagawiwa kwa wananchi au la?


Pia soma:
Hussein Bashe, Waziri wa Kilimo: Waagizaji hawakupaswa kuleta mchele wa Msaada kutoka Marekani kwani Tanzania ina hazina ya mchele

TBS: Mchele, mafuta ya kupikia ya alizeti na maharage kutoka Marekani, ni Salama kwa Walaji
TBS wamebebwa tu kutoa kauli. Binafsi,..nasema mimi binafsi, nahisi ni NGO hizo zinazowekwa na wamarekani wameletewa mzigo kuharibu vijana wetu na watoto kwa virutubisho wawe mashoga au wakose uzazi.

Kuna habari za uhakika ubeberu wa magharibi wameapa afrika kusini ya jangwa la sahara tusiruhusiwe kupata maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Eneo letu wamepanga ni eneo la kupatikana mali ghafi za bei bure ili wengine wawe tajiri. Sisi lazima tubakie wajinga maskini na dhaifu.

Hebu fikiri watu hatujatangaza njaa. Wakulima wetu wanalima tunavuna ziada na maghala yamejaa vyakula. Kwanini badala ya kununua kwetu mchele wanataka wao kutupa mchele wa bure?
 
Shule za msingi zilizopokea huo msaada kwa ajili ya lishe zimeambiwa chakula kilichokwisha kuletwa kiliwe kisha baada ya hapo hawatapokea tena. Swali ni je, kama kina madhara kwa nini shehena isiteketezwe badala ya kuruhusu iliyopo iliwe?
 
Waajiriwa wenye kuna siku huwa wanashinda njaa mchana,Itakuwa watoto huko vijijini?

Nchi tajiri husika ina chakula cha ziada,unataka ikupe hela ununue chakula KWA wakulima wa ndani ndio uwape watoto wako masikini.

Halat USA taarifa ya njaa yetu anaijua miaka na miaka.

Wenye hofu na virutubisho,wapewe sample wakaipime kwenye maabara zao ,sio maneno matupu.
 
TBS wamebebwa tu kutoa kauli. Binafsi,..nasema mimi binafsi, nahisi ni NGO hizo zinazowekwa na wamarekani wameletewa mzigo kuharibu vijana wetu na watoto kwa virutubisho wawe mashoga au wakose uzazi.

Kuna habari za uhakika ubeberu wa magharibi wameapa afrika kusini ya jangwa la sahara tusiruhusiwe kupata maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Eneo letu wamepanga ni eneo la kupatikana mali ghafi za bei bure ili wengine wawe tajiri. Sisi lazima tubakie wajinga maskini na dhaifu.

Hebu fikiri watu hatujatangaza njaa. Wakulima wetu wanalima tunavuna ziada na maghala yamejaa vyakula. Kwanini badala ya kununua kwetu mchele wanataka wao kutupa mchele wa bure?
Hapo sasa ni sisi wenyewe kuchagua bu sometimes cheap is expensive
 
Back
Top Bottom