Vipi hakuna binadamu wa mwanzo hahaha,
Je ni lazima kila kitu kilichopo kiwe na mwanzo?
Kila kitu kina mwanzo wake.
Kama kila kitu lazima kiwe na mwanzo wake, Hata huyo Mungu lazima awe na mwanzo wake.
Huyo Mungu hawezi kuwepo tu, from nowhere.
Huyo Mungu haiwezekani atokee tu from nothing.
Kufanya EXEMPTION kwa Mungu asiwe na chanzo, Hiyo ni logical fallacy inaitwa
special pleading fallacy.
nani aliye muumba binadamu?
Binadamu hawaumbwi.
Binadamu wanazaliwa, kwa kuzaliana wenyewe kwa wenyewe.
Hakuna binadamu aliyeumbwa.
Hili swali tayari nilishakujibu lakini bado huelewi.
Kama binadamu hakumbwa vipi afe?
Kufa na kuzaliwa ndio nature(asili) ilivyo.
Hatuwezi kuishi milele kwa sababu kama hatufi, Tutazaliana kwa wingi na kuwa wengi sana duniani, kiasi kwamba hata sehemu za kuishi zitaisha.
Kutakuwa na msongamano mkubwa wa watu na viumbe kiasi kwamba hata huduma za kijamii zitakuwa shida kwa wingi wa watu.
Hivyo ili watu wengine wapate nafasi ya kuishi lazima wengine wafe. Na ndio maana tunakufa ili kuwapatia nafasi viumbe wengine waishi.
unaposema sema binadamu wanaziliana wenyewe hio ni issue ingine kabisa na pia nilisha kuambia hawezi binadamu kupata mtoto kwa shahawa tu bila mkono wa Mungu,
Hii ni logical fallacy ya
non-sequitur.
Unaunganisha vitu viwili tofauti visivyo na uhusiano wowote ule kuunda hitimisho potofu.
Shahawa hazihitaji uwepo wa huyo Mungu. Upatikanaji wa mtoto hauhitaji uwepo wa huyo Mungu.
Ni wewe tu unajaribu kupachika na kufosi
imani zako za huyo Mungu kuzihusisha na shahawa.
Nenda kasome zaidi kuhusu logical fallacies.
wangapi wanawake wanamwagiwa shahawa na wanaume zao na hawawezi shika mimba kwa sababu gani,
Sababu za mwanamke kutoshika mimba zipo nyingi sana.
Kwani hukusoma Biology?
Nenda kasome Biology itafute sababu mbalimbali za kwa nini wanawake hawashiki mimba.
Hakuna
uhusiano wowote wa mimba na uwepo wa Mungu.
narudia tena tulizaliana vipi kama hakuna binadamu wa mwanzo.
Tunazaliana kupitia kujamiiana.
Sexual intercourse.
Kuhusu kuwa tofouti kama sote tumetoka kwa Adamu we labda huelewi genetic drift ndio sababu upo kwenye giza. Binadamu wote tumetoka kwa Adam we endelea kubisha tu.
Unasema binadamu wote tumetoka kwa
Adamu kwa sababu ndivyo ulivyo aminishwa kwenye
Biblia.
Hata mwislamu atakwambia binadamu wote tumetoka kwa
Allah kwa sababu ndivyo alivyo aminishwa na
Quran .
Zote hizi ni
imani mbili zisizo na uthibitisho wowote ule.
Hakuna uthibitisho wala ushahidi wowote ule wa binadamu wa kwanza kuwa ni Adamu.
Kwa hiyo kusema kwamba binadamu wote tumetoka kwa Adamu ni
uongo.
Unajaribu kufosi imani zako za kwenye vitabu vya dini zisizo na ukweli wala uthibitisho wowote ule.
Na hi ardhi au tuseme dunia na mbingu vipi zilijijenga zenyewe au kuna aliye zijenga. Sa aliye zijenga ni nani.
Kama kila kitu lazima kiwe kimefanywa na fulani, Hata huyo Mungu lazima awe amefanywa na fulani.
Kama kila kitu lazima kiwe kimeumbwa, hata huyo Mungu lazima awe ameumbwa.
Mungu huyo haiwezekani atokee tu from nowhere.
Na kama si lazima kwamba kila kitu kilichopo kimeumbwa, Hata ulimwengu na vyote vilivyomo except man-made things, Havijaumbwa na havihitaji muumbaji.