APHFTA: Tutasitisha huduma za NHIF kuanzia saa sita usiku, wagonjwa mahututi tutawaongezea saa 48

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464

Imeelezwa vituo vyote Binafsi vya Afya vitasitisha kutoa huduma kwa Wagonjwa wapya wanaotumia Kadi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)kuanzia Usiku wa Saa Sita kuamkia Machi 1, 2024 huku wale ambao watakuwa katika Uangalizi Maalum (ICU) wakiongezewa muda wa Saa 48 kuendelea kupata huduma.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Vyama vya Watoa Huduma Binafsi za Afya Tanzania (#APHFTA), Dkt. Egina Makwabe ambaye amesisitiza maamuzi hayo yameafikiwa katika kikao chao Bodi ya APHFTA kilichofanyika Februari 29, 2024.

Amesema “Watakaohitaji huduma watalazimika kulipa fedha Taslim kuongezea pale ambapo gharama za kadi zao za bima zinapoishia, wale wa ICU baada ya muda huo tutafanya mchakato wa kuwahamishia Hospitali za Serikali.”

Uamuzi huo umefikiwa baada ya NHIF kufanya maboresho ya Kitita cha Mafao kwa Wanachama wake na kutangaza utekelezaji wake utaanza rasmi Machi Mosi.

Pia soma - Wenye Hospitali binafsi wakataa kuwahudumia wateja wa NHIF kutokana na vifurushi vipya

News Alert: - Hatimaye APHFTA na Hospitali Binafsi zote Warejesha huduma Hospitalini
 
Mwenyekiti wa Vyama vya Watoa Huduma Binafsi za Afya nchini (APHFTA), Dk Egina Makwabe amesema vituo vyote vya afya havitaendelea kutoa huduma kwa wagonjwa wapya wa bima ya NHIF kuanzia Machi 1, 2024.

Dk Makwabe amesema maamuzi hayo yanatokana na kikao cha bodi ya APHFTA kulichokaa mapema leo Februari 29, 2024.

Amesema wataendelea na matibabu kwa wagonjwa waliopo wodini na kwenye uangalizi maalumu (ICU) kwa saa 48.

Hatua ya APHFTA imekuja baada ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kufanya maboresho ya kitita cha mafao kwa wanachama wake na kutangaza utekelezaji wake utaanza rasmi Machi mosi.

Akilizungumzia hilo, Mwenyekiti wa kamati ya kupitia kitita cha mafao cha NHIF cha mwaka 2023, Baghayo Saqware amesema maamuzi ya ujio wa kitita hicho ni matokeo ya makubaliano ya pande zote na ni kwa ajili ya manufaa ya Serikali na sekta binafsi.

Chanzo: ITV
Kwa mantiki hii mwenyekiti wa kamati ya kupitia kitita amedanganya. Maana kama walikubalina APHFTA wasingegoma kuendelea na huduma.
 

Imeelezwa vituo vyote Binafsi vya Afya vitasitisha kutoa huduma kwa Wagonjwa wapya wanaotumia Kadi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)kuanzia Usiku wa Saa Sita kuamkia Machi 1, 2024 huku wale ambao watakuwa katika Uangalizi Maalum (ICU) wakiongezewa muda wa Saa 48 kuendelea kupata huduma.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Vyama vya Watoa Huduma Binafsi za Afya Tanzania (#APHFTA), Dkt. Egina Makwabe ambaye amesisitiza maamuzi hayo yameafikiwa katika kikao chao Bodi ya APHFTA kilichofanyika Februari 29, 2024.

Amesema “Watakaohitaji huduma watalazimika kulipa fedha Taslim kuongezea pale ambapo gharama za kadi zao za bima zinapoishia, wale wa ICU baada ya muda huo tutafanya mchakato wa kuwahamishia Hospitali za Serikali.”

Uamuzi huo umefikiwa baada ya NHIF kufanya maboresho ya Kitita cha Mafao kwa Wanachama wake na kutangaza utekelezaji wake utaanza rasmi Machi Mosi.

Chanzo: ITV


Pia soma - Wenye Hospitali binafsi wakataa kuwahudumia wateja wa NHIF kutokana na vifurushi vipya
Mtaenda kuuwa watu wasio na hatia bure.
Maisha ya sasa kila kitu ni pesa then kuna wafia dini watakwambia pesa sio issue..
 
Daaah hapo wakuumia ni wenye bima, yote kwa yote bora ukate hata bima ya voda ila sio ambayo matibabu yako yahusishe serikali
 
Chama cha wenye hospitali binafsi Tanzania wametangaza kuanza mgomo wa kutowapokea wagonjwa wapya kuanzia leo saa sita kamili usiku, ikiwa ni shinikizo dhidi ya maboresho yaliyofanywa kwenye mfuko wa bima ya afya NHIF.

Juzi Jumanne kwenye taarifa ya Mkurugenzi mkuu wa NHIF Bw. Bernad Konga, alitangaza maboresho kwenye kitita cha mafao kwa wanachama wa mfuko huo na kueleza kuwa utekelezaji wake utaanza kesho machi mosi, 2024.

Leo mara baada ya kumalizika kwa kikao cha baraza la watoa huduma binafsi za afya, Dr Egina Makwabe, mwenyekiti wa chama cha wenye hospitali binafsi amesema kuanzia usiku wa saa sita hawatahudumia wagonjwa wowote wapya wanaofika hospitali za binafsi.

Kuhusu wagonjwa ambao tayari wapo kwenye hospitali na vituo binafsi vya afya, Dr Makwabe amewaambia wanahabari kuwa wataendelea kupata huduma kwa saa 48 pekee na baadae watawahamishia kwenye hospitali za Serikali kuendelea na matibabu yao.

Wakati huo pia Chama hicho cha watoa huduma binafsi za afya kimeitaka Serikali kuitisha mkutano wa pamoja ili kuweza kujadili vyema kuhusu mabadiliko ya kitita cha NHIF kabla ya kuanza utekelezaji wa maboresho yake Katika kujenga hoja zake Chama hicho kinasema mabadiliko ya kitita hicho kitazifanya hospitali nyingi binafsi kufa kifo cha asili, kwani zitashindwa kujiendesha kutokana na kuongezeka kwa gharama za maisha huku gharama za matibabu zikishushwa.

Watoa huduma hao binafsi pia wanalalamika kutokushirikishwa katika maboresho hayo ya kitita cha NHIF, wakiitaka serikali kuzipa nguvu hospitali binafsi badala ya kuzitengenezea mitego ya kufa kutokana na mifumo na miongozo inayowakandamiza Wakati wa kutangaza maboresho hayo yanayotarajiwa kuanza kesho machi mosi,NHIF ilisema lengo la maboresho yake ni kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa kwa wanufaika wa
mfuko na mabadiliko hayo yamelenga kuzingatia maoni na mapendekezo mbalimbali ya wadau wa afya.

Screenshot_20240229_195546_X.jpg
 
Back
Top Bottom