betty marandu
JF-Expert Member
- Apr 4, 2011
- 1,163
- 725
Umejitahid kujib lakini bado nina swali kusema Islam ilikuwepo kabla ya Mohamad hiyo ni uongo mkubwa kuliko yote labda uniambie kitabu kingine chochote zaidi ya quran kinachozungumzia uislam kabla ya Mohamad maana dini zote kabla ya uislam zimezungumziwa hata za kipagan kama Buddha.Kuna watu ni wababaishaji sana na lau wanakutana na watu wasioenda shule au kuijua kidogo historia na mafundishonya dini yao basi watababaika sana na maneno ya huyu kijana PNC. Nakumbuka jina lako kwenye makala ya The. Bold. Lengine nalo kumbuka ulileta ubabaishaji kama huu kisha ukajibiwa na kutulia hapa tena umeleta wa aina nyingine haya subiri ufunzwe nukta moja mpaka nyingine.
Katika vitu visuvyo na shaka ni kua ALLAH ndie mola wa haqi na mwenye kupaswa kuabudiwa sijajua ni kweli hujaona maandiko au unafanya kusudi. Nasema hivi kwa sababu unaonekana unapitia pitia baadhi ya maandiko ya Quran lakini la kushangaza unayafumbia macho yaliyo dhidi yako moja kwa moja kisha unakuja kuuliza. Ok acha tukijibu
Ni kwamba ALLAH ndie yuleyule Mungu wa wayahudi kizazi cha Yaqubu na haya yanathibitisha na Quran 2:132-133
132."Na Ibrahim akawausia wanawe, na pia Yaaqub: Enyi wanangu! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteulieni Dini hii; basi msife ila nanyi mmekuwa Waislamu, wanyenyekevu.
133.Je! Mlikuwapo yalipo mfikia Yaaqub mauti, akawaambia wanawe: Mtamuabudu nani baada yangu? Wakasema: Tutamuabudu Mungu wako na Mungu wa baba zako, Ibrahim na Ismail na Is- hak, Mungu Mmoja tu, na sisi tunasilimu kwake"
Kwa uthibitisho huu swali lako la kwanza litakua limeyeyushwa. Si kitu tena.
Kuna maswali yako hayana msingi na ili yawe na msingi inabidi uyajenge kutokana na maandiko.
Katika kiarabu neno ilaha (إله) lina maana ya chochote kinacho abudiwa. Hivyo neno Al (ال) ni sawa na The katika kingereza na si "a" kama unavyodai wewe. Hivyo maana ya jumla ni "The worshiped one" ikiwa na maana mwenye kuabudiwa.
Umeleta case ya Muhamamad sala na salamu zimfikie amekuja kuuleta uislam na kwamba kabla yake haukuwepo na kusema kwamba ndomana hata baba yake hakua muislam.
Majibu ni kama ifuatavyo
Uislam haujaanzia kwa Muhammad sala na salam zimfikie bali ulikuwepo na tangu awali. Na hili utalijuam ikiwa utaijua maana ya usilam. Uislam ni kujisalimisha kwa Mola mmoja. Kwa maana ya kwamba kumuabudu mola huyo pekee pasi na kumshirikisha na wengine wenye kuabudiwa kinyume chake. Kwa maa a hii ya uislam, uislam upo tangua Adam, Nuhu na wengine waliokuja baada yao. Kwa waarabu Uislam huo ulianzia kutoka kwa Ismail mwana wa Ibrahimu. Kutoka na kurefuka muda miaka mingi kupita mafunzo ya kumuabudu Mola mmoja pekee kwa waarabu yalipotea na badala yake wakawa wanamuabudu hali wakimshirikisha na wenye kuabudiwa wengine ikiwemo Miti, masanamu, mawe n.k kwa mwenye kufanya hivyo uislam hautabakia kwake tena kwani amevunja sharti la kumuabudu ALLAH pekee. Na hilo ndili lililotokea kwa waarabu hivyo mpaka anakuja kuzaliwa baba yake Muhammad mzee Abdullah hali ilikua hivyo.
Ukaja kuunganisha nukta zako kwa kusema ndo maana jeshi la yule mfalme alietaka kuondoa kaaba likaangamizwa na mwenye kaaba.
Maelezo yapo kama ifuatavyo.
Katika vitu vinavyojulisha uislam ni dini ya kale ni uwepo wa nyumba ile tukufu Al kaaba kabla ya kuzaliwa Muhammad sala na salam zimfikie. Kiasili nyumba ile imejengwa na Ibrahim kwa kushirikiana na mwanae Ismail kwa maelekezo kutoka kwa ALLAH. Hili linathibishwa na Quran 2:127 "Na kumbukeni Ibrahim na Ismail walipo inyanyua misingi ya ile Nyumba wakaomba: Ewe Mola Mlezi wetu! Tutakabalie! Hakika Wewe ndiye Msikizi Mjuzi."
Na malengo yametajwa kwenye 2:125
"Na kumbukeni tulipo ifanya ile Nyumba (ya Alkaaba) iwe pahala pa kukusanyikia watu na pahala pa amani. Na alipo kuwa akisimama Ibrahim pafanyeni pawe pa kusalia. Na tuliagana na Ibrahim na Ismail: Itakaseni Nyumba yangu kwa ajili ya wanao izunguka kwa kut'ufu na wanao jitenga huko kwa ibada, na wanao inama na kusujudu."
Kwa kua yeye ndie mmiliki wa nyumba hiyi ndo maana akaihami. Wala kuwepo kwa masanamu hakukufanya umiliki wake usiendelee. Na kama nilivyosema hapo awali kutokana na muda kurefuka miaka mingi kupita mafunzo sahihi yalikua yakipotea sik mpaka sik na hata kufika katika hali ya kumuabudu ALLAH ili hali wakimshirikisha na wengine waliokua wakiwaabudu yakiwemo hayo masanamu.
Sioni msingi wa maswali yako kuhusu kufunga kwa. Kuona mwezi na kufungua kwa kuuona. Kama hautaelewa maelezo yangu hayo uliza tena nikufunze
Pili historia kwenye uislam /quran ni hadithi za kusadikika kiasi kwamba hata wanahistoria hawawezi kuitumia mfano quran inamzungumzia Mariam mamake Yesu ikimfananisha na Mariam ndugu yake Musa na Harun waloishi miaka zaidi ya 1500 kabla.
Kifupi huwezi kwa kutumia quran kuniambia Isa bin Mariam na mamake waliishi miaka ipi kihistoria na waliishi maeneo gani. Quran kusema kuwa kaaba ilijengwa na Ibrahim na Ishmael inaleta walakini maana maandiko ya kabla ya quran, biblia inasema wazi Ishmael na mamake walifukuzwa kwa Ibrahim mapema sana .Kuthibitisha hayo hata Ibrahim amezikwa eneo moja na Sara mkewe.Kifupi historia ya Ishmael kuwa na Ibrahim haiendelei kutajwa baadae.Na kwa uthibitisho zaidi ni kuwa hata kwenye historia ya vizazi vya Ibrahim mpaka wakati wa Yesu wanatajwa wa kizazi kilichotokana na Isaka na siyo Ishmael.
Na zaidi ya hayo umbali kutoka Kanani/Israel mpaka arabuni kwa uzee alokuwa nao Ibrahim na kwa aina ya usafir wa nyakati zake unatia shaka kuwa Quran inaongelea labda Ibrahim mwingine.
Zaidi ya hayo Ibrahim alikuwa nchi ya kanaan na ndo nchi alopewa siyo arabun,swali ilikuwaje akajenge Kaaba arabuni?
Kingine hicho unachozungumzia kuwa kilijengwa na Ibrahim /Kaaba ni kimondo ,walosoma jiografia wanaelewa vizuri sasa kimondo kinajengwa au hudondoka?
Naomba nijibu kwa evidence ili tuweze kuelewa.