A call for Kikwete to resign his presidency

Japokuwa kuzjiuzulu hakuji haraka na wala hatajiuzulu, yet ujumbe wa hii thread ni kuwa hajafikia malengo na matazamio ya wananchi. Kwa anayeweza kusoma katika mistari ya thread ilivyoanza, utajua tu kuwa watanzania wengi hawana tena matumaini na uongozi wa JK na kimsingi ni kuwa serikali iko likizo.

Mfumuko wa bei sasa unaumiza maisha ya watanzania ambao aliwaahidi maisha bora. kauli mbiu ya JK sasa haisemwi popote maana imepoteza maana. Kwa kura zetu, tusikubali tena kumweka madarakani JK hapo mwaka 2010.
Hata hivyo tufikirie namna ya kubadilisha mfumo mzima wa uongozi wa Tanzania ili tufikie malengo.

Mwanadiplomasia huyu anauma na kupuliza pande zote mbili.

Kwa hiyo MWK anatoa kauli za kisiasa za kuonyesha muelekeo? Nakubali kuna kauli za kisiasa za kuonyesha msimamo.Lakini hata serikali ya Tanzania ilipokuwa inalaani ubeberu wa siasa za kibaguzi za makaburu wa Afrika ya Kusini, serikali hii ilikuwa iko katika "Frontline States" na ilikuwa ina makambi ya wapiganaji wa ANC (Kongwa, Magadu, Dakawa etc) ambako condemnations hizi zilikuwa translated into action plans.

Sisi action plan yetu ya kumfanya JK ajiuzulu iko wapi? Au empty rhetoric?
 
Nisaidieni kidogo; ni nchi gani hapa duniani ambako Raisi wake alijiuzulu kwa kushindwa kazi?…

Kujiuzuru tunajua si rahisi sana...

Ninacho jua ni kwamba walau kwa wito na maneno haya yaliyo jaa kila aina ya ukweli, yatamtia shime ageuke na kuirudia kweli ili aweze kukiepuka kikombe cha siki hapo 2010, vinginevyo akae tayari!

Ahsante Rwabugiri.

Hicho ndio kitu watu hawaelewi, nini maana ya mwito wa kujiuzulu.

Kama Wildcard anavyo suggest, inawezekana ni kweli kabisa hakuna Rais aliyewahi kujiuzulu kwa kushindwa kazi, (mi nimepata mmoja tu, Shinzo Abe wa Japan, ambae nae ana utata utata.) Lakini kila siku vilio vya resignation vinasikika duniani kote. Kwa nini? Ni ku make a political statement, kwamba Rais unaharibu. Hicho kitu ma-commentator na ma-political pundits wa hapa hawakielewi, sijui kwa nini.

Hamna mtu mwenye ndoto za Alinacha hapa kwamba eti tutalala tutaamka na kukuta Kikwete kajiuzulu. Isipokuwa, tunaweka shinikizo la kisiasa, tunampelekea ujumbe, kwamba Kikwete unaharibu. Katika ulimwengu wa Siasa hiyo ndio maana ya wito wa kujiuzulu, japo hakuna aliyewahi kujiuzulu kwa kushindwa kazi! Rwabugiri, ahsante kwa upeo wako wa Kisiasa!
 
Ahsante Rwabugiri.

Hicho ndio kitu watu hawaelewi, nini maana ya mwito wa kujiuzulu.

Kama Wildcard anavyo suggest, inawezekana ni kweli kabisa hakuna Rais aliyewahi kujiuzulu kwa kushindwa kazi, (mi nimepata mmoja tu, Shinzo Abe wa Japan, ambae nae ana utata utata.) Lakini kila siku vilio vya resignation vinasikika duniani kote. Kwa nini? Ni ku make a political statement, kwamba Rais unaharibu. Hicho kitu ma-commentator na ma-political pundits wa hapa hawakielewi, sijui kwa nini.

Hamna mtu mwenye ndoto za Alinacha hapa kwamba eti tutalala tutaamka na kukuta Kikwete kajiuzulu. Isipokuwa, tunaweka shinikizo la kisiasa, tunampelekea ujumbe, kwamba Kikwete unaharibu. Katika ulimwengu wa Siasa hiyo ndio maana ya wito wa kujiuzulu, japo hakuna aliyewahi kujiuzulu kwa kushindwa kazi! Rwabugiri, ahsante kwa upeo wako wa Kisiasa!

Kuhani soma juu hapo kuhusu "political statements".A political statement alone is too passive for realists.We need an action plan, not a political statement.

Shinzo Abe hakuwa rais bali PM na haku resign kwa sababu tu watu walimwambia ajiuzulu

From Japan Times

http://search.japantimes.co.jp/cgi-bin/nn20070913a1.html

After less than a year in power, embattled Prime Minister Shinzo Abe said Wednesday he intended to step down to clear the political gridlock created by the ruling coalition's defeat in the House of Councilors in July and to expedite the extension of the controversial antiterrorism law.

Kwa hiyo mambo yalianza na political defeat in the House.Action plan yetu kumfanya Kikwete ajiuzulu kama Shinzo Abe inaweza kuwaiga Wajapani kwa kuanza na a political coup in the Parliament.Then we can even discuss forcing Kikwete out by a vote of no confidence.
 
Shinzo Abe hakuwa rais bali PM na haku resign kwa sababu tu watu walimwambia ajiuzulu

Kwa hiyo mambo yalianza na political defeat in the House.Action plan yetu kumfanya Kikwete ajiuzulu kama Shinzo Abe inaweza kuwaiga Wajapani kwa kuanza na a political coup in the Parliament.Then we can even discuss forcing Kikwete out by a vote of no confidence.

Shinze Abe hakuwa Rais ndio. Lakini "Rais" wa Japan anaitwa "Waziri Mkuu." Rais ikiwa na maana Kiongozi Mkuu wa nchi. Usilete ubishi wa kitoto toto mjomba!

Na kuhusu kujiuzulu kwake, si nilisema kwamba kuna utata kwamba nae unaweza kumuhesabu kama alishindwa kazi au hakushindwa. Nilisha qualify utafiti wangu, kwamba nao una utata. Kwa hiyo Pundit, usilete ubishi wa vijiweni kuharibu mjadala! Sio ushindani hapa!
 
In the interest of preciseness and JF's esteemed commitment to accuracy, kubali umekosea yaishe.Umeandika hivi.

Kama Wildcard anavyo suggest, inawezekana ni kweli kabisa hakuna Rais aliyewahi kujiuzulu kwa kushindwa kazi, (mi nimepata mmoja tu, Shinzo Abe wa Japan, ambae nae ana utata utata.)

Hujasema "Head of Government" aliyewahi kujiuzulu.Umesema rais.Kama kuna mtu anajifunza kutoka forum hii anaweza ku-conclude kwamba Shinzo Abe alikuwa rais wa Japan, kitu ambacho si kweli.

What's next? Utatafuta Waziri na kusema wote wanatoka kwenye executive?

Zaidi ya hapo, hata baada ya kukosolewa unaendelea kung'ang'ania kuwa mimi ndiye mbishi, na kwamba rais ni Waziri Mkuu.Rais ni rais na PM ni PM.

Halafu kama habari ina utata kwa nini unaileta hapa? Research before posting, sio unapost tu ilimradi.

If you do not put a high premium on preciseness and commitment to accuracy, ruhusa kuendelea kubisha.
 
Sisi action plan yetu ya kumfanya JK ajiuzulu iko wapi? Au empty rhetoric?
Action plan mojawapo ni hii hapa MWK aliyoleta kutu convince ya kuwa kuna haja kwa JK ajiuzulu.Pili itakuwa ile ya maandamano kama yale ya Thailand walipomtoa Thaksin.
 
Action plan mojawapo ni hii hapa MWK aliyoleta kutu convince ya kuwa kuna haja kwa JK ajiuzulu.Pili itakuwa ile ya maandamano kama yale ya Thailand walipomtoa Thaksin.

Hii ya kutuconvince is preaching to the choir.Na hata hao wachache wanaopita nje ya jengo kama unataka kuwa convince bila specifics nitawasamehe wasipokuelewa.

Tuleteeni hiyo ya maandamano.Tumeletewa petition idea hapa na jmushi hakuna aliyestep up to the plate. Tumeletewa idea ya kuprotest ubalozini DC the fourth watu wanakwenda kwenye barbecue.

Tupe hiyo plan tuione labda inaweza kuwa na kipya zaidi ya empty highminded rhetoric.
 
Mkuu Pundit

Sisi watanzania ni waoga sana hilo wala lisikupe shida.

Ndivyo tulivyolelewa. Unakumbuka hata kuna kiongozi mmoja alitamka hadharani kuwa watanzania wakale nyasi lakini RAIS apande ndege? Lakini ukichungulia kwa ndani wakati anahimiza wenzake wale nyasi unaweza kukuta alikuwa na mafao ya kutosha, katika dili yenyewe. Lakini pamoja na hayo aliendelea vizuri kuwa kiongozi wetu.

Katika suala hili kinachotakiwa siyo tu aliyoko Mkuu kujiuzulu, hila uongozi mzima unatakiwa kufukuzwa kazi. Assume yale makampuni makubwa mtu anapewa kazi mwaka mzima hakuna maendeleo, kinacho fanyika siyo kujiudhulu huwa ni kufukuzwa kazi.

Serikali ya iliyoko madarakani imekuwepo tangu uhuru kwa kupokezana, wana sera nzuri tu zilizopambwa mithili ya marashi ya pemba, lakini implimentatition yake tanzania ni kati ya nchi masikini duniani.

Kwa jinsi ilivyo tunaweza kuona tatizo siyo maandishi, tatizo ni wasimamia maandishi. Kwa hiyo mpaka sasa Chama tawala hakijaweza kupata mtu wa kusimamia maandishi yake, miaka sijui mingapi.

Kinachotakiwa (Dawa) ni kuwafukuza tu.
 
Mkuu Pundit

Sisi watanzania ni waoga sana hilo wala lisikupe shida.

Ndivyo tulivyolelewa. Unakumbuka hata kuna kiongozi mmoja alitamka hadharani kuwa watanzania wakale nyasi lakini RAIS apande ndege? Lakini ukichungulia kwa ndani wakati anahimiza wenzake wale nyasi unaweza kukuta alikuwa na mafao ya kutosha, katika dili yenyewe. Lakini pamoja na hayo aliendelea vizuri kuwa kiongozi wetu.

Katika suala hili kinachotakiwa siyo tu aliyoko Mkuu kujiuzulu, hila uongozi mzima unatakiwa kufukuzwa kazi. Assume yale makampuni makubwa mtu anapewa kazi mwaka mzima hakuna maendeleo, kinacho fanyika siyo kujiudhulu huwa ni kufukuzwa kazi.

Serikali ya iliyoko madarakani imekuwepo tangu uhuru kwa kupokezana, wana sera nzuri tu zilizopambwa mithili ya marashi ya pemba, lakini implimentatition yake tanzania ni kati ya nchi masikini duniani.

Kwa jinsi ilivyo tunaweza kuona tatizo siyo maandishi, tatizo ni wasimamia maandishi. Kwa hiyo mpaka sasa Chama tawala hakijaweza kupata mtu wa kusimamia maandishi yake, miaka sijui mingapi.

Kinachotakiwa (Dawa) ni kuwafukuza tu.

Katika Africa haijatokea nchi kupata maendeleo kwa kutumia Chama kilicholeta uhuru wa nchi. CCM na TANU au ASP are one so no change. Hata wangepata nani, sera zao zimepitwa na wakati na wanaokiongoza hawana dira ya kutupeleka mbele.

They are always suspicious of anything progressive. Ukiwaambia kuwa hii njia ni mbovu, wao wanaziba masikio, kesho yake yakiwageuka wanabadilika kama kinyonga na kudai wao ndiyo waliogundua huo uovu!
 
Mimi naungana na nyie kwa asilimia mia moja. kikwete hana jpya tena la kuweza kufanya kwa mda aliobakiwa nao hotuba yake ya kwanza bungeni ilijaa matumaini tele lakini sasa hivi hayapo na wala hayaonekani kama yakaa yaje. serikali yake inatumia muda mwingi kujitetea kuliko kufanya kazi. waache wazunguke mbuyu mpaka 2010 tuwateme tushachoka na huu usanii.
 
In the interest of preciseness and JF's esteemed commitment to accuracy, kubali umekosea yaishe.Umeandika hivi.



Hujasema "Head of Government" aliyewahi kujiuzulu.Umesema rais.Kama kuna mtu anajifunza kutoka forum hii anaweza ku-conclude kwamba Shinzo Abe alikuwa rais wa Japan, kitu ambacho si kweli.

What's next? Utatafuta Waziri na kusema wote wanatoka kwenye executive?

Zaidi ya hapo, hata baada ya kukosolewa unaendelea kung'ang'ania kuwa mimi ndiye mbishi, na kwamba rais ni Waziri Mkuu.Rais ni rais na PM ni PM.

Halafu kama habari ina utata kwa nini unaileta hapa? Research before posting, sio unapost tu ilimradi.

If you do not put a high premium on preciseness and commitment to accuracy, ruhusa kuendelea kubisha.

Dude, you nit-pick too much. You like to blow things way out of proportion. Na nadhani wote nyie (wewe na huyo Kuhani Mkuu) mna ubishi wa kijinga kijinga sometimes.
 
Dude, you nit-pick too much. You like to blow things way out of proportion. Na nadhani wote nyie (wewe na huyo Kuhani Mkuu) mna ubishi wa kijinga kijinga sometimes.

Nyani,

Galileo na Copernicus wasinge nit pick dogma za Aristotle na Ptolemy wote tungekuwa tunaamini kwamba vitu vyenye uzito tofauti vinaanguka kwa kasi tofauti na jua linazunguka dunia.

Albert Einstein asinge nit-pick kanuni za mwendo za Newton, asingekuja na kanuni za relativity.

Asingekuja na kanuni za relativity, leo hii tusingekuwa na GPS.

Nitpickers make the world go round, in the case of Copernicus this was very literal!

Sitaki madogo waje hapa kwa kujua kuwa JF kuna watu wa authority kama Kuhani Mkuu halafu kesho wakaquote hapa na kusema "Shinzo Abe alikuwa rais wa Japan"
 
Mwanadiplomasia huyu anauma na kupuliza pande zote mbili.

Kwa hiyo MWK anatoa kauli za kisiasa za kuonyesha muelekeo? Nakubali kuna kauli za kisiasa za kuonyesha msimamo.Lakini hata serikali ya Tanzania ilipokuwa inalaani ubeberu wa siasa za kibaguzi za makaburu wa Afrika ya Kusini, serikali hii ilikuwa iko katika "Frontline States" na ilikuwa ina makambi ya wapiganaji wa ANC (Kongwa, Magadu, Dakawa etc) ambako condemnations hizi zilikuwa translated into action plans.

Sisi action plan yetu ya kumfanya JK ajiuzulu iko wapi? Au empty rhetoric?

sio vibaya kama nitauliza swali hili hiil tena ! jibu lilotolewa sio sahihi (wale waliojaribu kutoa jibu)!
 
Tatizo la nchi sio President pekee ni kila mahali, kwa mawazo yangu yangu tunamlalamikia raisi kuliko uwezo wake. Lawama zinatakiwa kwenda kote kwani Culture iliyopo Tanzania ya rushwa haijaanza leo na haitachukua muda mfupi kuibadilisha.

Kikwete ameruhusu watu kumkosoa na JF ni mfano angalau sasa wananchi wanajua matatizo. Mimi naona tunamlaumu president kupita kiasi.
 
Nyani,

Galileo na Copernicus wasinge nit pick dogma za Aristotle na Ptolemy wote tungekuwa tunaamini kwamba vitu vyenye uzito tofauti vinaanguka kwa kasi tofauti na jua linazunguka dunia.

Albert Einstein asinge nit-pick kanuni za mwendo za Newton, asingekuja na kanuni za relativity.

Asingekuja na kanuni za relativity, leo hii tusingekuwa na GPS.

Nitpickers make the world go round, in the case of Copernicus this was very literal!

Sitaki madogo waje hapa kwa kujua kuwa JF kuna watu wa authority kama Kuhani Mkuu halafu kesho wakaquote hapa na kusema "Shinzo Abe alikuwa rais wa Japan"

Got ya!!!!
 
JK kuresign mmeishia wapi wazee ? naona hamjamaliza kwa jk, mmeanza kwa sitta, kabla ya hapo mlipitia kwa karume...lol...mnanichekesha humu !lol
 
JK is nothing
hata tukaongea vipi, ninalazimika kusema kuwa hakuna changes zitakazotokea kwa kupitia kwa JK
Watanzania tilimtegemea sana huyu JK kwa sera zake tukiona kama huyu ndiye mkombozi wetu, sasa ni tofauti kabisa na yeye ndiye anazidi kutukandamiza

Lakini hii yote nadhani ni kwa sababu JK hakustaili kwa Kazi hii, ila nadhani hii ni sawa na mtu kufanya vitu kwa kubahatisha, JK alifanya vitu kwa kubahatisha na kutafuta jina tu lakini hakuwa tayari kuwasaidia watanzania

Kwa nchi yetu sisi mambo mengi yanakwamishwana Rais (JK) kwani katiba inamruhusu kabisa kufanya mambo mengi, angekuwa ni mtu wa kuwasaidia watanzania, angeshafanya hayo mambo

Kwa JK tutakaa sana mpaka kuja kupata maendelo ya kweli
mkuu mimi nafikiri tulikosea kumpa kazi hii, ila kazi ambayo ingemfaa,ni hii anayoifanya LUNDENGA
 
Niliwahi kusema hapo awali kuwa hakuna jipya kwa Mh. zaidi ya kuendelea kutoa tabasamu lake. Wananchi hawahitaji tabasamu na ukenuaji meno wakati hawana uhakika wa kitoweo cha kesho. Mwananchi wa SUNUKA, KASULU, KIABAKARI, KITAGUTITI au na maeneo mengine utawaambia nini??

Watu walioko karibu na JK ndiyo wanazidi kujineemesha zaidi. SISIEMU yote haifai kabisa kutawala kwa sasa au baadaye. Watanzania wamechoka na wengine walishaanza kukata tamaa kabisa na maisha. Yeye jamaa haonyeshi kushtuka, DOWANS wanaendelea kulamba tu ile $ 152 kila siku.

Mpaka sijui uchunguzi uishe au ripoti ipelekwe bungeni mjadili pamoja na UPUPU wenu wa kila siku pesa itakuwa ilishalambwa kwa sana. Na mnamjua huyo anayelamba, anaharakishiwa malipo yake kwa sababu yuko karibu na MUUNGWANA. JK mie nafikiri unatakiwa kurudi Chalinze ukaendelee na KILIMO cha MANANASI. Hiyo kazi naamini utakuwa makini kwa sababu utakuwa na uchungu na familia yako. Kwa sasa huna uchungu na WATANZANIA, kwani una tabu ya nini....... PENSHENI yako iko online once ukiachia ngazi.
 
Back
Top Bottom