KakindoMaster
JF-Expert Member
- Dec 5, 2006
- 1,356
- 91
Niliwahi kusema hapo awali kuwa hakuna jipya kwa Mh. zaidi ya kuendelea kutoa tabasamu lake. Wananchi hawahitaji tabasamu na ukenuaji meno wakati hawana uhakika wa kitoweo cha kesho. Mwananchi wa SUNUKA, KASULU, KIABAKARI, KITAGUTITI au na maeneo mengine utawaambia nini?? Watu walioko karibu na JK ndiyo wanazidi kujineemesha zaidi. SISIEMU yote haifai kabisa kutawala kwa sasa au baadaye. Watanzania wamechoka na wengine walishaanza kukata tamaa kabisa na maisha. Yeye jamaa haonyeshi kushtuka, DOWANS wanaendelea kulamba tu ile $ 152 kila siku. Mpaka sijui uchunguzi uishe au ripoti ipelekwe bungeni mjadili pamoja na UPUPU wenu wa kila siku pesa itakuwa ilishalambwa kwa sana. Na mnamjua huyo anayelamba, anaharakishiwa malipo yake kwa sababu yuko karibu na MUUNGWANA. JK mie nafikiri unatakiwa kurudi Chalinze ukaendelee na KILIMO cha MANANASI. Hiyo kazi naamini utakuwa makini kwa sababu utakuwa na uchungu na familia yako. Kwa sasa huna uchungu na WATANZANIA, kwani una tabu ya nini....... PENSHENI yako iko online once ukiachia ngazi.
Mkuu naona hii imefika wakati wake