uchaguzi

Uchaguzi Tanzania
Uchaguzi hasa wa viongozi katika nchi ni utaratibu (mchakato) rasmi unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria kuwawezesha wananchi kufanya maamuzi kwa njia ya kuwapigia kura kuwachagua watu ambao wanawataka kuwaongoza kwa kipindi maalum.

Uchaguzi ni utaratibu wa kawaida wa demokrasia wa kuwapata wawakilishi wa kisiasa ambao umekuwa ukitumika tangu karne ya 17. Kuna aina tatu za msingi za uchaguzi zinazotumiwa kuwapata viongozi kulingana na mfumo unaotumiwa na nchi husika.

Aina hizo ni uchaguzi wa Rais, Uchaguzi wa Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Kutunga Sheria na Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Vyama vya Siasa kwa upande wao navyo huendesha chaguzi ambazo zinajulikana kwa jina la “Chaguzi wa Msingi” zinazotumika kuwachagua wateuliwa wa vyama katika aina za uchaguzi ambazo zimetajwa hapo juu.

Endapo Tume haitaridhika kabla ya kutangaza matokeo ya uchaguzi kwamba kulikuwa na kutokufuatwa kwa taratibu, matumizi mabaya au ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi au pale ambapo kura za wagombea waliopata kura za juu imelingana, Tume itasimamisha au kufuta uchaguzi au sehemu yoyote ya uchaguzi na itatangaza siku nyengine ya kurudiwa kwa uchaguzi huo.
  1. S

    Picha: Zitto akiongoza harakati za kupigania uchaguzi huru na wa haki huko nchini Marekani

    "Tumefika salama Toronto, Canada. Tunaendelea na ziara yetu ya kimataifa, kuonana na Watanzania wanaoishi nje ( diaspora) na kuzungumza na Serikali za Nchi hizo na Taasisi za Kimataifa ili kuhakikisha kuwa Uchaguzi wa Tanzania unakuwa Huru, wa Haki na unaoaminika."
  2. GE2020 Je, watanzania watamchagua nani kuwaongoza mwaka huu

    Habri za wakati huu; Nimekuwa nikifuatilia kwa kina mitazamo ya wananchi hasa vijana wa umri kati ya miaka 18 hadi 45 ambao wengi wao ndio wapiga kura watakaoshiriki katika kuamua nani awe rais mwaka huu wa 2020.Kwa fikra na mtazamo wao kwa hakika wanatafuta sana alternative candidate/Mbadala...
  3. J

    Serikali yakataa ombi la CHADEMA la kutaka uchaguzi wa Serikali za Mitaa urudiwe, Waziri Mkuu asema wagombea ndio walipaswa kukata rufaa

    Waziri Mkuu Mh Majaliwa amesema serikali haiwezi kukubali kurudiwa kwa uchaguzi wa serikali za mitaa kama ilivyoombwa na Chadema kwa sababu kila uchaguzi una kanuni na taratibu zake. Majaliwa amesema Wagombea wa Chadema ndio waliopaswa kulalamika na kukata rufaa kwa mujibu wa sheria na sio...
  4. Je, ikitokea Serikali ikakosa fedha za uchaguzi mkuu, Serikali iliyopo madarakani itaendelea kuongoza?

    Kwa wataalamu wa sheria na katiba ,naomba tu kufahamu najua hatuwezi kukosa fedha za uchaguzi hata kidogo lakini je ikitokea tuakakosa kabisa,nini kitatokea? Je, Serikali iliyopo madarakani itaendelea kuongoza wakati muda wake utakua umekwisha, hadi wakati itakapopata fedha za uchaguzi, au...
  5. J

    Mnyika: CHADEMA haitasusia uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba, amuomba Rais Magufuli kupeleka muswada wa Tume huru ya uchaguzi kwa hati ya dharura!

    Katibu mkuu wa Chadema mh John Mnyika amemuomba Rais Magufuli kupitia serikali kupeleka bungeni kwa hati ya dharura muswada wa kuanzisha Tume huru ya uchaguzi. Hata hivyo Mnyika amesema Chadema haitasusia uchaguzi mkuu wa mwezi October ila amewataka wananchi wote kupaza sauti zao kuidai Tume...
  6. Katiba Mpya, Tume huru chini ya CCM ni ndoto ya mchana! Upinzani chukueni hatua

    Ndugu zangu, hizi kelele zisizokoma kila siku za kwamba, tume ya taifa ya uchaguzi haiko huru, katiba tuliyo nayo ni mbovu na kwamba imepitwa na wakati, ni madai ya msingi kabisa. Tumeona uchaguzi ulivyo vurugwa, katiba yenyewe tuliyo nayo inavyo siginwa na watawala, wenye mawazo na mtazamo...
  7. J

    Upinzani wa kweli tuliushuhudia kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 1995 baada ya hapo Wapinzani walichakachuliwa

    Kwa wale tulioshiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 1995 tutakumbuka namna wagombea wa upinzani walivyokuwa makini na wasioyumba. Wagombea wale waliweza kujenga hoja bila matusi wala kejeli hali iliyopelekea hata mwalimu Nyerere kuwasupport katika baadhi ya majimbo likiwemo la Iringa mjini ambapo Dr...
  8. K

    Ahadi za Rais Magufuli kuhusu uchaguzi huru na haki hazitekelezeki, ni ahadi hewa kimazingira

    Hivi karibuni Rais Magufuli alipozungumza na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao pamoja na mambo mengine alitoa ahadi ya kufanyika uchaguzi huru na haki mwaka huu wa 2020 jambo lililoleta mjadala sana kwenye jamii. Hii kauli haitekelezeki kwa sasa. Hakuna mazingira ya kufanyika uchaguzi huru na...
  9. Kama Serikali imepeleka miswada kadhaa kwa hati ya dharula, kwanini isipeleke wa kuundwa kwa Tume huru ya uchaguzi wenye maslahi mapana kwa Taifa?

    Tunafahamu kuwa serikali yetu imekuwa "bingwa" wa kupeleka miswada kadhaa Bungeni kwa hati za dharula, swali kubwa ninalojiuliza hivi sasa ni kuwa kutokana na kilio cha mamilioni ya watanzania wanaotaka Tume huru ya uchaguzi, ni kwanini serikali hii inapata "kigugumizi" cha kupeleka muswada huo...
  10. Ni kwanini Rais Magufuli awaogope wapinzani aliowashinda kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa kwa asilimia 99.9?

    Nimeshangazwa sana na kauli aliyoitoa Rais Magufuli wakati ajihutubia makada wenzie wa CCM kuwa wasibweteke kuwa watashinda kirahisi uchaguzi mkuu ujao, ambao unategemewa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu na akawaeleza makada hao kuwa wapinzani wana mbinu nyingi za wazi na za kificho, kwa hiyo...
  11. Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika atema cheche kuhusu kauli ya Mwenyekiti wa CCM ya uchaguzi kuwa huru na haki

    Hapa ndio utaelewa kwanini Mh Mbowe ameamua John Mnyika awe Katibu Mkuu wa CHADEMA , yaani anatema madini matupu ! Mnyika amesema: "Sasa nifikishe ujumbe tu kwa Rais Magufuli, ambaye amesema yeye, akiwaambia mabalozi kwamba, uchaguzi wa mwaka 2020 utakuwa uchaguzi huru na haki ujumbe wangu kwa...
  12. GE2020 Tunaojiandaa kumpa tena kura Rais Magufuli tukutane hapa

    Ndio ni mwaka wa uchaguzi na ukweli ni kuwa ilani tuliyomkabidhi Dkt. Magufuli imeshakamilika mpaka Leo 1/1/2020 na tuone sasa ipo haja ya kukutana na kujipongeza kwa kazi kubwa aliyofanya maana haikuwa rahisi. Yeye ni mwanadamu yawezekana kuna sehemu alijikwaa na kutukwaza Ila kwa kuwa...
  13. GE2020 Rais Magufuli: Uchaguzi 2020 utakuwa huru na wa haki

    Rais wa Tanzania, John Magufuli amesema Serikali imejipanga kuhakikisha uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba, 2020 unakuwa wa amani, uhuru na haki. Kiongozi mkuu huyo wa nchi amesema utakapofika uchaguzi huo, nchi na taasisi mbalimbali zitakaribishwa Tanzania kushuhudia. Ametoa kauli hiyo leo...
  14. H

    Shilole: Nitagombea ubunge uchaguzi wa mwaka huu

    Mwanamziki nguli wa kimataifa na maarufu na mfanyabiashara mkubwa Tanzania Zena Yusuph Mohamed a.k.a Shilole ametangaza nia yake ya kugombea Jimbo la Igunga ambapo pia ni sehemu alipokulia kwenye uchaguzi Huu wa mwaka 2020.
  15. J

    Kwa sasa hakuna Mpinzani wa kuipigania Tume Huru ya Uchaguzi waliopo wanategemea huruma ya CCM

    Kiukweli kwa hawa wapinzani tulionao Tume Huru ya Uchaguzi itaendelea kuwa ndoto hadi pale CCM itakapotupa JK mwingine wa kuanzisha mchakato wa kutengeneza Katiba mpya. Hakuna namna vyama vya upinzani vitaweza kushinda uchaguzi bila kuwa na Tume huru. Sidhani kama CCM bado ina huruma au bado...
  16. K

    Zitto Kabwe adai kuna mkakati wa kumweka gerezani kabla ya uchaguzi

    Hii nimeitoa kwenye official Twitter page ya Zitto ==== Serikali ya Rais @MagufuliJP wameamua kutengeneza mashtaka ya utakatishaji Fedha dhidi yangu. Ofisi nzima ya TAKUKURU Makao Makuu imehamia Kigoma kubumba Mashtaka. Lengo ni kuhakikisha nakuwa Gerezani wakati wa Uchaguzi. CCM inatapatapa...
  17. J

    Dr. Bashiru: Mbinu na mikakati tuliyotumia kupata ushindi wa 99% kwenye Serikali za mitaa ndizo tutakazotumia uchaguzi mkuu 2020

    Katibu mkuu wa CCM Dr Bashiru amesema kuwa katika uchaguzi mkuu wa Octoba 2020 CCM itatumia mbinu, mikakati na ubunifu ule ule uliotumika kupata ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa. Dr Bashiru amesisitiza kuwa yeyote atakayejipendekeza kugombea udiwani, uwakilishi, ubunge...
  18. GE2020 CHADEMA kupoteza majimbo yafuatayo

    Kimahesabu, CCM ndio washindi wa Uchaguzi Mkuu wa 2020 kabla hata ya mwenda kwenye Box la Kupigia kura. Ushindi huu wa CCM ambao umetokana na utekelezaji kabambe wa miradi mbali mbali chini ya serikali ya awamu ya tano. HESABU ZA KISIASA zinaonesha majimbo yafuatayo ya Upinzani yanakwenda...
  19. Dkt Bashiru: Uchaguzi sio namba uchaguzi ni uamuzi wa umma

    Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally amewakumbusha baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa nchini maana halisi ya uchaguzi ni maamuzi ya Umma si kama ambavyo wamekuwa wakieleza kwa kupotosha kuwa, uchaguzi ni namba. Ameyasema hayo tarehe 13 Januari, 2020 alipokuwa akihutubia...
  20. GE2020 Kuelekea Uchaguzi: Tafadhali wale wanasiasa wote ambao hampendi, mnateseka sana mkikosolewa au mnahisi kuvunjiwa heshima mnapokosolewa, Msigombee!

    Hello Wana JF, Tanzania ni nchi ya vyama vingi tangu 1992! Tulikubaliana wenyewe kwamba tuendeshe nchi yetu kwa taratibu za kidemokrasia kwa kuruhusu mfumo wa vyama vingi. Na kwa mantiki hiyo, kila mtawala anaeapa kwa mujibu wa katiba tuliyonayo anapaswa kuheshimu taratibu tulizojiwelea...
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…