Siwamilele
JF-Expert Member
- Oct 22, 2019
- 288
- 730
Ndugu zangu, hizi kelele zisizokoma kila siku za kwamba, tume ya taifa ya uchaguzi haiko huru, katiba tuliyo nayo ni mbovu na kwamba imepitwa na wakati, ni madai ya msingi kabisa.
Tumeona uchaguzi ulivyo vurugwa, katiba yenyewe tuliyo nayo inavyo siginwa na watawala, wenye mawazo na mtazamo tofauti wanavyo tendewa, kundi la watu wachache linavyo jiona lina haki kuliko watanzania wengine wote!
Kinacho sikitisha ni kwamba, viongozi wa upinzani wamebaki kulalamika tu bila kuchukua hatua kali kukabiliana na hujuma hizi.
Wananchi mtaani wamechoka, lakini hamuwaambii nini cha kufanya?
2015 CUF Zanzibar mlishinda, mkanyang'anywa ushindi mchana kweupe. Wananchi wakasubiri muwaambie chakufanya mkaishia matamko na kutalii duniani, haki ikapotea!
Chaguzi ndogo za marudio mmefanyiwa hujuma za wazi, mmeishia matamko, haki inanyongwa siku zinaenda!
Haya, uchaguzi s/mitaa umekwisha, mmehujumiwa kweli kweli mpaka huruma, ajabu mmerudia yale yale ya kususia/kujitoa kushiriki na sasa mnaenda kuishia matamko!
Jafo (msimamizi wa uchaguzi huo) alijimwambafy hadharani kwamba wapinzani kufanyiwa hujuma kwenye uchaguzi ni jambo la kawaida, mkachukulia poa? Hivi, aliposema wapinzani mkomae kisiasa, mlimuelewaje?
Tuseme nini basi? Kwamba 2020 mnakwenda kwenye uchaguzi kufanya mlicho kifanya kwenye uchaguzi huu?
Mnatashiriki mchakato mzima halafu dakika za mwisho mtajitoa? Halafu?
Kwamba, serikali hii hii ya CCM kuna siku itaamka asubuhi na kuwaambieni kwamba, njooni tuunde tume huru?
Kwamba itasema tu, sasa tubadilishe katiba?
Au mnasubiri tu iseme "sasa kwa hiari yetu tumeamua kufuta uchaguzi uliofanyika kwakuwa haukuwa huru na haki, na sasa tunauandaa upya?"
Au mnasubiri nini hasa!!
Je, mtaishi matamko yenu mpaka lini?
Je, wananchi (nguvu ya umma) wataendelea kuwaamini, kuwavumilia na kusubiri maamzi yenu magumu hata lini?
Siku wakigundua hamna lolote zaidi ya kulialia na kutoa matamko na kuamua kuachana na ninyi itakuwaje?
Mtatumia hekima na busara katikati ya watawala wapumbavu mpaka lini?
Maswali ni mengi mno wacha niishie hapa, lakini niseme tu;
KAMA MNASUBIRI CCM IWAPE KATIBA MPYA NA TUME HURU, NAWASHAURI MUACHE SIASA. MNACHOSHA INGAWA MNAPENDWA.
Tumeona uchaguzi ulivyo vurugwa, katiba yenyewe tuliyo nayo inavyo siginwa na watawala, wenye mawazo na mtazamo tofauti wanavyo tendewa, kundi la watu wachache linavyo jiona lina haki kuliko watanzania wengine wote!
Kinacho sikitisha ni kwamba, viongozi wa upinzani wamebaki kulalamika tu bila kuchukua hatua kali kukabiliana na hujuma hizi.
Wananchi mtaani wamechoka, lakini hamuwaambii nini cha kufanya?
2015 CUF Zanzibar mlishinda, mkanyang'anywa ushindi mchana kweupe. Wananchi wakasubiri muwaambie chakufanya mkaishia matamko na kutalii duniani, haki ikapotea!
Chaguzi ndogo za marudio mmefanyiwa hujuma za wazi, mmeishia matamko, haki inanyongwa siku zinaenda!
Haya, uchaguzi s/mitaa umekwisha, mmehujumiwa kweli kweli mpaka huruma, ajabu mmerudia yale yale ya kususia/kujitoa kushiriki na sasa mnaenda kuishia matamko!
Jafo (msimamizi wa uchaguzi huo) alijimwambafy hadharani kwamba wapinzani kufanyiwa hujuma kwenye uchaguzi ni jambo la kawaida, mkachukulia poa? Hivi, aliposema wapinzani mkomae kisiasa, mlimuelewaje?
Tuseme nini basi? Kwamba 2020 mnakwenda kwenye uchaguzi kufanya mlicho kifanya kwenye uchaguzi huu?
Mnatashiriki mchakato mzima halafu dakika za mwisho mtajitoa? Halafu?
Kwamba, serikali hii hii ya CCM kuna siku itaamka asubuhi na kuwaambieni kwamba, njooni tuunde tume huru?
Kwamba itasema tu, sasa tubadilishe katiba?
Au mnasubiri tu iseme "sasa kwa hiari yetu tumeamua kufuta uchaguzi uliofanyika kwakuwa haukuwa huru na haki, na sasa tunauandaa upya?"
Au mnasubiri nini hasa!!
Je, mtaishi matamko yenu mpaka lini?
Je, wananchi (nguvu ya umma) wataendelea kuwaamini, kuwavumilia na kusubiri maamzi yenu magumu hata lini?
Siku wakigundua hamna lolote zaidi ya kulialia na kutoa matamko na kuamua kuachana na ninyi itakuwaje?
Mtatumia hekima na busara katikati ya watawala wapumbavu mpaka lini?
Maswali ni mengi mno wacha niishie hapa, lakini niseme tu;
KAMA MNASUBIRI CCM IWAPE KATIBA MPYA NA TUME HURU, NAWASHAURI MUACHE SIASA. MNACHOSHA INGAWA MNAPENDWA.