uchaguzi

Uchaguzi Tanzania
Uchaguzi hasa wa viongozi katika nchi ni utaratibu (mchakato) rasmi unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria kuwawezesha wananchi kufanya maamuzi kwa njia ya kuwapigia kura kuwachagua watu ambao wanawataka kuwaongoza kwa kipindi maalum.

Uchaguzi ni utaratibu wa kawaida wa demokrasia wa kuwapata wawakilishi wa kisiasa ambao umekuwa ukitumika tangu karne ya 17. Kuna aina tatu za msingi za uchaguzi zinazotumiwa kuwapata viongozi kulingana na mfumo unaotumiwa na nchi husika.

Aina hizo ni uchaguzi wa Rais, Uchaguzi wa Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Kutunga Sheria na Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Vyama vya Siasa kwa upande wao navyo huendesha chaguzi ambazo zinajulikana kwa jina la “Chaguzi wa Msingi” zinazotumika kuwachagua wateuliwa wa vyama katika aina za uchaguzi ambazo zimetajwa hapo juu.

Endapo Tume haitaridhika kabla ya kutangaza matokeo ya uchaguzi kwamba kulikuwa na kutokufuatwa kwa taratibu, matumizi mabaya au ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi au pale ambapo kura za wagombea waliopata kura za juu imelingana, Tume itasimamisha au kufuta uchaguzi au sehemu yoyote ya uchaguzi na itatangaza siku nyengine ya kurudiwa kwa uchaguzi huo.
  1. Barbarosa

    Kenya kufanya Uchaguzi Mkuu mwingine mwaka huu, Duh!

    Hawa jamaa wanajua kutupa pesa aisee, duh!
  2. J

    GE2020 Matokeo ya Uchaguzi Mkuu 2020 kutangazwa jijini Dodoma

    Tume huru ya Uchaguzi NEC imesema matokeo ya Uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi october mwaka huu yatatangazwa kutokea jijini Dodoma. Source: Habari Leo Maendeleo hayana vyama!
  3. Erythrocyte

    Isaya Mwita ni kikwazo cha CCM kuchota Pesa ya uchaguzi kwenye Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam, ndio chanzo cha kuwekewa zengwe

    Wakuu hii ndio sababu kubwa ya CCM kutaka kumuondoa Meya wa Jiji la Dar es Salaam , hakuna sababu nyingine yoyote ile. Mwita anatuhumiwa kuzuia matumizi ya zaidi bil 5 ambazo ni mgawo kutoka UDART, Je, ni matumizi gani hayo yaliyotakiwa kufanywa na kwanini yamezuiliwa ? Hakuna mwanaccm...
  4. Influenza

    Dar: Vurugu zatokea kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani Jijini Dar cha kuamua hatma ya Meya wa Dar, Isaya Mwita

    Kikao cha Baraza la Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam nchini Tanzania cha kujadili tuhuma zinazomkabili Meya wa jiji hilo, Isaya Mwita kimesimama kwa muda baada ya jina la mjumbe wa Chama cha Wananchi (CUF) kusainiwa wakati hayupo ukumbini. Kikao hicho kinafanyikia ukumbi wa Karimejee jijini...
  5. Abdalah Abdulrahman

    Tathmini ya kisayansi juu ya matokeo ya uchaguzi mkuu Novemba 2020

    Sayansi na Teknolojia vikitumika vizuri vina uwezo wa kutoa majibu ya wakati ujao,uliopo na uliopita kwa uhakika wa asilimia 99.9%. Katika andiko langu hili nitatumia taarifa za kisayansi zilizopo kuweza kutoa matokeo ya uchaguzi mkuu utakaofanyika Novemba 2020. Tathmini hii isitumike...
  6. Kajabila

    GE2020 Kuelekelea Uchaguzi mkuu 2020: Tupe tetesi na maoni yako, unapendekeza nani agombee wapi na nafasi gani?

    Amani iwe kwenu!! Tutumie thread hii kupendekeza wale wanaofaa kugombea 2020, Tetesi za watu watakaogombea Mimi naanza na Dr. Tulia, Huyu dada amekuwa msaada kwetu na jamii ya Wana Mbeya kwa ujumla kwani kawasaidia wakina Mama wengi kupata mikopo yenye riba nafuu na vijana wengi kwenda Shule...
  7. msela wa mbagala

    Mwaka wa uchaguzi umefika, tusishangae sana

    Huu ndo mwaka ambao wanasiasa tutacheza nao draft, mpira na bao. Ni mwaka ambao wanasiasa watabeba ndoo kichwani. Ni mwaka ambao usishangae kumuona mwanasiasa akishinda kijiweni. Ni mwaka ambao ligi za mpira za hovyo nyingi tutaziona. Msishangae sana. Msishangae sana kukutana na mwanasiasa...
  8. A

    GE2020 Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020

    Katika kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020. Je, serikali ina majibu ya kuwaeleza Watanzania ambao mpaka leo vijiji vyao havijapatiwa umeme nini sababu inayochelewesha ili hali kila siku tunahadithiwa kwamba hela zipo tutembee kifua mbele. Vipi mpango wa kunusuru kaya masikini unaendeleaje? Je...
  9. V

    GE2020 Watanzania mwaka 2020 ni mwaka wa uchaguzi mkuu, Tunachagua tena Rais pamoja na wabunge

    Watanzania mwaka 2020 ni mwaka wa uchaguzi mkuu, Tunachagua tena Rais pamoja na wabunge. Ni mwaka ambao una changamoto kubwa sana katika uchaguzi mkuu hususa upande wa visiwani Watia nia ya kugombea nafasi za ubunge wengi wao wamesha jijua kilichobaki tu ni taratibu za kiofisi Wapinzani...
  10. Corticopontine

    Dr. Bashiru Ally: CCM ni chama kinachoongoza kufanya siasa safi za kiungwana na kiustaarabu kitashinda kwa kishindo uchaguzi mkuu

    CCM YAAHIDI KUENDELEA KUHESHIMU MAAMUZI YA UMMA 02 Januari, 2020 Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally amesema kuwa, CCM mwaka 2020 itaongoza siasa safi za uchaguzi, ni mwaka wa kudhihirisha CCM inaongoza siasa safi na kuheshimu maamuzi ya Umma kama ilivyofanya mwaka 2019...
  11. J

    GE2020 Kwa sasa Udiwani na Ubunge ni ajira, tutegemee changamoto kubwa kuelekea uchaguzi mkuu hasa ndani ya CCM

    Tunakumbushana tu kwamba kwa sasa hapa nchini siasa ni ajira hivyo wabunge na madiwani tegemeeni changamoto kubwa kutoka kwa toleo jipya. Ndio hao akina Harmonize, Diamond, Juma Kaseja, Mrisho Mpoto na wengine wengi wanaopiga jalamba muda huu. Changamoto itaikumba zaidi CCM kwani ndio yenye...
  12. Mmawia

    GE2020 Dkt. Bashiru: Wanaotegemea Tume Huru iwape ushindi wanajidanganya! Tume haipigi kura

    Binafsi nimeshindwa kumuelewa kabisa huyu bwana mkubwa wa CCM. Maneno aliyo yaongea na elimu aliyo nayo sidhani kama vinaendana. HOTUBA YA DR. BASHIRU KWA UFUPI CCM inatoa salamu za mwaka mpya 2020, niwahakikishie watanzania kuwa tutaongoza siasa safi,ni mwaka wa kuheshimu maoni na uamuzi wa...
  13. Mzee Mwanakijiji

    GE2020 Ni Mwaka wa Uchaguzi Mkuu 2020: Kuthibitisha au Kutengua Maamuzi ya 2015?

    Mwaka 2020 ni mwaka wa kufanya uamuzi kuhusiana na utawala na mwelekeo wa taifa letu. Huu ni mwaka wa Uchaguzi Mkuu, mwaka wa Uamuzi Mkuu. Watanzania wataitwa kutoa jibu la maswali makubwa mawili. Je, tuendelee na Rais yule yule aliyechaguliwa mwaka 2015 au tufikirie mtu mwingine? Na pili, Je...
  14. Corticopontine

    GE2020 CUF yaapa kuingia Ikulu

    UCHAGUZI WA MWAKA 2020: Chama cha Wananchi CUF chataka mazingira mazuri Chama cha wananchi CUF kimetoa wito kwa Rais John Magufuli kukutana na viongozi wa Vyama vya Siasa ili kuweka mazingira mazuri ya kushiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020. Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Chama cha...
  15. Corticopontine

    Dr. Bashiru Ally ataka maoni ya wananchi kuhusu kuingizwa kwenye ilani ya uchaguzi 2020/2025 ya Chama tajiri na kikongwe zaidi Afrika baada ya ANC

    DKT. BASHIRU AZITAKA KAMATI ZA SIASA ZA WILAYA NA MIKOA KUWASILISHA MAONI 28 Desemba, 2019 Katibu Mkuu wa Chama Chama Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally amezitaka Kamati za Siasa za Wilaya na Mikoa kuwasilisha maoni yao ya namna ya kuboresha maisha ya wananchi kabla ya tarehe 15 Januari, 2020...
  16. Erythrocyte

    CCM kutogawa bure sare za chama kwenye uchaguzi mkuu 2020, wanachama waelekezwa kujinunulia wenyewe

    Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa chama hicho Mh Bashiru Ally , lengo kubwa la mpango huu ni kutunisha mfuko wa chama ili kupata fedha za kugharamia shughuli za chama , utaratibu huu mpya umeleta sintofahamu kwa wanachama na wapenzi wa chama hicho , ambao walitegemea sare hizo kama mavazi...
  17. J

    GE2020 Uchaguzi mkuu 2020 utakuwa mgumu sana kwa CCM na wapinzani wanaweza kutengenezewa mpenyo

    Uchaguzi mkuu wa 2020 utabebwa zaidi na kura za maoni kwa wagombea wa CCM ambao Kamati kuu ndio imeshika mpini. Jaribu kuangalia tafrani zilizoanza kujitokeza za wabunge kugawa pipi kwa wagonjwa mahututi na wengine kwenda kuutimbatimba uwanja wa Sokoine na kuwahamishia maafande wa Magereza...
  18. Bonde la Baraka

    Kama Magufuli ataendelea na Urais baada ya uchaguzi mkuu 2020 nitaacha kazi nikalime

    Kichwa kinajieleza. Mimi ni mtumishi wa umma, niliajiriwa 2015 June. Katika kipindi hiki cha Magufuli nimekopa fedha bank mara 3 kwa malengo tofauti. - Nilikopa 5m. Kwaajili ya ada - Nilikopa 3 kwaajili ya biashara ambayo ilifeli. Ilifeli kwaajili ya mzunguko mdogo (wateja hakuna). Biashara...
  19. J

    Waraka wa Anglican: 2020 ni mwaka wa uchaguzi wananchi itumieni haki yenu ya kikatiba ya Kuchagua na Kuchaguliwa, Msiogope

    Kanisa la Anglikana dayosisi ya DSM limetoa Waraka wa Christmas ambao umeandaliwa na baba Askofu Jackson na kusomwa katika makanisa yote ya dayosisi hiyo. Waraka huo umeelezea mafanikio ya Kanisa katika kuifikisha injili kwa wahitaji na changamoto zilizosalia. Waraka umesema ili uwe kiongozi...
  20. B

    Cecil Mwambe: Nimeshindwa kwenye uchaguzi Mkuu wa CHADEMA kwa kuwa uwanja haukuwa sawa

    Ikiwa ni siku moja imepita tangu kufanyika kwa uchaguzi wa viongozi wa kitaifa wa CHADEMA na viongozi hao kupatikana, aliyekuwa mgombea wa nafasi ya mwenyekiti na kushindwa Mhe. Cecil Mwambe amesema kuwa, ameshindwa kwenye uchaguzi huo kwa kuwa 'uwanja haukuwa sawa'. Amesema "Mhe. Mwenyekiti...
Back
Top Bottom