Kama Serikali imepeleka miswada kadhaa kwa hati ya dharula, kwanini isipeleke wa kuundwa kwa Tume huru ya uchaguzi wenye maslahi mapana kwa Taifa?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,483
30,155
Tunafahamu kuwa serikali yetu imekuwa "bingwa" wa kupeleka miswada kadhaa Bungeni kwa hati za dharula, swali kubwa ninalojiuliza hivi sasa ni kuwa kutokana na kilio cha mamilioni ya watanzania wanaotaka Tume huru ya uchaguzi, ni kwanini serikali hii inapata "kigugumizi" cha kupeleka muswada huo Bungeni?

Tunajua pia kuwa kwa Maelezo ya viongozi wengi wa CCM wanauona upinzani nchini, unapumulia "mashine" na wakati wowote utakufa, sasa sioni kitu kinachowazuia hao CCM wasipeleke muswada Bungeni, wa uundwaji wa Tume huru

Vile vile tunafahamu kuwa kwa mujibu wa matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa, uliofanyika mwishoni mwa mwaka Jana, ambapo chama hicho kikongwe barani Afrika cha CCM kilijizolea ushindi wa kishindo wa asilimia 99.9 na upinzani kwa ujumla wao waliambulia asilimia 0.1 pekee!

Ndipo hapo ninapojiuliza hivi ni kwavipi CCM iuogope sana upinzani nchini, ambao wao wenyewe wanadai kuwa unapumulia "mashine" na wakati wowote kutoka sasa watauzika rasmi?

Mwenye kujua sababu zinazowafanya hao CCM wawe na "mchecheto" mno kupeleka muswada Bungeni wa uundwaji wa Tume huru ya uchaguzi, naomba atujuze
 
Tunafahamu kuwa serikali yetu imekuwa "bingwa" wa kupeleka miswada kadhaa Bungeni kwa hati za dharula, swali kubwa ninalojiuliza hivi sasa ni kuwa kutokana na kilio cha mamilioni ya watanzania wanaotaka Tume huru ya uchaguzi, ni kwanini serikali hii inapata "kigugumizi" cha kupeleka muswada huo Bungeni?

Tunajua pia kuwa kwa Maelezo ya viongozi wengi wa CCM wanauona upinzani nchini, unapumulia "mashine" na wakati wowote utakufa, sasa sioni kitu kinachowazuia hao CCM wasipeleke muswada Bungeni, wa uundwaji wa Tume huru
Mwambie Mnyika apeleke hoja binafsi!
 
Serikali ya CCM kamwe haiwezi kupeleka muswada wowote Bungeni ambao haina maslahi nao. Never. Why would they do that? Harafu hili la kudai Tume Huru ya Uchaguzi halina udharura wowote. Upinzani nao walikuwa na nafasi kubwa ya kuanza movements za kuidai atleast tangu October 2015 lakini hawakufanya hivyo.

In most cases haki huwa haiombwi. Inadaiwa.
 
Serikali ya CCM kamwe haiwezi kupeleka muswada wowote Bungeni ambao haina maslahi nao. Never. Why would they do that? Harafu hili la kudai Tume Huru ya Uchaguzi halina udharura wowote. Upinzani nao walikuwa na nafasi kubwa ya kuanza movements za kuidai atleast tangu October 2015 lakini hawakufanya hivyo.

In most cases haki huwa haiombwi. Inadaiwa.
Sasa kwako wewe unaona ni vyema CCM ikaendelea kuweka pamba masikioni na kutotaka kabisa uundwaji wa Tume huru ya uchaguzi?

Hivi kukitokea umwagaji damu nchini kutokana na kutolewa matokeo yasiyo ya haki, ni nani atalaumiwa?
 
Nyinyi maccm ndiyo kila kukicha mnasema kuwa upinzani nchini imejifia wenyewe.......

Sasa ni kwanini mnashikwa na "mchecheto" wa kupeleka muswada Bungeni wa uundwaji wa Tume huru ya uchaguzi?

Sioni kwanini wapinzani wasubiri serikali ipeleke hoja binafsi ya tume huru ya uchaguzi, ifahamike ccm hawaitaki hiyo tume huru ya uchaguzi. Wapinzani wanatakiwa kila wakiongoea, popote walipo na wakilala watamke tume huru ya uchaguzi. Sioni ccm wakiwafanyia wapinzani kazi ya kupata tume huru. Huo uchaguzi unatakiwa utiwe shombo ya kitaifa na kimataifa kuwa hakuna uchaguzi bila tume huru bali uhayawani. Kama wapinzani watakubali kushiriki uchaguzi huu bila kudai tume huru ya uchaguzi kwa nguvu zote, tutawapuuza.
 
Sasa kwako wewe unaona ni vyema CCM ikaendelea kuweka pamba masikioni na kutotaka kabisa uundwaji wa Tume huru ya uchaguzi?

Hivi kukitokea umwagaji damu nchini kutokana na kutolewa matokeo yasiyo ya haki, ni nani atalaumiwa?

Mkuu ccm hawawezi kuwasadia wapinzani kupata tume huru. Kwenye hili sioni wapinzani wakiwa serious to be honesty.
 
Sasa kwako wewe unaona ni vyema CCM ikaendelea kuweka pamba masikioni na kutotaka kabisa uundwaji wa Tume huru ya uchaguzi?
No. Nachosema ni kwamba hawa watu hawawezi kutoa tu hiyo tume huru kirahisirahisi kwa kelele zetu za social media. Since status quo inawafavor, hawana haraka ya kufanya changes

Wapinzani wana platform ya kuongoza harakati za kuibana Serikali lakini hawafanyi hivyo. Wanakwama wapi?
 
Sioni kwanini wapinzani wasubiri serikali ipeleke hoja binafsi ya tume huru ya uchaguzi, ifahamike ccm hawaitaki hiyo tume huru ya uchaguzi. Wapinzani wanatakiwa kila wakiongoea, popote walipo na wakilala watamke tume huru ya uchaguzi. Sioni ccm wakiwafanyia wapinzani kazi ya kupata tume huru. Huo uchaguzi unatakiwa utiwe shombo ya kitaifa na kimataifa kuwa hakuna uchaguzi bila tume huru bali uhayawani. Kama wapinzani watakubali kushiriki uchaguzi huu bila kudai tume huru ya uchaguzi kwa nguvu zote, tutawapuuza.
Wapinzani wanajua kuwa wao wakipeleka hoja binafsi itatupwa kapuni.......

Kama ujuavyo kuwa Binge lina wabunge wengi wa CCM na kama ujuavyo kuwa wao CCM hawataki hata kuisikia Tume huru ya uchaguzi

Ila kwa Rais iwapo ataipeleka hoja hiyo, ndiyo itapita.........

Vile vile tunachukulia ile kauli yake aliyoitoa kwa mabalozi, alipowa-assure uchaguzi huru na wa haki, ndipo tumaposema kuwa kama kweli Rais wetu aliyaongea hayo toka moyoni mwake, kwa kumwogopa Mungu wetu, basi apeleke muswada Bungeni wa uundwaji wa Tume huru ya uchaguzi
 
Wapinzani wanajua kuwa wao wakipeleka hoja binafsi itatupwa kapuni.......

Ila kwa Rais kuipeleka hoja hiyo, ndiyo itapita

Inatakiwa wapeleke ittupwe, kisha kwenye bunge la ukweli ambao ni wananchi ipigwe kelele kama yote. Kwa hili wapinzani wanachemsha.
 
No. Nachosema ni kwamba hawa watu hawawezi kutoa tu hiyo tume huru kirahisirahisi kwa kelele zetu za social media. Since status quo inawafavor, hawana haraka ya kufanya changes

Wapinzani wana platform ya kuongoza harakati za kuibana Serikali lakini hawafanyi hivyo. Wanakwama wapi?
Wapinzani gani unaowazungumzia?!
 
Back
Top Bottom