jaji mkuu

No Wikipedia entry exists for this tag
  1. Roving Journalist

    Jaji Mkuu wa Tanzania awashukuru wananchi kwa fedha za kukamilisha majengo ya Mahakama Mwanga na Same

    Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma anazungumza kwenye Uzinduzi wa Majengo ya Mahakama za Wilaya ya Mwanga na Same leo Novemba 15, 2022 Nurdin Hassan Babu - Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro Haki siyo lazima upate wewe tu, hata mwenzako akipata haki na wewe unapaswa kukubali. Mwenyekiti...
  2. BARD AI

    Rais wa Afrika ya Kati amfuta kazi Jaji Mkuu aliyekataa kubadili Katiba kuruhusu agombee muhula wa 3

    Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati amemfuta kazi Jaji Mkuu wa Mahakama ya Katiba, Danielle Darlan, na kumuwekea "kizuizi cha kudumu". Agizo la Faustin Archange Touadera linakuja baada ya jaji huyo mwenye umri wa miaka 70 mwezi uliopita kutupilia mbali ombi la chama tawala la kufanyia marekebisho...
  3. Lady Whistledown

    Jaji Mkuu Mstaafu, Chande Othman amewataka majaji wa Mahakama Kuu kumaliza haraka kesi wanazopangiwa, ili kuondoa wasiwasi kwa jamii

    Jaji Mkuu mstaafu, Chande Othman amewataka majaji wa Mahakama Kuu kumaliza haraka kesi wanazopangiwa, ili kuondoa wasiwasi kwa jamii na wao kujiweka huru. Amesema ucheleweshaji wa kesi zikiwamo zenye mvuto huku akiitolea mfano kesi ya wabunge- Halima Mdee na wenzake 18 wanaopinga kuvuliwa...
  4. BARD AI

    Kenya2022 Jaji Mkuu ataja Hoja 9 zitakazoamua mustakabali wa Urais wa Ruto

    Hoja hizo zilizotajwa na Martha Koome, zitaamua Uhalali au Ubatili wa Matokeo ya Urais ni:- 1. Iwapo Teknolojia iliyotumiwa na Tume ya Uchaguzi (IEBC) kwenye Uchaguzi Mkuu ilifikia viwango vya Uadilifu, Uthibitisho, Usalama na Uwazi ili kuhakikisha matokeo sahihi na yanayoweza kuthibitishwa...
  5. JanguKamaJangu

    Jaji Mkuu apata dawa mlundikano mashauri, ashauri majaji wapangiwe idadi ya kesi za kumaliza kwa mwaka

    JAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahimu Juma, amesema kuna haja ya kuweka utaratibu wa kila Jaji wa Mahakama ya Rufani kumaliza idadi fulani ya mashauri kwa mwaka ili kuondoa mlundikano wa mashauri mahakamani. Alitoa kauli hiyo jana wakati wa mkutano wa nusu mwaka wa Majaji wa Mahakama ya Rufani...
  6. chiembe

    Jaji Mkuu, kulikoni mpaka Sasa una majaji wamestaafu wanafanya kazi kwa mkataba? Nchi haina wajuzi wa sheria?

    Namuuliza tu Jaji Mkuu, kulikoni mpaka Leo ana majaji wamestaafu wanapewa mkataba waendelee kuhudumu? Hawa si ndio watakuwa na utii kwa mtu anayewaongezea mkataba? Waende kupumzika SSH ateue watu, wako wengi, na mama anajua kuchagua
  7. Roving Journalist

    Jaji Mkuu atoa angalizo kwa Mahakimu kutojihusisha na siasa na kuhusu makundi ya WhatsApp

    Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma amewaapisha Mahakimu Wakazi wapya 20 na kuwapa angalizo kuhusu matumizi ya mitandao na marafiki wanaowazunguka Prof. Juma ametoa wito huo leo Jumamosi, tarehe 16 Julai 2022, akiwaapisha mahakimu wakazi wapya 20 Jijini Dar es Salaam. Amesema: “Ni wakati...
  8. Kufa c mwiko

    Jaji Dkt. Adam Mambi aheshimu ratiba na majukumu yake, tunaoteseka ni wenye mashauri kwake

    Nianze kwa kukupa pole na majukumu mazito ya kulijenga taifa letu. Mimi kama mwananchi nina maoni au ushauri kuhusu Jaji Dkt. Adam Mambi wa Mahakama Kanda ya Kati DODOMA. Sina shaka hata chembe na utendaji wake nikili wazi tatizo lipo kupanga ratiba za kazi zake, mtu unasafiri kilomita 500...
  9. JanguKamaJangu

    Jaji Mkuu Kenya ataka Kenyatta aondolewe madarakani kwa kukiuka Katiba

    Martha Koome ambaye ni Jaji Mkuu Nchini Kenya anataka Mahakama ya Rufaa ya Kenya kuangiza Rais Uhuru Kenyatta kuondolewa madarakani kwa kukiuka Katiba baada ya kukataa kuwateua majaji sita miongoni mwa 40 walioidhinishwa na Tume ya Huduma za Mahakama (JSC) miaka mitatu iliyopita Pamoja na...
  10. Wababa13

    Kwanini Jaji Mkuu anatumia hii sehemu ambayo Rais ndo huwa anatumia wakati wa hotuba?

    Habari za leo ndugu, jamaa na marafiki. Leo nimewaza nimeona ni vema niwashirikishe na nyie.. hapo aliposimama Jaji Mkuu binafsi huwa namuonaga Rais wa nchi peke yake, hata Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Spika wa Bunge na Katibu Mkuu kiongozi kwa upande wangu sijawahi kuwaona hapo (sijui...
  11. K

    Tanzania tunahitaji Jaji Mkuu mpya kutokana na yanayoendelea kwenye Mhimili wa Mahakama?

    Hatuwezi kuwa na Mahakama ambayo kazi yake inasikilizia Serikali badala ya kufuata sheria. Kesi za msingi zinachukuwa miaka mingi pasipo ulazima. Ni wakati wa huyu Professor kurudi kufundisha na kuokoa huu Muhimili muhumu kwa taifa letu. Lakini ni wakati wa kuwa na Jaji Mkuu ambaye katokana na...
  12. Linguistic

    Jaji Mkuu Kenya, Martha Koome: Mwanaume anayeishi kwenye nyumba inayomilikiwa na mwanamke anahitajika kuthibitisha mchango wake kwenye nyumba hiyo

    Jaji Koome anasema Mwanaume anayeishi kwenye nyumba inayomilikiwa na mwanamke naye anahitajika kuthibitisha mchango wake kwenye nyumba hiyo. Kucheka tu huku ukiwa kwenye nyumba ya mwanamke ukibadilisha chaneli za runinga haiwezi kumpa haki mwanaume kumiliki sehemu ya mali ya mwanamke. Haya...
  13. beth

    Jaji Mkuu: Hakuna mtu yeyote anatakiwa kumwingilia au kumpigia simu Hakimu ambaye kesi fulani ipo mbele yake

    Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma amesema hakuna mtu yeyote anatakiwa kumwingilia au kumpigia simu Hakimu ambaye suala au kesi fulani ipo mbele yake akisisitiza, "Ukiona anakupigia simu ya aina hiyo mpeleke mbele ya Tume ya Utumishi wa Mahakama" Ameeleza hayo katika Hafla ya kuapishwa...
  14. B

    Mihimili ya Kenya wanaiga nchi za ulimwengu wa Kwanza sisi tunaiga mfumo wa Burundi. Jaji Mkuu kamkaripia Rais uteuzi wa Majaji

    Jaji Mkuu wa Kenya amemtaka Mhe. Rais wa Kenya kuheshimu sheria na kite majaji sita wanaohitajika kikatiba. Aidha amesisitiza kuteuliwa kwa majaji wawili walimpinga wakati wa BBI. Hii ni mwendelezo wa uwajibikaji wa Jaji Mkuu kama mkuu wa mihimili. Jaji Mkuu aliyemaliza muda wake itakumbukwa...
  15. S

    2025 Rais Mwanamke, Spika Mwanamke, na Jaji Mkuu mwanamke?

    Ishara zinaonesha kuwa soon mihimili yote mitatu inaweza kuwa chini ya akina mama hodari, kwa sasa wawili washapatikana, watatu atakuwa nani? Namaanisha hii judiciary wingi mbona kama wako rigid and mascular sana, nao si watuletee mwana mama? ili tukamilishe utatu? mzee wa trend reading...
  16. B

    Jaji Mkuu alijumuika Maria Space Dec.20

    Iko recorded katika hoja zilizoongelewa katika Maria Space Dec. 20. Katika maelfu ya wajumbe ya waliokuwapo, Mh. Jaji Mkuu naye alikuwa katika mahudhurio. Kwamba katika maazimio, umuhimu wa kuwahusisha wananchi kwenye kupata tume huru ya uchaguzi na katiba mpya ulizingatiwa mno: "Kwa uhakika...
  17. Erythrocyte

    Kauli ya Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma ni vema ikajadiliwa' ni kuhusu Mitandao ya Kijamii

    MwanaHalisi Digital imemnukuu Jaji Mkuu wa Tanzania akikemea vikali tabia ya baadhi ya watu wakiwemo wanasheria ya kumkosoa Jaji au mwanasheria wa upande mwingine kiasi cha kumtaja kwa jina na picha yake, na wakati mwingine kutaja hadi mahali anakokaa. Amekwenda mbali hadi kufikia kusema , wote...
  18. H

    Hekima inaelekeza Jaji Mkuu kujiuzulu

    Kesi ya Mbowe na wenzake imethibitisha ubovu wa mahakama ya Tanzania. Ni dhahiri chombo hiki si huru na wala hakina uadilifu. Mahakama inashirikiana na mawakili wa Serikali kutoa nyaraka za mahakama kuwapa mashahidi wa upande wa Serikali. Jambo hili limethibitika wazi. Jambo la kushangaza ni...
  19. Abdul Nondo

    Jaji Mkuu Ibrahim Juma ametugeuka sasa anapotaka Magereza yaongezwe nchini

    Mapendekezo yetu siku zote sisi wananchi, Azaki, activists na vyama yapo wazi kabisa sio kuongeza Magereza kila wilaya hapana. Nakumbuka hata wewe Jaji Mkuu umekuwa ukiyapigilia msumari mapendekezo mahususi ya kutatua changamoto ya msongamano wa wafungwa na Mahabusu katika magereza yetu uliwahi...
  20. K

    Jaji Mkuu anapaswa kuomba Magereza yaongezwe au anapaswa kusaidia kupunguza mahabusu Magereza?

    Ukishangaa ya Musa utastaajabu ya firauni, nchi hii tunazidi kupoteana na Kama siyo kupoteana Basi tunazidi kuzama. Unapomsikia Jaji Mkuu akaiomba Magereza yaongezwe lazima ushangae, maana Magereza yaliyopo sasa yamejaa mahabusu. Badala akae na Watumishi wa mahakama wajadili kupunguza mahabusu...
Back
Top Bottom