Jaji Mkuu atoa angalizo kwa Mahakimu kutojihusisha na siasa na kuhusu makundi ya WhatsApp

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,808
11,973
FXxk_k9UsAI1Paa.jpg


Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma amewaapisha Mahakimu Wakazi wapya 20 na kuwapa angalizo kuhusu matumizi ya mitandao na marafiki wanaowazunguka

Prof. Juma ametoa wito huo leo Jumamosi, tarehe 16 Julai 2022, akiwaapisha mahakimu wakazi wapya 20 Jijini Dar es Salaam.

Amesema: “Ni wakati wa kuanza kuchambua marafiki ambao mtabaki nao. Makundi ya WhatsApp ni maeneo yanayoweza kuwavunjia maadili mkaanza kujadili mambo hayatakiwi.”

Amewataka Mahakimu wasijihusishe na masuala ya siasa kwa kusema: “Usifanye mambo au kutoa kauli ambayo mwananchi anaweza kukuhusisha na chama chochote, sababu sio lazima uwe mwanachama inaweza kuwa vitendo vyako, maneno unayosema, nguo unazovaa.”

Amewataka mahakimu wasijihusishe na masuala ya siasa, kwani yamepigwa marufuku na Ibara ya 113 A ya Katiba ya nchi.

“Naomba msome Ibara ya 113 A, ya katiba ambayo inasema itakuwa ni marufuku kwa Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jaji wa Mahakama Kuu, Msajili wa Mahakama ngazi yoyote, hakimu wa ngazi yoyote kujiunga na chama chochote cha siasa, isipokuwa utabaki na haki ya kupiga kura. Hivyo lazima tuelewane,” amesema Prof. Juma.

Katika hatua nyingine, Prof. Juma amewataka Mahakimu kutoahirisha kiholela tarehe za utoaji hukumu au uamuzi.

“Jambo lingine ambalo Mahakimu wamekuwa wakilifanya ambalo wananchi wamekuwa wakilalamika, ni kupanga tarehe ya kusoma hukumu halafu inafika husomi. Unapanga tarehe nyingine, inafika husomi. Wananchi wanakuwa na haki ya kukushuku,” amesema Prof. Ibrahim Juma.
 
Samaki anaoza kuanzia kichwani, hope's my CJ naye ameacha kuwa msikilizaji wa politics zinazotokea pale kwenye center of power;vipi majaji wetu wakaanza kuomba hizi nafasi na kufanyiwa usaili kama watumishi wengine wa umma?
 
Mahakimu wengi nk watumishi wa Mahakama hujiunga na group non aggressive na yasiyo ya kihuni na yasiyo na interest yoyote ya ku-take advantage sababu ya position yake kama mtumishi wa mahakama.

Mfano magroup ya wazazi wanawe wanakosoma au waumini wenzie reliable etc

Sidhani kama threat kubwa sana kwenye hilo.
 
Naomba msome Ibara ya 113 A, ya katiba ambayo inasema itakuwa ni marufuku kwa Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jaji wa Mahakama Kuu, Msajili wa Mahakama ngazi yoyote, hakimu wa ngazi yoyote kujiunga na chama chochote cha siasa, isipokuwa utabaki na haki ya kupiga kura. Hivyo lazima tuelewane,” amesema Prof. Juma.
Heheheee nimecheka sana.

🤣🤣🤣
 
Kuna kitu kipo wazi sana alichokigusia Jaji Mkuu, na nadhani amefanya hivyo akijua nini kinasababisha jambo hilo kutokea. Ukiona Hakimu au Jaji anaahirisha hukumu baada ya kusikiliza muda mreefu sana na yeye mwenyewe kupanga siku ya hukumu, lakini ikifika ile siku anaahirisha basi ujue kuna Mkubwa ameingilia kisiasa.

Na hilo hutokana zaidi na anayeelekea kushindwa kesi kutafuta mbinu za aidha kugeuza hukumu au kupunguza makali ya hukumu. Hayo ni mambo ambayo wananchi yanatusibu na yametuumiza sana.

Kama Jaji Mkuu anayo nia ya kweli ya kukomesha tabia hiyo basi apige marufuku kwa jambo hilo kutokea na kama kuna ulazima wa kuiahirisha kesi basi Haklmu au Jaji aombe rukhusa ya kufanya hivyo kutoka kwake Jaji Mkuu na wahusika wawe na haki ya kuona sahihi yake ikiruhusu kuahirishwa kwa Hukumu.

Pili Jaji Mkuu aunde jopo la ufuatiliaji wa kesi zilizokwisha tolewa hukumu au maamuzi kuwahoji wahusika kama wameridhika na hukumu au la, iwe aliyeshinda au aliyeshidwa.

Ni jambo lililo wazi kabisa kwamba Mahakimu au Majaji wamehusika katika kupunguza au kuongeza uzito wa adhabu stahiki na gharama za kesi kutokana na kuingiliwa na Viongozi wa siasa.
 
Jaji mkuu ameongea inavyopaswa kuwa, lakini uhalisia ni kinyume chake. Toka alipoingia kuwa jaji mkuu na jinsi alivyopata ujaji mkuu, yeye ndio amegeukia kuwa dhaifu kabisa kwa watawala.

Kwa kiwango kikubwa mahakama chini yake, imetumika na wanasiasa wa chama tawala kwa jinsi walivyotaka. Watu wengi wamefungwa kwa kesi za wazi za kubambikiwa.

Na ukweli huo anaujua lakini hana la kufanya aidha kwa hofu ya kusema ukweli, au kulinda ulaji. Kwa sasa watu wengi wamepoteza imani na mahakama kuliko ilivyokuwa hapo awali.

Mahakama kwa sasa imekuwa ni sehemu ya kukomoa watu kuliko kutoa haki.
 
Back
Top Bottom