Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,644
- 218,091
MwanaHalisi Digital imemnukuu Jaji Mkuu wa Tanzania akikemea vikali tabia ya baadhi ya watu wakiwemo wanasheria ya kumkosoa Jaji au mwanasheria wa upande mwingine kiasi cha kumtaja kwa jina na picha yake, na wakati mwingine kutaja hadi mahali anakokaa.
Amekwenda mbali hadi kufikia kusema , wote wanaofanya hivyo wanafahamika na kwamba siku zao zimekwisha.
Hii ni kauli kali mno kutolewa na Jaji Mkuu, ambayo bila shaka imechagizwa na jazba, mimi nilidhani Mh Jaji Mkuu angejaribu kuangalia kufuatilia kisa cha majaji kushutumiwa mitandaoni badala ya kuwapiga mikwara watoa shutuma.
======
JAJI Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahimu Juma amekubali na kuwasajili mawakili wapya 313 katika sherehe ya 65 ya kuwakubali na kuwasajili mawakili wapya iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mawakili hao wanahusisha wanawake 170 na wanaume 143 ambao sasa wafanya idadi ya mawakili kufikia 10,749 kutoka 10,436 mwezi Juni mwaka huu katika orodha ya mawakili nchini.
Tukio hilo limefanyika leo Ijumaa, Desemba 10, 2021 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam ambapo Prof. Ibrahimu Juma amewataka Mawakili hao kuwa na nidhamu na kufikiria mbali zaidi kuliko kusubiri ajira.
Maadili na viwango, hatupaswi kuwa na mawakili wasiokuwa na maadili, kosa moja la wakili linaweza kuzungushwa mitandaoni na kutuchafua na kuchukuliwa kama Tanzania nzima hatuna maadili. Endeleeni kupambana na mawakili vishoka.
Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma amesema, ndani ya mwezi mmoja, baada ya kuanza kazi Kituo Jumuishi cha Temeke, asilimia 38 ya mashauri yaliyofunguliwa na mawakili, “yalirejeshwa kwao, makosa kama kutaja kifungu cha sheria. Majaji tuangalia la kufanya ili tusiwe tunawarudishia tu.”
Huko mitandaoni nawajua mawakili, hata majina yenu ya bandia nayajua na wengine wako ndani ya mahakama, wanamshambulia jaji kwa jina na picha au wakili wa upande wa pili. Tunawafahamu. Siku zao zimekwisha- Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma
Kukosoa hukumu hakuna tatizo. Nitafurahi hukumu zangu kama zitakosolewe, nitajifunza. Lakini saizi mawakili wanawakosoa majaji, mahakimu kwa majina na picha zao, mara anaishi wapi, hii haikubaliki na mawakili wa aina hiyo hawafai kuwa mawakili- Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma
Amekwenda mbali hadi kufikia kusema , wote wanaofanya hivyo wanafahamika na kwamba siku zao zimekwisha.
Hii ni kauli kali mno kutolewa na Jaji Mkuu, ambayo bila shaka imechagizwa na jazba, mimi nilidhani Mh Jaji Mkuu angejaribu kuangalia kufuatilia kisa cha majaji kushutumiwa mitandaoni badala ya kuwapiga mikwara watoa shutuma.
======
JAJI Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahimu Juma amekubali na kuwasajili mawakili wapya 313 katika sherehe ya 65 ya kuwakubali na kuwasajili mawakili wapya iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mawakili hao wanahusisha wanawake 170 na wanaume 143 ambao sasa wafanya idadi ya mawakili kufikia 10,749 kutoka 10,436 mwezi Juni mwaka huu katika orodha ya mawakili nchini.
Tukio hilo limefanyika leo Ijumaa, Desemba 10, 2021 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam ambapo Prof. Ibrahimu Juma amewataka Mawakili hao kuwa na nidhamu na kufikiria mbali zaidi kuliko kusubiri ajira.
Maadili na viwango, hatupaswi kuwa na mawakili wasiokuwa na maadili, kosa moja la wakili linaweza kuzungushwa mitandaoni na kutuchafua na kuchukuliwa kama Tanzania nzima hatuna maadili. Endeleeni kupambana na mawakili vishoka.
Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma amesema, ndani ya mwezi mmoja, baada ya kuanza kazi Kituo Jumuishi cha Temeke, asilimia 38 ya mashauri yaliyofunguliwa na mawakili, “yalirejeshwa kwao, makosa kama kutaja kifungu cha sheria. Majaji tuangalia la kufanya ili tusiwe tunawarudishia tu.”
Huko mitandaoni nawajua mawakili, hata majina yenu ya bandia nayajua na wengine wako ndani ya mahakama, wanamshambulia jaji kwa jina na picha au wakili wa upande wa pili. Tunawafahamu. Siku zao zimekwisha- Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma
Kukosoa hukumu hakuna tatizo. Nitafurahi hukumu zangu kama zitakosolewe, nitajifunza. Lakini saizi mawakili wanawakosoa majaji, mahakimu kwa majina na picha zao, mara anaishi wapi, hii haikubaliki na mawakili wa aina hiyo hawafai kuwa mawakili- Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma