Kauli ya Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma ni vema ikajadiliwa' ni kuhusu Mitandao ya Kijamii

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,644
218,091
MwanaHalisi Digital imemnukuu Jaji Mkuu wa Tanzania akikemea vikali tabia ya baadhi ya watu wakiwemo wanasheria ya kumkosoa Jaji au mwanasheria wa upande mwingine kiasi cha kumtaja kwa jina na picha yake, na wakati mwingine kutaja hadi mahali anakokaa.

Amekwenda mbali hadi kufikia kusema , wote wanaofanya hivyo wanafahamika na kwamba siku zao zimekwisha.

Hii ni kauli kali mno kutolewa na Jaji Mkuu, ambayo bila shaka imechagizwa na jazba, mimi nilidhani Mh Jaji Mkuu angejaribu kuangalia kufuatilia kisa cha majaji kushutumiwa mitandaoni badala ya kuwapiga mikwara watoa shutuma.


Majaji_wa_michongo..jpg


======


JAJI Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahimu Juma amekubali na kuwasajili mawakili wapya 313 katika sherehe ya 65 ya kuwakubali na kuwasajili mawakili wapya iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Mawakili hao wanahusisha wanawake 170 na wanaume 143 ambao sasa wafanya idadi ya mawakili kufikia 10,749 kutoka 10,436 mwezi Juni mwaka huu katika orodha ya mawakili nchini.

Tukio hilo limefanyika leo Ijumaa, Desemba 10, 2021 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam ambapo Prof. Ibrahimu Juma amewataka Mawakili hao kuwa na nidhamu na kufikiria mbali zaidi kuliko kusubiri ajira.

Maadili na viwango, hatupaswi kuwa na mawakili wasiokuwa na maadili, kosa moja la wakili linaweza kuzungushwa mitandaoni na kutuchafua na kuchukuliwa kama Tanzania nzima hatuna maadili. Endeleeni kupambana na mawakili vishoka.

Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma amesema, ndani ya mwezi mmoja, baada ya kuanza kazi Kituo Jumuishi cha Temeke, asilimia 38 ya mashauri yaliyofunguliwa na mawakili, “yalirejeshwa kwao, makosa kama kutaja kifungu cha sheria. Majaji tuangalia la kufanya ili tusiwe tunawarudishia tu.”

Huko mitandaoni nawajua mawakili, hata majina yenu ya bandia nayajua na wengine wako ndani ya mahakama, wanamshambulia jaji kwa jina na picha au wakili wa upande wa pili. Tunawafahamu. Siku zao zimekwisha- Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma

Kukosoa hukumu hakuna tatizo. Nitafurahi hukumu zangu kama zitakosolewe, nitajifunza. Lakini saizi mawakili wanawakosoa majaji, mahakimu kwa majina na picha zao, mara anaishi wapi, hii haikubaliki na mawakili wa aina hiyo hawafai kuwa mawakili- Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma

 
J
MwanaHalisi Digital imemnukuu Jaji Mkuu wa Tanzania akikemea vikali tabia ya baadhi ya watu wakiwemo wanasheria ya kumkosoa Jaji au mwanasheria wa upande mwingine kiasi cha kumtaja kwa jina na picha yake , na wakati mwingine kutaja hadi mahali anakokaa .
Jaji Mkuu yuko SAWA, hao WANAWASHAMBULIA hivyo na yeye anayo haki ya KUWASHAMBULIA kwa mkwara mzito na hata ikibidi KWA VITENDO. Kama wana hoja waende huko kwenye mfumo wao wa Mahakama waitafute haki yao. Siyo kufanya mambo kama watu ambao hawakusoma.
 
MwanaHalisi Digital imemnukuu Jaji Mkuu wa Tanzania akikemea vikali tabia ya baadhi ya watu wakiwemo wanasheria ya kumkosoa Jaji au mwanasheria wa upande mwingine kiasi cha kumtaja kwa jina na picha yake , na wakati mwingine kutaja hadi mahali anakokaa .
Wote wanaofanya hivyo wanafahamika na kwamba siku zao zimekwisha .haya mambo kumbe bado yapo
 
MwanaHalisi Digital imemnukuu Jaji Mkuu wa Tanzania akikemea vikali tabia ya baadhi ya watu wakiwemo wanasheria ya kumkosoa Jaji au mwanasheria wa upande mwingine kiasi cha kumtaja kwa jina na picha yake , na wakati mwingine kutaja hadi mahali anakokaa .

Amekwenda mbali hadi kufikia kusema , wote wanaofanya hivyo wanafahamika na kwamba siku zao zimekwisha .


View attachment 2039314




Hii ni kauli kali mno kutolewa na Jaji Mkuu , ambayo bila shaka imechagizwa na jazba , mimi nilidhani Mh Jaji Mkuu angejaribu kuangalia kufuatilia kisa cha majaji kushutumiwa mitandaoni badala ya kuwapiga mikwara watoa shutuma
CJ wetu siyo mtu makini na ile nafasi aliipata kwa itikadi ya ukanda wakati wa Magufuli. Japo ni mtu mwema kama binadamu na mwalimu mzuri wa sheria, lakini kuwa CJ ni mzigo mkubwa sana kwake
 
Halafu watu wanashangaa kwanini cdm hawakwenda mahakamani baada ya uchafuzi Mkuu wa 2020. Jaji mkuu ndio huyo anatishia watu kuongea mtazamo wao kwenye uhuni unaoendelea mahakamani. Bila machafuko na kuonyeshana makali, sioni mifumo yetu ikirudi kwenye njia sahihi.
 
MwanaHalisi Digital imemnukuu Jaji Mkuu wa Tanzania akikemea vikali tabia ya baadhi ya watu wakiwemo wanasheria ya kumkosoa Jaji au mwanasheria wa upande mwingine kiasi cha kumtaja kwa jina na picha yake , na wakati mwingine kutaja hadi mahali anakokaa .
Huyu hafai kuwa Jaji mkuu anatakiwa kuwa magereza kwa maovu yanayofanyika nchini
 
Back
Top Bottom