JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,314
- 5,478
JAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahimu Juma, amesema kuna haja ya kuweka utaratibu wa kila Jaji wa Mahakama ya Rufani kumaliza idadi fulani ya mashauri kwa mwaka ili kuondoa mlundikano wa mashauri mahakamani.
Alitoa kauli hiyo jana wakati wa mkutano wa nusu mwaka wa Majaji wa Mahakama ya Rufani uliofanyika mjini hapa, akibainisha kuwa mahakama haijaweka kiwango, bali unatumika utaratibu wao wa muda mrefu tangu mwaka 1979, yaani miaka 43 iliyopita.
Alisema, utaratibu huo hufanyika kila kinapoketi kikao cha Mahakama ya Rufani kinapaswa kumaliza mashauri yote yanayopangwa katika kikao husika isipokuwa kama kuna sababu zisizozuilika za kutokumaliza shauri husika ambapo pia hawakufikia malengo.
Alisema takwimu zinaonyesha kuwa Mahakama ya Rufani ina mashauri ya muda mrefu 611 na mashauri 42 yanayosubiri kusomwa hukumu yaliyozidi siku 90.
Alisema vigezo vya kupunguza mlundikano wa mashauri mahakamani vinalenga kushusha mlundikano hadi asilimia 0.05 ambapo tayari wamefanikiwa kushusha kwa asilimia 0.15 na kwamba lengo kuu ni shauri liwe mahakamani ndani ya siku 350.
Alisema wako vizuri katika kutekeleza hilo, sasa shauri linadumu mahakamani kwa wastani wa siku 338.
Jaji wa Mahakama ya Rufani, Augustine Mwaliga, alisema kikao hicho kimefanyika mwaka huu baada ya kutokufanyika kwa miaka miwili mfululizo iliyosababishwa na janga la UVIKO-19.
Source: Nipashe
Alitoa kauli hiyo jana wakati wa mkutano wa nusu mwaka wa Majaji wa Mahakama ya Rufani uliofanyika mjini hapa, akibainisha kuwa mahakama haijaweka kiwango, bali unatumika utaratibu wao wa muda mrefu tangu mwaka 1979, yaani miaka 43 iliyopita.
Alisema, utaratibu huo hufanyika kila kinapoketi kikao cha Mahakama ya Rufani kinapaswa kumaliza mashauri yote yanayopangwa katika kikao husika isipokuwa kama kuna sababu zisizozuilika za kutokumaliza shauri husika ambapo pia hawakufikia malengo.
Alisema takwimu zinaonyesha kuwa Mahakama ya Rufani ina mashauri ya muda mrefu 611 na mashauri 42 yanayosubiri kusomwa hukumu yaliyozidi siku 90.
Alisema vigezo vya kupunguza mlundikano wa mashauri mahakamani vinalenga kushusha mlundikano hadi asilimia 0.05 ambapo tayari wamefanikiwa kushusha kwa asilimia 0.15 na kwamba lengo kuu ni shauri liwe mahakamani ndani ya siku 350.
Alisema wako vizuri katika kutekeleza hilo, sasa shauri linadumu mahakamani kwa wastani wa siku 338.
Jaji wa Mahakama ya Rufani, Augustine Mwaliga, alisema kikao hicho kimefanyika mwaka huu baada ya kutokufanyika kwa miaka miwili mfululizo iliyosababishwa na janga la UVIKO-19.
Source: Nipashe