ccm

Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndicho chama tawala nchini Tanzania na chama cha pili kwa muda mrefu zaidi barani Afrika, baada ya Chama cha True Whig cha Liberia. Kilianzishwa mwaka 1977, baada ya kuunganishwa kwa Tanganyika African National Union (TANU) na Afro-Shirazi Party (ASP) cha Zanzibar.
  1. Abdul Said Naumanga

    JamiiForums Tanzania Je, Makonda kuteuliwa kama mkuu wa mkoa kutoka kuwa katibu wa halmashauri kuu CCM taifa (itikadi na uenezi) amepanda cheo ama ameshuka?

    Baada ya Makonda kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha leo hii, kumeibuka maswali na mijadala mbalimbali ikiwemo, Je amepanda cheo ama ameshuka?. Hapa nitajitahidi kieleza kadiri ya ninavyo fahamu. Ipo hivi, katika mfumo wa utawala wa Tanzania, Mkuu wa Mkoa ni mwakilishi wa Rais katika mkoa na...
  2. G

    JamiiForums Tanzania Rais Samia anataka mtu wa namna gani kwenye nafasi ya Uenezi wa CCM?

    Tangu mama awe mwenyekiti wa ccm taifa ameteua na kiwatengua watu 4 kwenye nafasi ya uenezi. 1. Alimtengua Humphrey Polepole. Mtu mwenye akili na uwezo mzuri wa ku -connect na hadhira anapozungumza 2. Alimteua na kumtengua Abdul Shaka (mpwa wake kabisa). 3. Alimteua na kumtengua Sophia Mjema...
  3. Jaji Mfawidhi

    JamiiForums Tanzania PreGE2025 CCM ndio hii, angalia anguko lake! Fomu ya Urais iuzwe Milioni 200!

    1. Je, katika kumpata mgombea wake wa Urais kwa muhula wa pili, CCM inataka kurudi kwenye utaratibu wake uliokuwa ukitumika wakati wa mfumo wa chama kimoja ? 1.1 Wakati wa uchaguzi chini ya mfumo wa chama kimoja (1965, 1970, 1975 & 1980) Rais JK Nyerere hakuwahi kujaza fomu ya kugombea Urais...
  4. Ndata

    JamiiForums Tanzania Mbowe kijana wa CCM kwa kivuli cha upinzani

    CCM kama chama dola nchini Tanzania kimefanikiwa sana kujitengenezea upinzani wake na wapinzani wake ambao kwa uhalisia nao ni Ccm nje ya Ccm. Mmoja wao ni Mbowe na chama chake cha Chadema. Historia inatuambia, waanzilishi wote wa Chadema walikuwa Benki kuu. Yaani Mtei, Bob Makani na Mbowe na...
  5. Mjanja M1

    JamiiForums Tanzania Picha: Vyombo vya CCM

    Maandalizi yameshaanza.
  6. mangikule

    JamiiForums Tanzania Nini kitakachowafanya CCM washinde 2025?

    Chama ambacho kimewapeleka wapiga kura wake kuzimu kwa kuwahadaa mengi ya uongo: Chama ambacho kimeruhusu raslimali za Nchi ziuzwe na kugawiwa hovyo kwa wageni bila utaratibu na wakati mwingine utaratibu fichi wizi kabisa. Rejea 1. DP world Kugawiwa bandari zote na kufukuza wafanyakazi kama...
  7. Kipenzi Changu

    JamiiForums Tanzania Asilimia 100 hujifichia CCM kutenda maovu na haramu

    Kama hujagundua hili bado wewe hufikirii sawasawa. Watu wote hupenda kuwa CCM na kupigania kupata nafasi zaidi na zaidi kama sehemu salama ya kujifichia maovu na haramu. Hii inahusu viongozi wote kuanzia juu mpaka chini. Kuanzia mwenyekiti wa shina mpaka namba moja. Chunguza hilo bila kutumia...
  8. Kaka yake shetani

    JamiiForums Tanzania Viongozi wa CCM wengi wameacha kutumia JF ukilinganisha kipindi cha nyuma? Sababu ni uwoga

    Miaka ya nyuma JF inaanza kulipamba sana viongozi wa CCM wengine mpaka wakawa wanajinadi kwa wafanyao na kutoa mawazo ya kiutendaji. Ila mambo yamebadilika kama wanao kuwepo hapa JF ni wachache au wamebadilisha ID ambazo kwamtazamo zinaonesha ni watu wa ovyo ID mpya. Tatizo ni uwoga hapa JF...
  9. Inside10

    JamiiForums Tanzania Uhamiaji: Dereva na V8 Iliyobeba wahamiaji Haramu 20 wa Ethiopia Isihusishwe na CCM

    Baada ya Dereva Mtanzania Edward Erihard (31) Mkazi wa Dodoma kukamatwa akiwa amebeba Wahamiaji 20 Raia wa Ethiopia katika gari aina ya Land Cruiser V8 likiwa na bendera ya Chama cha Mapinduzi CCM katika eneo la Minjingu mkononi Manyara, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji Mkoani Manyara Philon...
  10. M

    JamiiForums Tanzania PreGE2025 LGE2024 Ya uchaguzi wa 2019 na 2020 yamejirudia uchaguzi wa marudio wa madiwani. Tutarajie uchaguzi mbovu tena 2024 na 2025

    Hakika nimeukumbuka uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu 2019 na 2020 jinsi Rais magyfuli, CCM tume ya uchaguzi na vyombo vya ulinzi na usalama vilivyo uvuruga uchaguzi ule mpaka wahusani wetu wa nje wakakata misaada na mikopo kutokana na uchaguzi kuwa wa vurugu na mateso makubwa kwa...
  11. Nyendo

    JamiiForums Tanzania Asafirisha wahamiaji 20 kwa V8 yenye bendera ya CCM

    Mtanzania Edward Erihard (31) Mkazi wa Dodoma anashikiliwa na Polisi Mkoani Manyara kwa kosa la kusafirisha kinyume na sheria Wahamiaji 20 Raia wa Ethiopia. Akiongea Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Manyara ACP Lucas Mwakatundu amesema tukio hilo limetokea March 23 2024 ambapo gari hilo...
  12. technically

    JamiiForums Tanzania CHADEMA na CCM zote hakuna kitu. Uchaguzi wa mwaka huu 2024 na 2025 watu watachagua nini?

    Niseme tu ukweli toka amefariki Rais Magufuli nchi imepoa kisiasa hakuna hoja kabisa. Chadema chini ya Mbowe chama kimejifia kabisa. Hakuna sera wala mikakati ya kuwasaidia Watanzania nao wengi wao mamegeuka kama mafisadi ya nchi hii. Wamewekeza kwenye biashara wanavuna Mbowe anaomba misamaha...
  13. K

    JamiiForums Tanzania Ushindi wa kishindo uliopata CCM kwenye uchaguzi mdogo ni ishara ya kukubalika Kwa Rais Samia. Upinzani ujipange kweli kushindana na CCM ya Samia

    Kunapofuka Moshi moto unawaka na dalili ya mvua ni mawingu, wahenga walisema. Rais Samia anakubalika, anapendwa na anahitajika mno na watanzania na watanzania watafanya juu chini kumheshimisha. Nasema haya Sasa ili kukae tukijua kwenye akili zetu kwamba CCM ni jabali. Tumeshuhudia ushindi wa...
  14. J

    JamiiForums Tanzania Maajabu ya Upinzani Tanzania: CHADEMA wanashangilia ACT kuibiwa kura na CCM

    Kuna chaguzi ndogo zilizofanyika katika maeneo mbalimbali nchini, na Chadema waliamua kutoshiriki, ACT wao wakafanya maamuzi yao kama chama huru cha siasa kushiriki, ACT wamelalamika na kusema kuna ukiukwaji mkubwa wa taratibu za uchaguzi zimefanyiwa kwenye chaguzi hizo. Maajabu ni kuwa...
  15. Melvine

    JamiiForums Tanzania Tatizo sio CCM na wala tatizo sio mchakato wa uchaguzi yaani upigaji kura, tatizo ni wapiga kura wa vyama hivyo vya upinzani

    Unapozungumzia Demokrasia ni ile hali ya mtu kuchagua au kuchagulia, fairness, ulingo sawa wa kufanya shughuli za kisiasa, vyama kuwa na mchakato wa ndani wa kutafuta wawakilishi wao katika nafasi mbali mbali za uwakilishi katika levo tofauti tofauti za chaguzi. Demokrasia ni uwanja mpana na...
  16. MamaSamia2025

    JamiiForums Tanzania PreGE2025 Arusha mjini CCM twende na nani kwenye ubunge 2025?

    2025 iko pale kwenye kona je, wapiga kura wa Arusha mjini tumeshatafakari wa kwenda naye kwenye uchaguzi dhidi ya Godbless Lema. Huko CHADEMA inajulikana kuwa ni mgombea wao wa Ubunge ni Lema. Mchakato wao wa kumpata mgombea Ubunge huwa ni kiini macho tu. Tayari mgombea wao ni Lema na hata yeye...
  17. Jaji Mfawidhi

    JamiiForums Tanzania Tetesi: CCM Kilimanjaro imepasuka, Mkoa unazidi kurudi nyuma

    WAsalaam,Kwa wajumbe wa halmashauri kuu ya wilaya, hebu jadilini pale old CCM. Mji wa Moshi ni mchafu na haukui sababu kubwa ni CCM kukamata, kushikilia na kuhodhi maeneo muhimu ya mji ambapo ni kwaajili ya ukuaji wa mji. Sehemu zote huwa wanweka vibanda vsivyo elewekw, kuzungushia ma-fremu...
  18. Mto Songwe

    JamiiForums Tanzania Vyama vya upinzani vinaoneana wivu, ni nani mwenye urafiki na upinzani kwa CCM?

    Vyama vya upinzani vya Tanzania ni kama wapo kwenye league ya kuoneana wivu. Ni chama gani chenye urafiki na ushindani kwa chama tawala CCM, hii ni toka utawala wa Samia uanze. Hali hii inanishangaza sana.
  19. tpaul

    JamiiForums Tanzania Dr Nkwasi: CCM hawana jipya, wanatafuta kiki kwa kutumia umbumbumbu wa wananchi

    Siku hizi wanasiasa na chawa wa CCM wakipanda majukwaani wanatumia muda mwingi sana kumsifia Rais Samia hata kwa mambo yasiyokuwepo hadi wanatia kichefuchefu. Utasikia "Rais katoa pesa kujenga bwawa la umeme la mwalimu Nyerere, kajenga SGR na mirai mingi sana na anawalipa wafanyakazi mishahara"...
  20. Mto Songwe

    JamiiForums Tanzania Vyama aina ya CCM huwa havitoki madarakani kwa sanduku la kura

    Wengi wanaweza wasipende lakini ukweli halisia ni kuwa vyama aina ya CCM au watawala mmoja mmoja aina ya CCM huwa hawatoki madarakani kwa sanduku la kura. Hivi vyama vya namna hii vina mtindo wake wa kutolewa madarakani.
Back
Top Bottom