mangikule
JF-Expert Member
- Jun 11, 2012
- 6,054
- 5,432
Chama ambacho kimewapeleka wapiga kura wake kuzimu kwa kuwahadaa mengi ya uongo:
Chama ambacho kimeruhusu raslimali za Nchi ziuzwe na kugawiwa hovyo kwa wageni bila utaratibu na wakati mwingine utaratibu fichi wizi kabisa. Rejea
1. DP world
Kugawiwa bandari zote na kufukuza wafanyakazi kama ngedere katika shamba la mahindi ya binadamu. Hivi sasa wa kuwapa mbadala wa uongo wa kuweka kusudio la kuacha kazi ili waajiriwe na DP world. Najua wengi watameza hii ndoano na watatupwa nje ya Mfumo ajira kama makapi.
DP world mkataba uliofichwa hata kwa wabunge wetu! Maumivu kwa wananchi yanakuja hasa waarabu watakapojana bandarini na mkileta fyoko silaha zinakuja kuwanyamazisha!
2. Mbuga za wanyama
Kwa mara ya kwanza katika Historia wamasai wanalazimishwa kuacha mtindo wao wa maisha ya mbuga walikolinda ikolojia kwa karne nyingi. Waarabu wanakabidhiwa kwa lazima ili kujenga mahoteli "yanayolinda" ikolojia. Wamasai wamefanywa kama raia daraja la tatu.
Mwarabu ametumika kuwahonga nyumba ya vyumba vitatu ili waache mtindo wao wa maisha. Aliyeruhusu na kupokea hela za waarabu kuhonga wamasai huyu ni MHAINI mkubwa.
Hakuna aliyejali sheria namba 5 na 6 kuhusu ulinzi wa raslimali asilia zetu!
3. Kikokotoo(Wizi wa michango ya viinua mgongo vya wastaafu)
Wastaafu wamepangiwa wafe kabla hawajamaliza kulipwa stahili zao za mafao/viinua mgongo vyao. Baada ya kuiba michango ya wastaafu kukapangwa namna ya kuhakikisha hawapati zote! wakaja na kikokotoo. Wameshaiba kiasi kwamba hawana kiasi tena cha kuwapa wastaafu lumpsum
4. Vifurushi vipya vya Bima ya afya (Wizi wa michango ya matibabu ya waajiriwa)
Utashangaa kwanini kelele zimeibuka kati ya watoa huduma za afya na mfuko wa bima ya afya unaosimamiwa na serikali. Hawana tena kiasi kile kwa ajili ya matibabu. Imebaki kubanana na watoa huduma. Atakayeumia ni mwananchi anayehitaji huduma ya afya.
Ukweli ni huu- WIZI - CAG amegundua mabilioni yalikwapuliiwa kutoka NHIF na kuzuga kupelekwa UDOM bila utaratibu wowote WIZI.
Wafanyakazi wa NHIF nao wakaamua kukwapua Tsh 14,000,000,000 ili kwenda sawa sawa na serikali jambazi wao wakasema "wanajikopesha"
YAPO mengi sana! mengine mama wa kizimkazi ameamua kujimilikisha machimbo huko morogoro bila utaratibu.
kipo chama tawala kinasimamia huu uozo wote na kudai kinatetea wananchi.
Chama hiki kinataka kurudishwa tena madarakani katika sanduku la kura!
JE, WATASHINDA?
Chama ambacho kimeruhusu raslimali za Nchi ziuzwe na kugawiwa hovyo kwa wageni bila utaratibu na wakati mwingine utaratibu fichi wizi kabisa. Rejea
1. DP world
Kugawiwa bandari zote na kufukuza wafanyakazi kama ngedere katika shamba la mahindi ya binadamu. Hivi sasa wa kuwapa mbadala wa uongo wa kuweka kusudio la kuacha kazi ili waajiriwe na DP world. Najua wengi watameza hii ndoano na watatupwa nje ya Mfumo ajira kama makapi.
DP world mkataba uliofichwa hata kwa wabunge wetu! Maumivu kwa wananchi yanakuja hasa waarabu watakapojana bandarini na mkileta fyoko silaha zinakuja kuwanyamazisha!
2. Mbuga za wanyama
Kwa mara ya kwanza katika Historia wamasai wanalazimishwa kuacha mtindo wao wa maisha ya mbuga walikolinda ikolojia kwa karne nyingi. Waarabu wanakabidhiwa kwa lazima ili kujenga mahoteli "yanayolinda" ikolojia. Wamasai wamefanywa kama raia daraja la tatu.
Mwarabu ametumika kuwahonga nyumba ya vyumba vitatu ili waache mtindo wao wa maisha. Aliyeruhusu na kupokea hela za waarabu kuhonga wamasai huyu ni MHAINI mkubwa.
Hakuna aliyejali sheria namba 5 na 6 kuhusu ulinzi wa raslimali asilia zetu!
3. Kikokotoo(Wizi wa michango ya viinua mgongo vya wastaafu)
Wastaafu wamepangiwa wafe kabla hawajamaliza kulipwa stahili zao za mafao/viinua mgongo vyao. Baada ya kuiba michango ya wastaafu kukapangwa namna ya kuhakikisha hawapati zote! wakaja na kikokotoo. Wameshaiba kiasi kwamba hawana kiasi tena cha kuwapa wastaafu lumpsum
4. Vifurushi vipya vya Bima ya afya (Wizi wa michango ya matibabu ya waajiriwa)
Utashangaa kwanini kelele zimeibuka kati ya watoa huduma za afya na mfuko wa bima ya afya unaosimamiwa na serikali. Hawana tena kiasi kile kwa ajili ya matibabu. Imebaki kubanana na watoa huduma. Atakayeumia ni mwananchi anayehitaji huduma ya afya.
Ukweli ni huu- WIZI - CAG amegundua mabilioni yalikwapuliiwa kutoka NHIF na kuzuga kupelekwa UDOM bila utaratibu wowote WIZI.
Wafanyakazi wa NHIF nao wakaamua kukwapua Tsh 14,000,000,000 ili kwenda sawa sawa na serikali jambazi wao wakasema "wanajikopesha"
YAPO mengi sana! mengine mama wa kizimkazi ameamua kujimilikisha machimbo huko morogoro bila utaratibu.
kipo chama tawala kinasimamia huu uozo wote na kudai kinatetea wananchi.
Chama hiki kinataka kurudishwa tena madarakani katika sanduku la kura!
JE, WATASHINDA?