Uhamiaji: Dereva na V8 Iliyobeba wahamiaji Haramu 20 wa Ethiopia Isihusishwe na CCM

Inside10

JF-Expert Member
May 20, 2011
26,060
23,943
Baada ya Dereva Mtanzania Edward Erihard (31) Mkazi wa Dodoma kukamatwa akiwa amebeba Wahamiaji 20 Raia wa Ethiopia katika gari aina ya Land Cruiser V8 likiwa na bendera ya Chama cha Mapinduzi CCM katika eneo la Minjingu mkononi Manyara, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji Mkoani Manyara Philon Kyetema leo amesema gari hilo, bendera pamoja na Dereva havina uhusiano wowote na Chama cha Mapinduzi.

“Gari lilikuwa na mlingoti na baada ya kufunuliwa ikakutwa bendera inayofanana na bendera ya Chama cha Mapinduzi maana yake ni kwamba huyu bwana Edward alijiandaa kuhadaa Vyombo vya ulinzi na usalama ili visimtie nguvuni lakini tunashukuru Askari Polisi wa Minjingu waliweza kumtilia shaka na kuzuia gari na ndani kukuta Wahamiaji hao 20, kesho tutawafikisha Mahakamani”

“Naomba kufafanua kwa Watanzania ninaomba wasihusishe gari hilo na bendera inayoonekana kwenye gari hilo haina uhusiano na Chama Tawala cha CCM, hilo gari lenyewe, bendera yenyewe pamoja na Dereva hawana uhusiano na Chama cha Mapinduzi”

Source: Millard Ayo

Taarifa ya Awali: Asafirisha wahamiaji 20 kwa V8 yenye bendera ya CCM
 
Yeye ni msemaji wa chama angejikita zaidi kwenye jambo lake professionally..

Hilo la chama bashite na wenzake si wapo?
Upo sahihi labda hao jamaa ni wanachama wa hicho chama inakuaje mambo ya Chama Uhamiaji wamegeuka wasajiri wa Vyama hapo ingekua bendera ya Chama cha Upinzania angefatwa alietoa hiyo Bendera hata kama yupo Mwanza ili mradi kumchafulia tu..
 
Wale wafia DP World.

Haichomoki safari hii.

Kitaeleweka.

CCM kama vyama vingine vya Kisiasa vinatumiwa na mafisadi wanaojinasibu kuwa ni Mabilionea au Wafanyabiashara.
Haijlaishi.

Yaani mie gari langu utumie mikilomita hayo yote, gari lirudi lnanukia injera, mda gari langu halionekani, iwe ni kwa masaa au siku halafu nije kusema 'Sikujua' Muulizeni Dereva? Na ni najua watakuja watu kutetea na kusema-anayo magari mengi-shenzi taipu hata ikiwa ndio hivyo, hakuna Tajiri au mfanyabiashara, au katibu wa chama ambaye anafanya shughuli zake bila ya kuwa na Accountabilty-usipofanya hivyo hutoboi, piga ua....itoshe

Wale waliotoa ripoti ya Kuwa Tanzania kuna makundi au watu wanaohusika na biashara haramu ya watu(Human Trafficking) sasa nimeanza kuwaelewa. Ikumbukwe biashara hii huwa inakuwa na watu wa juu Serikalini na mara nyingi Uhamiaji kinara namba 1.

Huu ni Ushahidi wa ukinara huo.

"Watu wenye maamuzi" watumbuliwe?
 
Kamishina wa uhamiaji huu ni upumbavu,lini vyombo vya usalama na ulinzi nchini vitafanya kazi yake bila ya kuwaogopa hawa politicians wetu?

Zile drugs zilizokamatwa pale kilwa bandarini zimepotelea wapi?,nasoma hapa news24.com,speaker wa Bunge la SA anaweza kuwa arrested muda wowote kwa tuhuma za ubadhilifu wa fedha za umma,lini DPP utamchunguza president kikwete na speaker anna makinda?
 
Back
Top Bottom