Mbona unarudia hadithi za kale, Huyu ZITTO si ameshaelezea sababu za yeye kutofautiana na viongozi wenzie kuwa ni kukuza demokrasia ndani ya CHAMA?au DEMOKRASIA kwenye CHADEMA inamaanisha nini?
Haya maswali ya kitoto, kwani ni siri kuwa ugomvi wa hawa mafahari wawili ni kwa sababu ya ZITTO kutaka kuwa mwenyekiti?sasa akagombane na Slaa katibu mkuu wakati yeye aspiration yake kuwa mwenyekiti wa CDM?
Dr.Slaa hakuwahi kuwa na ambitions za kuwa Mwenyekiti wa CDM especially publicly.
Hakuna mtu aendaye mahakamani bila kuwa na Kinyongo, concept nzima ya mahakama ni kugawa haki, kuondoa vinyongoi kwa lugha nyengine.alichokielezea ZITTO ni kuwa ameenda UMRA ili kuondoa kinyongo cha kupelekana na jamaa zake mahakamani.
Hujui kuwa CDM walituma waraka kuonesha kuwa ZITTO anahongwa na CCM?hujui kuwa ghadhabu za kutuhumiwa ndio zilisababisha yeye kutoa tuhuma zile?mbona maswali yako mengi ni public knowledge?hayana tofauti na kuwauliza wazanzibari kwa nini wanapenda kuvaa kanzu.
Wewe umeishia darasa la ngapi?la nne?TISS wawe na Uhasimu na CDM TISS ni chama cha siasa?Umesahau Slaa alisema NUSU ya TISS wanaripoti kwake?kuna ubaya gani 10% ya TISS wakiripoti kwa ZITTO if we are to assume Katibu Mkuu wa CDM kama Taasisi?ZITTO katika capacity yake kama Naibu Katibu Mkuu anafanya kazi kwa ukaribu na Katibu Mkuu,hivyo hayo mawasiliano kwa Slaa ni shujaa, ila kwa Zitto Msaliti.
Huwezi kutunga Bank statement????????
Ndugu,hiyo mihuri ya magogoni tu inapatikana posta itakuwa Bank statement?
naona hapo kwenye red umeamua kututajia kiwango chako cha elimu sasa.
Kijana acha kuwa mshabiki, acha kushabikia watu, nyie ndio sehemu ya tatizo, tafuta itikadi unayoiamini, unayoielewa, unayoshabihiana nayo, ifuate hiyo.Kinyume na hapo utageuka bendera. Siasa sio kandanda.