Ahahaha hahaha! samahni mkuu wangu imenitoka tu silidhani..
Apology accepted wacha nikupe hesima yako kama mkongwe wa jukwaa hili unavyotakiwa kuwa addressed Mkuu Mkandara....tunaendelea.
Hapo sasa unaona ulivyojibu, kama bajeti ya serikali imetoka, inakuwaje hata baadhi wajumbe wa CCM wanaipinga? wengine wanauliza ni lini maendeleo yatafika kwao, lini barabara itajengwa yaani siku kabla ya bajeti ila mtu Kipofu hajui ule mfuko ni kama box la Chocolate. hii ina maana hata CCM wenyewe hawakuandaa bajeti yao kutokana na itikadi ama sera zao isipokuwa sera hutungwa pale pale bungeni na wao husubiri Ilani ya Mheshimiwa itawahifadhi lipi.
Hapa unachanganya CCM sera yake kuu mpaka budget iliyopita ilikuwa ni kilimo kwanza nguvu nyingi zimeelekezwa kwenye mabwana shamba, mafunzo ya kilimo bora na menginio yenye kuzalisha zaidi ili mkulima apate mavuno bora na yenye tija.
Kuna watu wanaweza kataa mafanikio yake lakini ulimwengu unatambua ni sera bora iliyotokea africa kwa muda mrefu majuzi nilikuwa nasikiliza interview ya Governor alieenguliwa wa Benki Kuu ya Nigeria
'Mallam Sanusi Lamido Sanusi' kwenye kipindi cha 'HardTalk' kitu alichokitaja kama njia kuu ya ku-propel growth in Nigeria which is inclusive alitoa mfano wa sera ya kilimo EA ambapo unajuwa mlengwa alikuwa Tanzania na kilimo kwanza, akataja changamoto ambazo jukwaa la biashara kutwa watu wanaongelea hila wavivu nao wale awapendi ku-debate wakati mwengine. Maswala yenyewe yalikuwa ni kukosekana kwa soko na changamoto zingine; akaendelea kusisitiza wamejifunza sana kwenye ubora wa sera na wao wanataka kukopy hila mambo yale yale tunayosema sisi kuhusu miundo mbinu, soko, secondary production lazima wayazingatie, truth of the matter hiyo ndio baseline policy anayopendekeza kwenye uchumi wao kwa sasa.
Sasa basi katika implemention ya kwenye hiyo sera ya kilimo katikati kuna mawakala wazushi wa mbolea, wafanyakazi wa serikari matapeli, uchakachuaji wa mbolea kila sehemu kuna matatizo yake aina maana wabunge ku-question uzembe uliotokea jimboni kwao ndio ku-fail kwa sera nzima, in short mambo kama hayo ni kwenye kila sector ya wizara ikiongozwa na ya elimu kutwa kuna utata kule.
kwa hivyo kuna tofauti kubwa sana kuhoji kama delegate kwa kile ambacho unaona wale unao wawakilisha kimewagusa directly na pale unapotoa hoja ambazo zakukosoa serikari au kuiweka accountable as in matter of ufisadi halafu kukataa group efforts hili uonekane wewe mwenyewe ndio unajua kuikosoa serikari zaidi hata kama ni mawazo yako ili kukipaisha chama chako it is commonsense wapiga kura wajue CDM inafanya kazi kwa pamoja na sio mtu mmoja.
Leo wataamini Elimu bure ni right, kesho ni privilege mara haiwezekani rais akisema inaweekana shangwe na makofi, ili mradi tu wapo wapo. Na ndio maana siku zote husubiri kumsikia mkuu wa kaya atasema nini maana wao hawana msimamo na kama ingekuwa tunarushiwa moja kwa moja kura za wabunge basi utakuta hata wale wa Upinzani wameipitisha bajeti.
Mie sikuhizi wala sijali nani kasema nini tena sasa hivi nataka kuilewa big-result now nione utekelezaji wake maana zile sera ambazo IMF/World bank wanazopewa ndio nguvu ujue zinaelekezwa zingine CCM wenyewe wala awajali nani kafisadi wapi na wala wahusika awafungwi despite PCCB, Takukuru, Mahakama and all the existing regulatory and supervisory bodies ndio maana naamini swala hili linahitaji raisi kijana.
Nakuhakikishia kwamba pale Bungeni kila mtu huenda na hoja yake kichwani, kisha yeye mwenyewe hutafuta watu kumuunga mkono, wizara na mashirika ya serikali vivyo hivyo tena hubeba na posho mkononi, huoni kama hii ni ajabu hata katika swala la kisera utafute watu wa kuuunga mkono utadhani mkutano wa saccos! Kumbe upo upande huo ndio maana basi. Kama umemchoka mtu hata akisema nini huwezi kufurahia nilidhani upo open minded kumbe tayari ulishamhukumu, Aaah basi nimekuelewa maana yanayotoka upande wa pili hunaosema kwamba Zitto hivi na vile, Slaa hivi Slaa vile, Mbowe ndiye jembe hakuna zaidi yake na sio Chadema toka nazifuatilia siasa za Bongo.
Hakuna haja ya maelezo mengi ila kumbukeni mtakuja vuna mlichopanda..
Hakuna mahala nimesema Mbowe jembe (looh salalee) lakini pia siwezi kukataa skills zake za uongozi unaweza kuona despite level yake ya elimu anaweza waweka Mbatia na Lipumba nyuma yake that tells you about his ability to command and winning people over.
Unapo ongelea maswala ya kupeleka hoja bungeni lazima ujue nani anaetoa hoja na inalenga nini, kama mmbunge anatetea maslahi ya jimboni kwakwe hiyo inakuwa inasukumwa na personal motive, kama ni swala la kukosoa sera za serikari especially kama ni mmbunge kutoka upinzani anatakiwa atoe credit za timu kuwa wao wanadhani wangefanya nini (ata kama wazo limetoka kwa mtu mmoja), vilevile kuna wabunge wanatoa hoja za kutumwa na makampuni kwa sababu hayaingii bungeni na kuna sababu nyingi za motions, lakini huwezi kuchukua credit ambazo zinastaili kuwa za timu useme ni mimi that is just selfish.