Zitto: Wapambe wametufitini na Mbowe

Zitto: Wapambe wametufitini na Mbowe

Chadema ni vigumu sana kuwaamini waislamu, waliopo watatumika kama toilet paper..akiwa bright upstairs watatafuta namna ya kummaliza ..

ACT kwenye uernyekiti mna mwamini nani? Mmemchagua kwa sababu ya dini yake?
 
Si huyu alisema Lissu ni kifaranga tu anamtafuta mama yao?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

kwahiyo wewe unataka umlinganishe zitto na lissu kwenye siasa za bongo? zitto ni level nyingine kabisa ambazo lissu hafikii
 
mara nyingi sana huwa naamini uwezo wa zitto

Yuko smart sana ila sema siasa za kibongo zinapenda malofa ndo wanaoziwezea. Ndio maana wenye akili zao huwezi kuwaona kwenye siasa.

Siasa ya tanzania ukionekana una akili sana lazima MAZWAZWA watafte namna ya kukumaliza.
 
Yuko smart sana ila sema siasa za kibongo zinapenda malofa ndo wanaoziwezea. Ndio maana wenye akili zao huwezi kuwaona kwenye siasa.

Siasa ya tanzania ukionekana una akili sana lazima MAZWAZWA watafte namna ya kukumaliza.

kumbe ndo maama maprofesa na madokta weng ccm imebidi wajitoe ufahamu na kuweka kando usomi woote ili waendane na chama kwa kufikiria kwa kutumia masa.buri!
 
Wanabodi,

Naanza kwa angalizo, hii ni thread ya news tip tuu, for your info!, sio lazima kuchangia!.

Na ikibidi kuchangia, please please please!, usitaje nina la mtu yeyote kwa sababu hata mimi muanzisha thread, sijataja nina la mtu yeyote bali nimeweka sifa tuu!.

Kama wewe uu miongoni mwa wale wajinga wajinga ambao kazi yao ni kutaja taja tuu majina ya watu!, I'm sorry hapa sii mahala pako!.

Mwanasiasa kijana, mwenye mvuto kwa vijana, na nguvu kubwa ya ushawishi, kutokana na uwezo wake wa kujenga hoja!, ambaye yuko kwenye mgogoro na chama chake, inasemekana hatimaye amekubali yaishe, ataifuta kesi aliyokifungulia chama chake, atabwaga manyanga katika chama hicho, ikiwa ni pamoja na kuusamehe ubunge wake, atafungasha kilicho chake na kujisepea zake, huku akiwaachia wenyewe chama chao, waendelee kungaika nacho!.

Japo taarifa hii niumeipata toka kwa mtu wa kuaminika, naaita tetesi hadi hapo hili litakapofanyika, kwa sababu wanasiasa sio watu wa kuwaaminia sana!, leo anaweza kusema hivi na kesho kuamua kingine, au leo anaweza kuahidi hili na kesho akabadili mawazo!.

Le bila hata kuithibitisha, ni kukupa wewe mwana jf, ile advantage ya "be the first to know!".

Kufuatia ethics za journalism, silitaji kwanza jina, mpaka hili tukio litakapotokea, na pia naomba nisiitaje source yangu, kwa kutumia kipengele kiitwacho "the confidentiality of the source!".

Information is power, be informed kwa jambo hili kubwa kabisa kuwahi kutokea kwenye siasa za upinzani!.

My Take!.

Kama tetesi hizi ni kweli, then hii itakuwa ni one of the best moves mwanasiasa huyo ameweza kuifanya!.

Wengi wa wanasiasa wetu, ni wanasiasa njaa!, siasa kwao ni ajira!, wanautafuta ubunge sio kwa lengo la kutumikia watu bali kutafutia ulaji!, hivyo kwa wanasiasa wengi njaa njaa, ubunge ndio ajira yao, wakiukosa ubunge, wataishia kujifia njaa!. Kitendo cha mwanasiasa huyu, kukubali kuachia ubunge, ni uthibitisho, ubunge kwake sio ajira bali ni utumishi wa watu!, kama hapo ulipo, umefungwa mdomo, mikono na miguu kushindwa kuwatumikia watu, then, unajifungashia virago vyako na kujiondokea kwa amani, kwenda kuwatumikia watu mahali pengine!.

Move hii pia itakisaidia sana chama chake, kitendo cha kukubali yaishe kwa ridhaa yako mwenyewe na kuifuta kesi, ni uthibitisho wa good faith, ikitokea 2015, chama chake kikashindwa kufikia malengo ya kutinga Ikulu, wasndishwe kwa mengine, wasije kumletea, kisingizio, cha kesi!.

Na mwisho, kama ni kweli mwanasaiasa huyu ni msaliti kama alivyoelezwa kwenye chama chake, then, "karma" itamchapa bakora vilivyo!, lakini kama amesingiziwa, na kuhukumiwa kwa maonevyo, hivyo hiyo "karma" ita mu elevate to an imaginable height huko aendako, at the same time, kitakula bakora za "karma" kwa maovu waliomtendea!.

Kama una nyota, una nyota tuu, kama uling'ara, maisha ni popote na utang'ara tuu!, kama huta nyota, bali uling'arishwa, basi ukitoka ni lazima utafifia!. Hata maisha ya kisiasa pia ni maisha popote!.

NB. Baadhi ya thread nyingine zinaita "info pack" kwa ajili ya kutoa tuu information, na sio kujibishana na watu au kuchangia!. Unaweza kusoma tuu na sio lazima kuchangia!, na kuyasubiria haya yaliyozungumzwa humu yameterialize!.

Natanguliza shukrani kwa kunielewa.

Asante.

Pasco
 
Mkuu amesha andaliwa makao kule ACT muda umefika wa kwenda kukalia kiti chake rasmi ili tujue rangi yake halisi
 
All in all,kwa ajili ya manufaa ya watanzania wote,nchi yetu inahitaji upinzani imara kwa ajili ya kuifanya serikali iliyopo madarakani kutimiza majukumu yake ipasavyo. Kama uamuzi wake huo utasaidia kuimarisha upinzani,that is well and good for the benefit of our country,
 
Basi Heri tu kama kweli ni hivyo! ila nimependa sana alivoamua kujikausha kipindi hiki..tuliiii!
 
Difficult to give up kirahisi hivo mpaka kupoteza ubunge wake otherwise labda nia yake akibwaga mayanga aje kusimama mwakani kwa either ubunge au mgombea urais kwa chama lingine,alianzisha kesi ya nini kama rahisi kihivo au ashaona dalili kupoteza.
BTW atakuwa kawapiga mpunga mkubwa wale wa upande wa pili
 
Pasco,kiuandishi hapo umeshamtaja. Afadhali aende zake.Wenzake hawamtaki na yeye anang'ang'ania tu akipoteza muda wake
 
Last edited by a moderator:
Kama ni kweli nimpongeze kwa uamuzi huu atakaoenda kuufanya, hii itamsaidia sana kujirudisha kwenye siasa za tz..

Ameona hatari ambayo iko mbele yake, kwani kesi aliyoifungulia chama chake alikuwa anaenda kushindwa kitu ambacho kingemletea taswira mbaya na kumuondoa kabisa kwenye ulingo wa siasa.

Na endapo angeshinda kesi yake bado asingekuwa na nguvu kama hii atakayo ipata kwa kufuta kesi na kujiondoa mwenyewe,kitu ambacho kitamfanya aonekane mwanasiasa mkomavu kwa wale wajinga wajinga wasiasa za majitaka..
 
Kwa sasa yupo busy na kutunga nyimbo za bongo flava kwenye kundi lao la wapagazi walizamia Dar kutafuta maisha.
 
Back
Top Bottom