Zitto: Wapambe wametufitini na Mbowe

Zitto: Wapambe wametufitini na Mbowe

Endelea kuota ndoto za mchana,kama kusoma hujui ina maana hata picha zimekushinda? Hivi huzioni hizi movement za masalia au wafuasi wa zitto dhidi ya cdm? Ni lini kajitokeza hadharani kuwakana hawa mchange,nyakarungu and co'z? Pole sana kwa kukubali kuwa msukule wa zzk!
Wala hujakosea mimi msukule wa ZZK haswaaa isipokuwa wewe? Kama mimi wa ZZK wewe wa nani? maana msukule atamjua mwenzake kwani wote hawana kauli. Kifupi haya ni maoni yangu huna sababu ya kutoka povu, unaweza yasikiliza ama kuyapuuza, chaguo ni lako.
 
Dear Zitto,

My brother and my Friend. It is time to do what your heart tells you to do. Do not follow the popular push from the mob. Seeking reconciliation is much better than waging wars. This is time to reflect and come to terms with the reality and the reality is Tanzania needs you to continue with the fight, the fight within the confines of Chadema. Tanzania needs quick change and it has to happen within 5 years. Strategically starting a new party wouldn't move our dreams of change to reality it will push them further a distance more. There is no harm to sit down with Mr. Mbowe and the rest of the key leaders of chadema and reconcile and move back to the agenda of redeeming our country.

Dear Mr. Mbowe,
In politics there is no permanent enemy, we have permanent goals. As long as the goals are aligned we have to move together. I entreat you to meet with the young man and try to resolve the challenges between him and the party. Tanzanians would still want to see the energy combined to topple the corrupt party CCM. We are not interested in the arduous and long court process. It won't solve the problem, it might even prolong it. You guys can forgive each other and move on. We need Chadema as a formidable force to get our hopes back.

It is upon you guys to move above your egos and truly make decisions for the good of this country.

Unfortunately these will just be wishes, reality on the ground is CDM decided to become a popular party and not a proper party. They personally part ways with my support when they decided to go head on in a self destructive campaign that surely served NO ONE. Leo hii wamebaki kulaumiana kuchwa kucha. Na hawa Kina mbowe wanaona hii ni sahihi.
 
Mh ZITTO. unakumbuka mwaka 2009 kama sikosei ulikorofishana na CHADEMA wenzio ikapelekea hadi kina Kafilila na wenzie wakahamia NCCR? Unakimbuk iliundwa kamti kukusuruhisha akiwemo marehemu mpendwa wetu mama yako? Unkumbuka ulisema unatembea na barua mfukoni ya kujiuzuru wakati wowote? Unakumbuka ulipokua umelazwa hosp nchini INDIA ulituhumiwa kutaka kumpindua Mwenyekiti wa NCCR ndg Mbatia kwa kumtumia Kafulila mkajaribu kumshawishi Moses Machali lakini alikataa na Machali alikukemea sana wewe kupitia kipindi cha tuongee asubuhi? Unakumbuka hali hiyo ilipelekea Kafulila kufukuzwa NCCR hadi akalia na baadae kusamehewa? Mh kwa nini wenzio wakipanga kutoka bungeni wakati KIKWETE alipozindua bunge wewe uligoma kuungana nao na kubaki chumbani? Unakubaliana na mimi kuwa wakati huo wabunge wote wa Chadema walikua wegeni bungeni isipokua wabunge wote wa 2005 kasoro DK Slaa tu? sasa ni wageni gani au wapambe gani waliokukuta CHADEMA waliokugombanisha na Mbowe 2010 ambao pia walikugombanisha nae 2009 kabla ya uchaguzi mkuu ikapelekea wewe kutembea na barua na akina KAFULILA kuhamia NCCR? WHY ONLY YOU? Mkuu kwa nini ugombanishwe wewe tu na Mbowe na sio Slaa na Mbowe.Mkuu kama umesema huna kinyongo umeanza lini kutokuwa na kinyongo? Mkuu kwa nini ulisema Mbowe alihongwa na Nimrod Mkono na Mkono akakanusha?. Mkuu uko tayari CHADEMA iendelee bila wewe kuwepo? na uko tayari CCM ing'olewe uchaguzi ujao? Mahusiano na mawasiliano yako na Jack Zoka na Rostam unafikiri yaliwafurahisha viongozi wenzio wa CHADEMA? na unafikiri yalikua yana manufaa kwa chama cha CHADEMA? JE? huoni kuwa mawasiliano hayo ndio yamekuchonganisha na wenzio? Unafikiri wenzio watakuamini kweli kwa mawasiliano ja mahasimu wao.Unajua kuwa mtu hawezi kutunga bank statement au kumbukumbu za mawasiliano ya simu za CELLPHONE? Kwa hayo machache yote umechonganishwa n wapambe? mimi ni mmoja wa watu niliokua mshabiki wako mkubwa na hadi leo.
 
I saw this coming... two years ago. Nilitumia nguvu na juhudi nyingi sana kumshauri Zitto, kwani nilishaona kinachoelekea kutokea. Nilitukanwa na kuitwa msaliti humu lakini niliamini, na bado naamini kuna watu "wame - take advantage" ya udhaifu wa Zitto kummaliza na kuidhoofisha CHADEMA...
Kwa bahati mbaya Zitto hakunisikiliza! Najua mimi sio yeyote katika siasa, lakini kutokana na kufuatilia mambo machache kwenye hiyo siasa, basi yale machache ninayoyafuatilia nakuwa makini nayo...

Tatizo moja la Zitto ni kutokujua "weaknesses" zake... Kwani angeziua, bila shaka angezifanyia kazi, na isingekuwa rahisi kuchezewa kiasi hiki...

- Zitto wewe ni kiongozi mzuri sana lakini una ubinafsi kwenye suala la madaraka na umaarufu wa ksisiasa. Najua utakataa sana, but ukweli ni huo... Ulitakiwa tu ujue CHADEMA ni chama kimoja, na hakiwezi kuongozwa na watu wawili... baas. Then ujue kuna siku Mbowe angeachia madaraka, na wewe ungeongoza CHADEMA... baaas

Ushauri tena kwa sasa
Watu ulio nao ACT sio watu wa hadhi yako, wala sio watu wanaokutakia mazuri. Ndio wametumiaka kukudondosha CHADEMA, na wataendelea kutumika kukumaliza kisiasa... Huwezi kuwa na watu kama kina Mchange, eti useme ni watu makini! Are you kidding?

Ndugu hujawahi kukutana na watu wenye Msimamo.Ulitaka Zitto aende kinyume na Msimamo wake kwasababu ya kupewa amnesty na Mbowe?

Historia huhukumu watu baada ya miaka mingi sana, binafsi nitamhukumu Zito kwa kusimamia alichokiamini, kama bado anakiamini, nacho ni Demokrasia ya wazi na ya kweli ambayo CDM wanaipigania.

Sitampa KURA Milele mwanasiasa asiye na AMBITION, Hafai kuwa KIONGOZI, Kiongozi ni mtu anayefikiria kufanya maamuzi na sio kusubiri aamuliwe, au kufuata mkumbo.

Nadhan ndugu Tuko umesahau kuwa career ya zitto ni SIASA, na Mwanasiasa bila Madaraka wala UMAARUFU huitwa, kada wa chama, aka Mshabiki, ZITTO is Many things but Sio MSHABIKI.
 
" Lakini nasononeshwa zaidi na kitu kinachoendelea ndani ya Chadema.

“Nini kimetokea Chadema? Kwa nini tumejikuta tumeondoka katika mstari? Tupo wabunge 48 bungeni sasa, lakini hatusogezi mbele nchi, tumerudi nyuma wakati huo tulikuwa watano lakini tulikuwa tunaenda vizuri sana."

Hapo ndipo watu wengi humu ndani hawajawahi kukaa na kupatafakari kwa kina.

Wale wabunge wa cdm wanaojifanya ni mabingwa wa kumdhalilisha zito wote wameshindwa kufanya hiyo kazi hapo juu, mwenzao aliweza na ndio maana wao wakapata nafasi ya kuwepo bungeni Sasa hivi.

Leo wanajifanya wao ni cdm zaidi kuliko zito. Ifike mahala tukubali, mchango wa zito kwa cdm ni mkubwa sana na haupimiki kirahisi kama watu wengi humu ndani wanavyodhani.

Mlio wengi humu ndani mnaopiga kelele pia mmejaa cdm mainly kwa kazi kubwa aliyofanya zito. Lakini cha ajabu, na tena kwa umbumbu mkubwa kabisa mmeungana na hao wabunge waliongia bungeni kwa juhudi za mwenzao kumdhalilisha.

Kweli binadamu hawana shukrani.

Ndio maana washahili wakasema "tenda wema nenda zako usingoje shukrani".

Mkuu..ukifuatilia sana humu hakuna anaesema ZITTO hakuna kitu cha maana amefanya CDM labda mtu huyo km anatumia kiungo kingine kufikiri badala ya Ubongo...nandio maana cc wengine tunaitamani cku ZITO atakayo maliza matatizo.na viongoz wake kwa Lengo lakupeleka mbele jahazi la cdm....Binafsi nitackitika akienda ACT kule ataumia sana kwasababu kujenga chama sikitu chepesi amepitia humo kwenye op.sangara anajua....plz ZITO kuomba Radhi ni jambo dogo sn cc tunaopenda mageuzi ya ukweli...bado tunauthamini na kuuhitaji Mchango wako ndani ya cdm
 
Wala hujakosea mimi msukule wa ZZK haswaaa isipokuwa wewe? Kama mimi wa ZZK wewe wa nani? maana msukule atamjua mwenzake kwani wote hawana kauli. Kifupi haya ni maoni yangu huna sababu ya kutoka povu, unaweza yasikiliza ama kuyapuuza, chaguo ni lako.

Safi sana mkandara. Kuna watu humu ndani wanajiona wao ndio Pekee Wenye kufahamu ukweli na Wenye haki ya kutoa mawazo yao. Wenzao wakitoa ni wendawazimu na hawajui knachoendelea na wala hawaitakii mema cdm.

Kwamba mawazo yako lazima yafanne na ya kwao tu Ili uweze kuwa sahihi.

Ndio maana kwa hoja hizi za kizembe Huwa naishia kuwa msomaji.
 
Mh ZITTO. unakumbuka mwaka 2009 kama sikosei ulikorofishana na CHADEMA wenzio ikapelekea hadi kina Kafilila na wenzie wakahamia NCCR? Unakimbuk iliundwa kamti kukusuruhisha akiwemo marehemu mpendwa wetu mama yako? Unkumbuka ulisema unatembea na barua mfukoni ya kujiuzuru wakati wowote? Unakumbuka ulipokua umelazwa hosp nchini INDIA ulituhumiwa kutaka kumpindua Mwenyekiti wa NCCR ndg Mbatia kwa kumtumia Kafulila mkajaribu kumshawishi Moses Machali lakini alikataa na Machali alikukemea sana wewe kupitia kipindi cha tuongee asubuhi? Unakumbuka hali hiyo ilipelekea Kafulila kufukuzwa NCCR hadi akalia na baadae kusamehewa? Mh kwa nini wenzio wakipanga kutoka bungeni wakati KIKWETE alipozindua bunge wewe uligoma kuungana nao na kubaki chumbani? Unakubaliana na mimi kuwa wakati huo wabunge wote wa Chadema walikua wegeni bungeni isipokua wabunge wote wa 2005 kasoro DK Slaa tu? sasa ni wageni gani au wapambe gani waliokukuta CHADEMA waliokugombanisha na Mbowe 2010 ambao pia walikugombanisha nae 2009 kabla ya uchaguzi mkuu ikapelekea wewe kutembea na barua na akina KAFULILA kuhamia NCCR? WHY ONLY YOU? Mkuu kwa nini ugombanishwe wewe tu na Mbowe na sio Slaa na Mbowe.Mkuu kama umesema huna kinyongo umeanza lini kutokuwa na kinyongo? Mkuu kwa nini ulisema Mbowe alihongwa na Nimrod Mkono na Mkono akakanusha?. Mkuu uko tayari CHADEMA iendelee bila wewe kuwepo? na uko tayari CCM ing'olewe uchaguzi ujao? Mahusiano na mawasiliano yako na Jack Zoka na Rostam unafikiri yaliwafurahisha viongozi wenzio wa CHADEMA? na unafikiri yalikua yana manufaa kwa chama cha CHADEMA? JE? huoni kuwa mawasiliano hayo ndio yamekuchonganisha na wenzio? Unafikiri wenzio watakuamini kweli kwa mawasiliano ja mahasimu wao.Unajua kuwa mtu hawezi kutunga bank statement au kumbukumbu za mawasiliano ya simu za CELLPHONE? Kwa hayo machache yote umechonganishwa n wapambe? mimi ni mmoja wa watu niliokua mshabiki wako mkubwa na hadi leo.

Ngumu kumesaaa rafikii
 
Mkuu..ukifuatilia sana humu hakuna anaesema ZITTO hakuna kitu cha maana amefanya CDM labda mtu huyo km anatumia kiungo kingine kufikiri badala ya Ubongo...nandio maana cc wengine tunaitamani cku ZITO atakayo maliza matatizo.na viongoz wake kwa Lengo lakupeleka mbele jahazi la cdm....Binafsi nitackitika akienda ACT kule ataumia sana kwasababu kujenga chama sikitu chepesi amepitia humo kwenye op.sangara anajua....plz ZITO kuomba Radhi ni jambo dogo sn cc tunaopenda mageuzi ya ukweli...bado tunauthamini na kuuhitaji Mchango wako ndani ya cdm

Kula tano fasta
 
Utofauti wa Rika? Ideology? methodology and Approach? Mbona imetokea kwingine mfano wa ODM na wamesolve tofauti? Tena Saga la ODM lilikuwa baya zaidi kuliko la saga la CHADEMA, kwanini Saga CHADEMA haiwezi kuwa solved?
 

Attachments

  • Ababu Vs. Odinga.jpg
    Ababu Vs. Odinga.jpg
    8.5 KB · Views: 102
  • Zitto Vs. Mbowe.jpg
    Zitto Vs. Mbowe.jpg
    8.8 KB · Views: 94
Ndugu hujawahi kukutana na watu wenye Msimamo.Ulitaka Zitto aende kinyume na Msimamo wake kwasababu ya kupewa amnesty na Mbowe?

Historia huhukumu watu baada ya miaka mingi sana, binafsi nitamhukumu Zito kwa kusimamia alichokiamini, kama bado anakiamini, nacho ni Demokrasia ya wazi na ya kweli ambayo CDM wanaipigania.

Sitampa KURA Milele mwanasiasa asiye na AMBITION, Hafai kuwa KIONGOZI, Kiongozi ni mtu anayefikiria kufanya maamuzi na sio kusubiri aamuliwe, au kufuata mkumbo.

Nadhan ndugu Tuko umesahau kuwa career ya zitto ni SIASA, na Mwanasiasa bila Madaraka wala UMAARUFU huitwa, kada wa chama, aka Mshabiki, ZITTO is Many things but Sio MSHABIKI.

Then it's ok, akatafute madaraka act....ambako mwigamba naye anayataka....ameanzisha chama na kukieneza tanzania wakati anaendelea kuvaa koti la cdm akiwa act kwa support ya magamba.
 
Then it's ok, akatafute madaraka act....ambako mwigamba naye anayataka....ameanzisha chama na kukieneza tanzania wakati anaendelea kuvaa koti la cdm akiwa act kwa support ya magamba.

I think huu uamuzi ni wa ZITTO mwenyewe, wwaliobaki ni washabiki tu , hawawezi kuchukua uamuzi kwa niaba yake.Wanachoweza kufanya ni kumchochea, atakaloamua mwenyewe atajua mwenyewe na mungu wake.

Wanachokifanya ACT ndiocho walichokifanya CDM 2005-2010, Historia inaonesha walikusanya able and non able. Ndio maana ukifungua thread inayohusu CDM leo hii hapa JF nusu ni matusi.

CDM Kumejaa takataka,wanayaziba hata yale mazuri waliyoyafanya. ACT haiwezi Kuhukumiwa mapema hivi, kwani 2005 CUF ndio ilikuwa chama KIKUU cha UPINZANI, nao wangeweza kuidismiss CDM kama tawi la CCM,lakini leo hii kiko wapi? Ngangari imebaki zenji tu.

Siasa za TZ inabidi ufyatuke kidogo, ndio maana straight people kama kina ZITTO wanaonekana kama wehu, halafu wale mazumbukuku kama kina LEMA ndio wanaonekana MAKAMANDA. Kazi ipo
 
Kisiasa Zitto ana uwezo uliopishana kidogo sana na Mnyika ila Mnyika atafanikiwa kisiasa kuliko Zitto kwasababu ni Mvumilivu na ana subira,Msishangae mbeleni akawa Mwenyekiti wa Chadema hata Mgombea Urais kabla ya Zitto japo Zitto kamtangulia na ndoto hizo,Tatizo la Zitto ni dogo tu kiburi,pupa na uroho wa madaraka.Huenda hata sio msaliti wa chama ila the way anavyolazimisha ndoto zake watu wanamtafsiri tofauti kwa kuona sio kawaida huenda kuna nguvu nyuma yake,na mi naendelea kusema kwenda ACT kajimaliza ni vyema akaangalia alipojikwaa akarudi nyuma akashirikiana na wenzake wamsaidie atimize ndoto zake na ajifunze kwa mdogo wake Mnyika anavyokithamini chama chake na alivyo na nidhamu kwa Viongozi wake na anavyoshirikiana nao,kujifunza kwa mdogo sio kosa ila kwa kiburi cha Zitto anaweza kuona anadhalilishwa na hapo ndipo anapokosea.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Katika ya mwanadamu ushindi mkubwa sana ambao mwanadamu anaweza kujivunia na ambo ni very expensive ni kusamehe bila masharti. Hapa na maanisha kwamba si Zito si Chadema wote wanapaswa kusamehe bila masharti. Wakifanya hivyo wataeshimika na chama kitakuwa imara sana. Lakini kama kila upande ukawa too proud basi mwishoe ni majuto tu. Chama kimsamehe Zito na Zito pia awasamehe wote bila lakini lakini. Kama tunahitaji ukombozi tunahitaji kuvumiliana na kusaidiana pale mmoja anatereza.
 
arola.Umejuaje kama Zitto alikua anaungwa mkono ma wajumbe wengi wa Baraza Kuu? umejuaje hata kama alikua ana makosa baraza kuu lingemuunga mkono?Je? huoni kama alikua hana imani na kamati kuu lakini ana imani na Baraza kuu basi kulikua kuna upangwaji wa matokeo ambao Zitto aliufanya kwa baraza kuu? yaani alikua amekwisha lihonga baraza kuu. Je? Kwa sisi tunaoona Zitto ameonewa au anaogopwa na Mbowe kwamba amefukuzwa ili mbowe apumue, je? Waraka wa Mwgamba na Kitila ni halali? je? kufukuzwa kwa mwigamba na Kitila ni halali au si halali? je kwa nini na wao hatuwatetei? Ni Mbowe ndio alimtafuta Zitto akiwa chuoni hii ni kwa mujibu wa Mbowe mwenyewe. Je? ni kwa nini wagombane wakati Mbowe ni mwenyekiti na Zitto alikua naibu katibu mkuu.Je unafikiri ni kwa sababu Zitto alitaka kugombea uenyekiti tuu au kuna la ziada?.Swala la urais sidhani kama Zitto ana haja nalo kwa sababu katiba ya taifa haimpi ruhusa sababu ya umri.Unafiki kama zitto angekua ana subira nani ndani ya CHADEMA angemzuia kuwa mwenyekiti huko mbeleni kwani Dk Slaa na Mbowe sidhani kama wangeendelea kwa zaidi ya miaka 15.Kikwete angekua hana subira leo hii asingekua rais,kwani aliutaka urais pamoja na Mkapa lakini ilibidi asubiri miaka 10 ndio akaupata urais na wakati Kikwete anaanza harakati hizo alikua ana umri mkubwa kuliko umri aliokua nao Zitto wakati anutaka umwenyekiti wa Chadema. Naamini Zitto angetulia hakuna kazi nyingine ambayo ingemfaa hapa Tanzania ambayo angeweza kupewa na ingemfaa zaidi ya U Rais. Zitto asingekua na mpinzani huko mbeleni.
 
Mh ZITTO. unakumbuka mwaka 2009 kama sikosei ulikorofishana na CHADEMA wenzio ikapelekea hadi kina Kafilila na wenzie wakahamia NCCR? Unakimbuk iliundwa kamti kukusuruhisha akiwemo marehemu mpendwa wetu mama yako? Unkumbuka ulisema unatembea na barua mfukoni ya kujiuzuru wakati wowote? Unakumbuka ulipokua umelazwa hosp nchini INDIA ulituhumiwa kutaka kumpindua Mwenyekiti wa NCCR ndg Mbatia kwa kumtumia Kafulila mkajaribu kumshawishi Moses Machali lakini alikataa na Machali alikukemea sana wewe kupitia kipindi cha tuongee asubuhi? Unakumbuka hali hiyo ilipelekea Kafulila kufukuzwa NCCR hadi akalia na baadae kusamehewa? Mh kwa nini wenzio wakipanga kutoka bungeni wakati KIKWETE alipozindua bunge wewe uligoma kuungana nao na kubaki chumbani?

Mbona unarudia hadithi za kale, Huyu ZITTO si ameshaelezea sababu za yeye kutofautiana na viongozi wenzie kuwa ni kukuza demokrasia ndani ya CHAMA?au DEMOKRASIA kwenye CHADEMA inamaanisha nini?


Unakubaliana na mimi kuwa wakati huo wabunge wote wa Chadema walikua wegeni bungeni isipokua wabunge wote wa 2005 kasoro DK Slaa tu? sasa ni wageni gani au wapambe gani waliokukuta CHADEMA waliokugombanisha na Mbowe 2010 ambao pia walikugombanisha nae 2009 kabla ya uchaguzi mkuu ikapelekea wewe kutembea na barua na akina KAFULILA kuhamia NCCR? WHY ONLY YOU? Mkuu kwa nini ugombanishwe wewe tu na Mbowe na sio Slaa na Mbowe.
Haya maswali ya kitoto, kwani ni siri kuwa ugomvi wa hawa mafahari wawili ni kwa sababu ya ZITTO kutaka kuwa mwenyekiti?sasa akagombane na Slaa katibu mkuu wakati yeye aspiration yake kuwa mwenyekiti wa CDM?
Dr.Slaa hakuwahi kuwa na ambitions za kuwa Mwenyekiti wa CDM especially publicly.

Mkuu kama umesema huna kinyongo umeanza lini kutokuwa na kinyongo?
Hakuna mtu aendaye mahakamani bila kuwa na Kinyongo, concept nzima ya mahakama ni kugawa haki, kuondoa vinyongoi kwa lugha nyengine.alichokielezea ZITTO ni kuwa ameenda UMRA ili kuondoa kinyongo cha kupelekana na jamaa zake mahakamani.

Mkuu kwa nini ulisema Mbowe alihongwa na Nimrod Mkono na Mkono akakanusha?. Mkuu uko tayari CHADEMA iendelee bila wewe kuwepo?
Hujui kuwa CDM walituma waraka kuonesha kuwa ZITTO anahongwa na CCM?hujui kuwa ghadhabu za kutuhumiwa ndio zilisababisha yeye kutoa tuhuma zile?mbona maswali yako mengi ni public knowledge?hayana tofauti na kuwauliza wazanzibari kwa nini wanapenda kuvaa kanzu.

na uko tayari CCM ing'olewe uchaguzi ujao? Mahusiano na mawasiliano yako na Jack Zoka na Rostam unafikiri yaliwafurahisha viongozi wenzio wa CHADEMA?na unafikiri yalikua yana manufaa kwa chama cha CHADEMA? JE? huoni kuwa mawasiliano hayo ndio yamekuchonganisha na wenzio? Unafikiri wenzio watakuamini kweli kwa mawasiliano ja mahasimu wao.
Wewe umeishia darasa la ngapi?la nne?TISS wawe na Uhasimu na CDM TISS ni chama cha siasa?Umesahau Slaa alisema NUSU ya TISS wanaripoti kwake?kuna ubaya gani 10% ya TISS wakiripoti kwa ZITTO if we are to assume Katibu Mkuu wa CDM kama Taasisi?ZITTO katika capacity yake kama Naibu Katibu Mkuu anafanya kazi kwa ukaribu na Katibu Mkuu,hivyo hayo mawasiliano kwa Slaa ni shujaa, ila kwa Zitto Msaliti.

Unajua kuwa mtu hawezi kutunga bank statement au kumbukumbu za mawasiliano ya simu za CELLPHONE? Kwa hayo machache yote umechonganishwa n wapambe? mimi ni mmoja wa watu niliokua mshabiki wako mkubwa na hadi leo.

Huwezi kutunga Bank statement????????
Ndugu,hiyo mihuri ya magogoni tu inapatikana posta itakuwa Bank statement?

naona hapo kwenye red umeamua kututajia kiwango chako cha elimu sasa.

Kijana acha kuwa mshabiki, acha kushabikia watu, nyie ndio sehemu ya tatizo, tafuta itikadi unayoiamini, unayoielewa, unayoshabihiana nayo, ifuate hiyo.Kinyume na hapo utageuka bendera. Siasa sio kandanda.
 
Nakubaliana na uloyasema isipokuwa pengine nimeanza vibaya ktk maelezo yangu.
nachosema mimi ni kwamba Zitto hakuwa Tatizo bali CCM walielewa kwamba ndoto ya Zitto ni kuwa rais baadaye na Mbowe vile vile wakijua kwamba Mbowe hawezi kuachia ambiton hiyo kirahisi. Hivyo wakaona kati yao the weakest link ni Zitto. Kama wangejua Dr.Slaa ndiye angegombea urais 2010, nakuhakikishia usingeyasikia ya Zitto na Mbowe bali Mbowe na Dr.Slaa.

Ni sawa na Chadema leo wanavyoyazungumza ya CCM kuhusu kugombea Urais na kama CCM watayachukulia personal basi hawatafika popote kwa sababu kila anayesemwa hafai ndani ya CCM ni weakest link haina maana kwamba hafai. Tunamsema Membe, Makamba na wengine wengi ambao tunajua nia zao ili kuwatia jamba moto CCM. Na hakika Makamba na hoja yake ya Ujana ilikuwa silaha ya watu kutumia ili kuivuruga tu CCM na sii kwamba Makamba hafai, ama Lowassa ndiye kweli anafaa kuwa rais wa Tanzania kutokana na mapenzi ya wana Chadema isipokuwa kisiasa yeye ndiye weakest link kwa mtazamo wa Chadema ili kuzua chokochoko ndani ya chama. Na CCM walifikia kugombana lakini kwa sababu ya busara na hekima za wazee wa chama hicho na kwamba Chadema haikuwa na vibaraka ndani ya CCM, waliweza kuyamaliza.
Ndivyo navyoliona swala la Mbowe na Zitto.

we naye sasa huyo msaliti angegombeaje Urais,wakati hata sasa miaka 40 hana
 
Back
Top Bottom