Nimeshindwa kuelewa inakuwaje baadhi ya watu wanashindwa kusoma makala na kisha ndiyo wachangie?Inakuwaje waje wengine waibuke na kutaka au kuonyesha dalili za kuzima mjadala kwa visingizio kibao kuhusu chaguzi ndogo zinazoendelea? binafsi mimi nina-discourage majungu na fitina katika kipindi hiki cha chaguzi ndogo ila nashindwa kuelewa tumefikiaje hatua ya kumzuia mtu asiweke sawa upotoshaji uliofanywa na mtu kwenye makala.
Kama Zitto angekaa kimya na mjadala ukaendelea kwa jinsi ambavyo watu walikuwa wameanza kuupotosha kwa vyovyote vile ungekuwa na madhara.Watu wangesubiri hadi tarehe 2 Aprili huku wengine wakiendelea kuamini ndivyo sivyo.je ndiyo tulikuwa tunataka iwe hivyo?kwa maslahi ya nani?Halafu sijui tunapata wapi moral authority ya kuchagulia watu kitu cha kusema?Wengine wamedhani linalojadiliwa ni umri tu wa Urais,makala iliyoandikwa iko wazi.
Kuna Mwingine ameibuka na kuanza kushambulia kuhusu siasa za Alliance.Mwingine alitunga jina "BENZITTO" alliance kwa sababu anazozijua yeye mwenyewe.Labda pengine kwa kuonyesha msimamo wangu,kama Zitto atagombea nafasi hiyo ndani ya chama na chama kikamteu kwa kuzingatia muafaka ndani ya chama NITAMUUNGA MKONO.Hata makala hii NIMEIUNGA MKONO.Tatizo tumezoea kuwa na wanasiasa wanafiki na wanaofanya hila kwenye siasa.sijui ni nani alisema kuweka msiamo wako wazi ili watu wakujue na wakupime bila kuathiri utangamano ndani ya chama ni tatizo?
Nina uhakika makala hii iliyoandikwa na Zitto,kwenye jina lake angekuwa ameandikwa mwingine mjadala ungekuwa tofauti.pia niweke wazi sina Alliance yoyote ndani ya chama,na hata hivyo ninashangaa sana watu wanaoharamisha siasa za Alliance.Tangu lini siasa za Alliance zikawa haramu?Nilishawahi kusema tena,siasa za alliance haziepukiki.
Hata chama changu kilifanya alliance na NCCR-Mageuzi mwaka 1995.Mwaka 2000 Chadema hakikusimamisha mgombea urais kwa kuwa kilifanya alliance na CUF na mwaka 2005 chama kilisimamisha mgombea urais halikadhalika mwaka 2010.Kama kijana ninayeelewa vyema nadharia za siasa na kwa vitendo napata shida kuona baadhi ya watu wenye akili timamu wanataka kuharamisha siasa za Alliance.
Kenya mwaka 2002,siasa za Alliance ndizo zilizoiondoa brutal party (KANU) madarakani. Raila Amolo Odinga alimuunga mkono Mwai Emilio Kibaki wa chama cha DP.Pale Uhuru Park Raila alimu-endorse Kibaki kwa kusimamia "Kibaki Tosha".Muungano wa NAARC ulifanikiwa kukipoteza chama tawala cha KANU katika ramani ya siasa za Kenya.
Uchaguzi wa juzi hapo Congo DRC,Mgombea wa Upinzani nusura amuangushe the Incumbent Joseph Kabila baada ya kufanya alliance na wagombea wengine.Tshisekedi aliiungwa mkono hadi naJean pierre Bemba akiwa The Hague
Tusiharamishe vitu bila kufuat principle za siasa kwa kusukumwa na utashi binafsi na matamanio ya upotoshaji tu.Sasa wanaosema kuhusu kuunga mkono hoja ya kutanua wigo wa ugombea urais,wanaopinga hawaji na logic yoyote kisiasa,kisheria wala kiuchumi.Mwandishi na mwanafalsafa Nguli Jenerali Ulimwengu aliandika kuhusu hili kwenye makala yake nadhani ni the East African Standard wiki 2 zilizopita.Nilifurahi jinsi alivyojadili hili ndani ya mantiki na kujenga hoja nzito ya kiunafalsafa.Hakuna mtu aliyemuhusisha na alliance,pia mwandishi mahiri na msomi aliyebobea Comrade Ayoub Rioba ameandika makala kuhusu hili na akaitendea haki taaluma yake na kufafanua kwa weledi kuhusu hili jambo.Hakuna aliyemuhusisha na Alliance.Ninachoona hapa ni hofu zaidi kuliko logic.
Jamii forums(Where we dare to talk openly) ni jukwaa la hoja ndani ya mantiki na inajulikana hivyo.Pia,tusikubali kuyumbishwa na upotoshaji wa watu wachache kwa maslahi yao tu.
Vijana msikubali/tusikubali kutumika kama daraja kwa baadhi ya wanasiasa.kuna baadhi ya wanasiasa wana-take advantage ya matatizo ya vijana hasa ajira n.k. mmewasikia CCM wakigombea hoja ya ukosefu wa ajira upande mmoja ukitoa takwimu na upande mwingine ukitoa tuhuma.Aliyeituhumu serikali alikuwa waziri mkuu na alikuwa na uwezo wa kulisiammia hilo angalao angetoa data kwamba alilisimamia hapa hadi pale serikali ikashindwa.kumbe mwenzetu tunaweza kumhoji ilikuwaje akasimamia mradi wa shule za kati huku akijua sera hiyo inakuja kutuzalishia failures ambao leo hii ndiyo wako mtaaani na kulifikisha taifa katika alarming stage.(bomu linalokaribia kulipuka)Upande mwingine wa CCM hawakuonyesha jitihada zozote zaidi ya kutoa takwimu na kumshambulia kada wao aliyejiuzulu uwaziri mkuu bila kutoa suluhisho au kuainisha mkakati madhubuti wa kupamabana na tataizo hilo. Hii inaonyesha ni jinsi gani wanasiasa hawa walivyozoea kutumia mataizo ya vijana kujipatia political mileage
Tusikubali kucheka na wale waliochangia taifa hili kufikia hapa,tufanye kazi na tuungane na wale wanaotekeleza kwa vittendo yale wanayosema.Vijana tusikubali sasa kuamuliwa hatima yetu kwa kigezo tu cha umri ati mtu akishafikisha umri wa miaka 40 tayari ana hekima na busara.Katika mikataba yote ya ufisadi hakuna katibu mkuu yoyote wa wizara ambaye alikuwa below 40,wote walikuwa juu ya miaka 40. Hizi ndizo buasara tunazosimamia?
Zitto kuweka hadaharani msimamo wake hakuna tatizo lolote.Mbona wenzetu huko magharibi tunakoiga demokrasia wanaweka misimamo yao mapema?Seneta Barack Obama aliweka nia yake hadharani mwaka 2004,ndiyo 4 years before General Election.Iweje leo hili suala liwe tatizo?au huwa tunaangalia majina ya watu?hebu tujenge hoja ndani ya mantikiVijana tusikubali kuwa daraja,tusikubali kufanywa door mart.
Tatizo kubwa ninaloliona hapa ni kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi bila kuaandaa watu kifikra.Lazima tuapambane na hii status quo haramu.Vijana tujisimamie,tujenge taifa lenye kuzingatia merits na siyo hisani.Tusitumie kigezo cha dini,kabila wala rangi na tusitumie kigezo cha umri bali tuzingatie uwezo wa kufikia kule kwenye change,not only change but Radical change/reforms.
Sasa hili ndilo lengo la Youths patriotic movement(YPM) iliyozuiwa katika usajili kwa ghiliba za wanasiasa wachache wenye hofu na matamanio mfu tu.We are an assemblage of young Tanzanins whose primary aim is to change the course of governance, not from the sidelines this time, but from inside the system. We plan to build a membership of, at least, 20 million people -from every tribe and religion - who will participate in educating Tanzanins about the need to destroy the existing order that is fast running our country out of existence and instituting a new order that will birth equity, fairness, justice and development for all. We will be partisan becausepolitics is too serious a business to leave for the politicians alone.
We will participate fully in the politics of this country. Our army of 20 million people will organize themselves, pick intelligent, courageous, transparent and detribalized candidates for all positions in the 2015 elections and run their campaigns from ground up. There is no age limit, but leadership of the movement will be restricted to young people alone.We are tired of just becoming critics. Aluta Continua isnt one of our favorite quotes. We wont continue with the struggle. WE SIMPLY WILL END THE STRUGGLE by ending the grip of the corrupt in our polity. We owe our generation the duty of saving this country, building it to become a force to be respected in the world, and passing down to our children a nation they can be proud of.