Zitto: Ndio ninautaka urais

Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
@mushi

Zitto hawezi kupata urais kupitia chadema NEVER.

Maximum they can offer ni kumsaidia Mbowe na Slaa beyond that anahatarisha uanachama wake chadema..

Tatizo dogo hajui na ni mbishi..
Kwanini unaamini hivyo?
 
NIMEKUWA nikitafakari mwenendo wa ndugu yangu Zitto, ambapo sasa anasema anataka awe mgombea urais kupitia CHADEMA. Ataupata? Au ndyo kama alivyotaadharisha mchambuzi mmoja, kwamba magamba wanauana kwa lengo la kutaka kuwakilisha chama chao kwenye urais 2015, je wana uhakika kwamba mgombea wa CCM ndye atakeyeshinda!.

Nina wasi ikiwa huu ni ujanja/aggressiveness alionao Zitto katika kutafuta maendeleo yake binafsi kama kiogozi, ama kwa kujua au bila kustuka anatumika kuvuruga angalao kidogo kilichokwishapatikana katika mapambano kuelekea ukombozi kamili.

Kwa hakika sina ugomvi na kwamba anayo sifa ya kuwa kiongozi, na hata kuutamani urais, kama yeye alivyobainisha, wasiwasi wangu ni kwamba alitegwa, akanaswa na sasa yumo mikononi mwa wajanja (waite magamba) wanampeleka wanamtumia wanavyotaka, hana ujanja tena. Japo, hata kama hatumiki, lakini kwa mwendo huu anamfaidisha nani?

Nionavyo mimi hata kama nia hiyo anayo, kuna haja gani ya kuitangaza leo! Maana yake anataka wanachama wagawanyike makundi, kuanzia sasa, wanaomuunga mkono, na wale ambao wanaona Dk Slaa aliwakilisha vyema na hivyo anastahili kuendelea kushika bendera ya chama, labda "mungu akiamua vinginevyo"

Ukichunguza kila Zitto anapoingia na ‘ubunifu' wake, kwa bahati mabya umeishia kuwagawa wana CHEDEMA na wanaowaunga mkono, kurudi nyuma, na hata kugawanyika. Ndiyo maana nahoji, ‘ubunifu' huu ni kwa manufaa ya nani?

Inakuwa hivyo kwa sababu, hatua hizi, kwa bahati mbaya mara zote zimeungwa mkono na kushabikiwa na wapinzani wao wakuu (CCM) ambao ndiyo wanaonufaika/watakaonufaika ikiwa kutatokea mafarakano ndani ya CHADEMA kutokana na mwenendo huu wa Zitto.

Lengo la maoni yangu si kufifisha demokrasia ndani ya chama, bali kama nilivyosisitiza awali, nachelea kukubali kwamba matukio haya hayana ajenda nyuma yake, ikizingatiwa kuporomoka kwa umaarufu aliokuwanao Zitto hapo awali kabla ya kuanza kujiingiza katika matukio yaliyotishia kuvuruga chama, kama lile la kugombea uenyekiti na mara nyingi kuwa na msimamo tofauti na chama tena adharani, mfano kuhsiana na mapendekezo ya kuuzwa kwa mitambo ya Dowans, na ukaribu wake na Makamba jr ambaye kwa bahati mbaya, intelligency (kama wanavyomsifia) haiwezi kunifanya nimwamini, na kwa bahati mbaya sitamwamini hata rafiki yake maana lao ni moja; wanatuzigua tu kwa maneno mazuri. tustukie hila zao maana hawa (akina makamba) ni chimbuko la mafisadi na watakaa wakajivua dhambi hiyo, iweje uwe msafi ujiambatanishe nao.

Nasema hivi kwa sababu wanaotaka mabadiliko ya uongozi, angalau kwa sasa wanajua ni nani takayeongoza mapambano kuelekea ushindi ambaye ni Dk. Slaa, labda likitokea la kutokea. Na kwa sababu hiyo, ikiwa mazingira yatabaki ilivyo sasa, Zitto awezi kuibuka kuongoza (kupeperusha bendera ya) CHADEMA kuishinda CCM na hila zake.

Ni bora wanamageuzi wanaotaka mabadiliko, wakatulia, siku ikifika kama hakuna cha maana kinachoweza kuwafanya wabadilishe mgombea, basi Dk Slaa apeperushe tena bendera, vinginevyo uamuzi ufanyike wakati ukifika
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Kwanini unaamini hivyo?

Kwasababu anatakiwa awe na nafasi kama ya kawawa kwa nyerere otherwise anatafuta kutupwa nje ya chama..kwasababu huo ni utukutu na usumbufu kwa wakubwa wa chama..
 
Zitto bado mapema mno ukifuata nyayo za kina LOWASSA Itakugharimu mno still we have time acha haraka kama kafulila maana unaweza onekana una mkakati wa siri ukajimaliza mwenyewe kwani bado mapema mno.
 
Haijasemekana ni nani atapeperusha bendera ya cdm mnamo miaka 3 ijayo, hivyo hakuna sababu ya kuzibana vinywa muda huu. Kama hujui ni kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo. Wanaogawanyika hawana misimamo
 
Mkuu Mwanakijiji,
Hizi soga za wanajamvi hapa zinazuia nini kule arumeru? La muhimu makamanda wanaendeleza mapambano.
Huyo anayejiita msomi wa chuo kikuu haikuwa sawa kumsema Zitto mambo ya uongo, ilikuwa sahihi Zitto kumjibu.


Basi miye nina tatizo? wala sina nawaangalia tu...
 
sitampa kura yangu na wala hatutampitisha.

Yaani hamtampitisha kwa kuwa Chama ni cha Kwenu? sawa hata kama nichenu kwanini msimpitishe mwenye uwezo huoni hizo kauli zinacreate loop hole ya magamba kupenyeza propaganda ya ukabila na mwenzio ameshaingiza element za udini ee Mungu tusaidie watz tumekwama!
 
Zitto hawezi kupeperusha bendara ya chama kwa urais NEVER

Zitto nafasi yake chadema ni kama kawawa kwa nyerere period

Akitaka kwenda beyond (kubeba mabegi ya maboss wake mbowe, slaa, JJmnyika) anahatarisha kufukuzwa kwenye chama..

Zitto wewe unatakiwa uwe msaidizi wa wakubwa, period.
 
Zitto, much the same as youth joblessness to the nation, is a time bomb awaiting to blow up Chadema.
 
Georgina ni muislam kwa sasa

Huyo mchagga unamsema wewe? kama yupo ajitokeze tu tutamshambulia Lipumba..lakini kwasasa hakuna mwanamume aliyesema georgina na mke wake kama asemavyo mahimbo na josephine

usipindishe mada mkuu Slaa anazini au mnataka kubadili maandiko kwasababu ya mahaba, kwani si ajabu kwenu maana kuna kanisa limeshakubali shoga kuwa priest..just declare..

Topical,

..jamaa wa Kichagga yupo, siku CCM wakimhitaji ataibuka tu.

..umesahau 1995 jinsi CCM walivyokuwa wanazunguka naye akidai mke wake toka kwa Prof.Lipumba?

..pia Prof na Georgina walifunga ndoa mwaka gani?
 
Je mjadala huu tija wiki hii ambamo Chadema imo vitani kule Arumeru? Ningetamani mjadala huu uanzishwe na mtu mwingine hasa wa CCM anayetafuta ku-divert attention ili watu tusiangalie yanayotokea kule Arumeru. Kwamba, mjadala huu unaanzishwa na mwana Chadema inatia shaka sana. Tuuweke kiporo, tuanze nao tarehe 2 April baada ya kujua mbivu na mbichi huko Arumeru.
 
USHAURI: Zitto umejieleza vizuri ila kumbuka mara nyingi kwenye siasa mtu huwa ANAJIMALIZA Mwenyewe unaweza kuwa unadhamira nzuri na unelewana sana viongozi wenzako lakkini nje watu tunaanza kupata mashaka untumiwa kuchelewesha ukombozi wa mtanzania masikini kwani ni ukweli usiopingika kuwa dr Slaa tayari ni mtu anayekubalika na kuaminiwa na watu wote(vijana, wazee na kinamam) hata watu wa vyama vingine wanamkubali mno pamoja na ccm wenyewe .......... nakubali umekijenga chama umekuwa role modal by inspiring many including me but watch your comments becouse ur not mere citizen it may cost your in politics ( not every body can understand u)
 
Hakuna ubaya mtu akitueleza nia yake au lengo lake kisiasa.
 
kula kwa mtindo said:
Hadithi yako inatufundoisha nini?
Urais unakutafua mhusika, Urais hautafutwi!!Tizama Picha


ukweli mada ni defu sana kiasi mtu unaishia njiani kusoma. Nimeelewa kuwa urais unauhitaji na kwa namna fulani unaweza. Kama jakaya kaweza (?) why not you? Kuna hoja hapo juu ya mdau kuwa katiba inasema ni miaka 5 then 5. Sasa kama umefanikiwa kuongoza miaka 10 ukawa na miaka 50 then tutegemee nini? Si uchakachaji tu hapo? Miaka 50 kustaafu urais bado mdogo sana! Zitto utakuja kuwa Rais. Take it from me if the party maintain this pace, ila kwa sasa hata chama kitakukatalia. Wananchi wanaweza kuwa na mahaba nawe kwa sasa na wakasema uwe Rais lakini madhara yake mbele mabaya. Ukiwa na miaka 50 utakuwa Rais. Jiandae kwa urais 2025

Kwa rumous za mitaani wanaojua kilichojili kwa JK wanasema hakuwa na wazo wala mpango wa kugombea,ila kama kawaida tulishasema Urais umfuata mhusika.JK hakuitaji Urais wala hakujipeleka kuonyesha kuwa anaitaji kuwa Rais kwa ile mara ya kwanza mwaka 1995,ila alipofuatwa na watu wazima ambao yeye anawaamini na hakutegemea wamwambie kauri hiyo ndio walipomuinua dhamira ya kuanza kuona kuwa hivi kama wazee hawa wananiambia nifanye hili kumbe naweza.Na hiyo ni hali ya binadmau yoyote yule tena zinangatia mtoto wa kiume kwa kuwa watoto wa kiume ni tofauti kibailojia katika swala la kumilki power.Wakati mtoto wa kiume power kwake ni silaha na kitu muhimu kwa mtoto wa kike ni tofauti sana.Hata kama ingekuwa ni mimi binafsi lazima kungekuwa na hisia fulani zakuanza kuzingatia.

Na ndio maana ndani ya CCM uwa nasema picha usema mengi.

attachment.php


attachment.php

Baada ya kukubaliana kuwa nguvu yake inamsupport Mzee BMW mwaka 1995 Baba wa Taifa JKN na JK.Ndani ya Dodoma uteuzi wa mgombe Urais Mwaka 1995.Hapa ndio wengine kupitia picha sisi ambao tulikuwa makinda uenda tunajifunza kupitia picha Mwalimu alitoa kauri za umri akimaanisha maana ambayo wengine wamebaki kushupalia number baada ya content ya Candidate ambayo Mwalimu ndiyo aliyozingatia ipatikane toka kwa mtegemewa.
 

Attachments

  • Mwalimu & JK 2.jpg
    Mwalimu & JK 2.jpg
    37.5 KB · Views: 168
  • Mwalimu & JK 3.jpg
    Mwalimu & JK 3.jpg
    27.2 KB · Views: 168
Ndio tatizo lenu watu wa kaskazini mnalazimisha Slaa 2015 agombee urais ili hali atakuwa mzee na hatufai tena. Na isitoshe mzee hana jipya kwa sasa, awaachie vijana wakina Zitto. Kuhusu umri katiba ijayo tunalirekebisha hilo na Zitto ambae ni chaguo la CDM wengi ata qualify.

zitto ana haki kama wengine lakini anapaswa awe na Subira. Kwangu mimi Slaa yuko juu kuliko mwingine yeyote si chadema tu. Ndiyo Rais anayetufaa kwa namna yoyote ile. Zito avumilie 2050. Na kama tunataka kijana basi ni Mnyika au Nape kwa chama chao. Mawazo yangu.
 
Haijasemekana ni nani atapeperusha bendera ya cdm mnamo miaka 3 ijayo, hivyo hakuna sababu ya kuzibana vinywa muda huu. Kama hujui ni kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo. Wanaogawanyika hawana misimamo

Mimi naamini kila mtu anao uhuru wa kusema anautaka uraisi, hii ndio freedom yenyewe. Lakini timing ya kauli kama hizi ndio inayoleta maswali ya kujiuliza pengine wengi wetu tunaishia kukosa majibu. Hiki kijitabia cha mtu kuona watu wanamuandika andika kwenye magazeti kila siku akafikiri kila kitu anaweza ni hatari sana. Mh. Zito anakurupuka mambo mengi sana, siasa makini haziendi namna hiyo, mtu anajengwa kwenye chama na kuna wakati unafika unakuwa automatic choice, sio lazima ujitangaze bila taratibu.

Wakati ule anataka kugombea uenyekiti, ijapokuwa ni haki lakini mtu unajiuliza hivi kweli kwa umri wake wakati ule tuseme 33 hata ukiupata huo uenyekiti je unaweza kuvutia watu wa rika zote kujiunga na chama? je umekomaa kiasi cha kutosha kuweza kuhimili hiyo nafasi? Hekima nyingine jamani zinakuja na umri, kwa nchi zetu za kiafrika na tamaduni zake Mh Zito bado hawezi kukabidhiwa chama akiongoze, ni mtu anayetakiwa kulelewa na kukuzwa na chama kwa ajili ya miaka ijayo.

Hata nafasi anayosema anaitaka ya uraisi bado mda wake, he is not matured enough. Amelewa sifa na anatumiwa vibaya. Chadema lazima msimame makini na mtu wa namna hii, akileta za kuletwa mnafanya maamuzi magumu maana he always create unnecesary distractions. Chama ni taasisi lazima kiheshimiwe kama taasisi, chama kinapogeuka kuwa ni majina ya watu huwa hakina muda kinakufa. Kunao watu wengi tu, wazuri wenye mvuto mkubwa wa kiuongozi ijapokuwa huwezi kuwasikia kwenye magazeti kila kukicha, wapewe nafasi.

Chaguzi ndani ya vyama ziwe mahali ambapo talents zinavumbuliwa, mtu anasikilizwa hoja zake,vision zake na strategies zake na kama ziko convincing mtu apate nafasi, sio hii tabia ya kushabikia majina yasiyo na chochote ndani yake. Ndio maana vyama vya siasa huwa vinakufa maana vimejengwa juu ya majina ya watu. Ati watu wanakuwa na makundi, upuuzi mkubwa kabisa huu badala ya kuangalia ni nani anatoa sera za maana yunashadadia majina, mara Zitto, mara Slaa mara Mbowe n.k Haiwezekani mtu ambaye ni mwanachama wa kawaida tu wala hana kashfa wala nini akapewa nafasi mbele ya kamati akajieleza akapita kwa ubora wa hoja zake! lini tutafika hapo?
 
Je mjadala huu tija wiki hii ambamo Chadema imo vitani kule Arumeru? Ningetamani mjadala huu uanzishwe na mtu mwingine hasa wa CCM anayetafuta ku-divert attention ili watu tusiangalie yanayotokea kule Arumeru. Kwamba, mjadala huu unaanzishwa na mwana Chadema inatia shaka sana. Tuuweke kiporo, tuanze nao tarehe 2 April baada ya kujua mbivu na mbichi huko Arumeru.

Mkuu wangu ndiyo hiicho tu ambacho kinanitatiza. Majibu ya Zitto ni mazuri tu na yanaweza kuwashawishi watu vizuri tu. Kama mtu atakubaliana nayo au la hilo ni jambo jingine. Lakini, ilipaswa kutolewa wiki moja kabla ya uchaguzi wa Arumeru na viti kadhaa vya udiwani? Hivi kuna tishio gani kwa wiki hii kwa Zitto kutaka kugombea Urais? Hakuna kikao cha kutafuta wagombea, hakuna mchakato wa kutafuta wagombea, hakuna chochote kinachohusiana na Urais wa 2015. La pili ni kuwa Zitto anamjibu mtu aliyeandika makala; mtu ambaye kwa kweli kabisa ametoa maooni tu na labda hayajapangwa vizuri. Zitto asingekubali kuingizwa kwenye hili.

Nimemsema juzi Mnyika naye kwenda kwenye kipindi cha Diva na kusababisha watu wazungumzie mambo ya kama ana mchumba au la! Really? Do these young friends of ours show the temperance and sobriety of potential leader? Do they make their judgments wisely? Binafsi nakwazika zaidi na jinsi wanavyopima haya mambo kuliko substance ya hivyo wanavyovizungumzia. Jibu la Zitto kwa mfano lingetolewa wakati wa mchakato wa kumtafuta mgombea lingekuwa potent katika kujenga hoja ya yeye kugombea lakini leo in March 2012?

Slaa kwa mfano yuko presumed na watu wengi tu kuwa atagombea tena 2015; wananchi na watu wengi - hasa waliompigia kura - wanaamini kuwa anastahili kugombea tena. Lakini yeye mwenyewe hajasimama kutetea kuwa anastahili au ni haki yake hata kama anaonekana kuwa ni presumed candidate. Lakini hasimami kupush kuwa yeye ndiyo awe mgombea ni mashabiki wake. Zitto ana watu wanaopenda awe Rais na hili si ajabu kwani Mbowe naye bila ya shaka ana watu ambao wangependa awe Rais vile vile kama Lowassa alivyo na watu wanaotaka Urais. Lakini hujamsikia Lowassa kuwa anatkaa kuwa Rais japo inaonekana hivyo.

Sasa tuko kwenye wiki muhimu kweli ya uchaguzi halafu kutwa nzima ya leo watu wanazungumzia kitu ambacho hakipo! Watu wanakwazana na kuhisiana vibaya kwa hazina isiyopatikana bado? Kama siyo ku-self destruct ni nini? Angalia magazeti yamepokea habari hii na kuifanya kubwa na watu wataizungumzia sana come Monday; Zitto atajikuta anatoa tamko jingine kujifafanua (labda akalichochea moto zaidi) na watu wakasahau kabisa kufuatilia ugomvi wa CCM na CDM huko Arumeru!

This is just sad. Nendeni mkashinde kwanza halafu mkishashinda anzeni kuzungumzia mambo ya vyeo. Sasa hili liwe limefikia mwisho - Zitto anataka kuwa Rais that settles it. Hakuna utata tena - watakaopenda au kuchukia hilo lwao lakini keshalisema na ndivyo lilivyo. Sasa kama ataanza kusukumiza kuwa yeye ndio awe mgombea 2015 - hata kama anastahili hiyo ni haki yake lakini atakuwa anajua pia kuwa anajiexpose kupingwa na watu wengine na kwa chama kinachotaka kuiondoa CCM madarakani hekima nzima ya kuanza kugombania "ugombea wa Urais" mapema hivi inabidi tufikirie sana.

Binafsi ningefurahi sana kuona Zitto akituandikia wiki moja kabla ya uchaguzi hoja ya kwanini wananchi watakaopiga kura Arumeru Mashariki na sehemu nyingine wasiichague CCM na badala yake wachague wagombea wa CDM. But well matamanio huwa hayana mbawa vingenevyo yangeruka na kuwa kweli.

Vinginevyo, CDM italazimika/lazimishwa ifanye uteuzi wa mgombea wake wa Urais mwaka huu ili ajulikane yaishe.
 
......I don wana pass through no thread..... jus that.... Zito is f*kd up.... NO WAY......... HE NEVER SHOULD EVER HAD SUCH A DREAM......
 
Mimi naamini kila mtu anao uhuru wa kusema anautaka uraisi, hii ndio freedom yenyewe. Lakini timing ya kauli kama hizi ndio inayoleta maswali ya kujiuliza pengine wengi wetu tunaishia kukosa majibu. Hiki kijitabia cha mtu kuona watu wanamuandika andika kwenye magazeti kila siku akafikiri kila kitu anaweza ni hatari sana. Mh. Zito anakurupuka mambo mengi sana, siasa makini haziendi namna hiyo, mtu anajengwa kwenye chama na kuna wakati unafika unakuwa automatic choice, sio lazima ujitangaze bila taratibu.

Wakati ule anataka kugombea uenyekiti, ijapokuwa ni haki lakini mtu unajiuliza hivi kweli kwa umri wake wakati ule tuseme 33 hata ukiupata huo uenyekiti je unaweza kuvutia watu wa rika zote kujiunga na chama? je umekomaa kiasi cha kutosha kuweza kuhimili hiyo nafasi? Hekima nyingine jamani zinakuja na umri, kwa nchi zetu za kiafrika na tamaduni zake Mh Zito bado hawezi kukabidhiwa chama akiongoze, ni mtu anayetakiwa kulelewa na kukuzwa na chama kwa ajili ya miaka ijayo.

Hata nafasi anayosema anaitaka ya uraisi bado mda wake, he is not matured enough. Amelewa sifa na anatumiwa vibaya. Chadema lazima msimame makini na mtu wa namna hii, akileta za kuletwa mnafanya maamuzi magumu maana he always create unnecesary distractions. Chama ni taasisi lazima kiheshimiwe kama taasisi, chama kinapogeuka kuwa ni majina ya watu huwa hakina muda kinakufa. Kunao watu wengi tu, wazuri wenye mvuto mkubwa wa kiuongozi ijapokuwa huwezi kuwasikia kwenye magazeti kila kukicha, wapewe nafasi.

Chaguzi ndani ya vyama ziwe mahali ambapo talents zinavumbuliwa, mtu anasikilizwa hoja zake,vision zake na strategies zake na kama ziko convincing mtu apate nafasi, sio hii tabia ya kushabikia majina yasiyo na chochote ndani yake. Ndio maana vyama vya siasa huwa vinakufa maana vimejengwa juu ya majina ya watu. Ati watu wanakuwa na makundi, upuuzi mkubwa kabisa huu badala ya kuangalia ni nani anatoa sera za maana yunashadadia majina, mara Zitto, mara Slaa mara Mbowe n.k Haiwezekani mtu ambaye ni mwanachama wa kawaida tu wala hana kashfa wala nini akapewa nafasi mbele ya kamati akajieleza akapita kwa ubora wa hoja zake! lini tutafika hapo?
Kwa faida ya CHADEMA wafike sehemu huu upuuzi unapaswa kwisha kwa kuwa kuendelea kufuga kidonda ni kukalibisha magaonjwa na hatimae kilema.Kwa sasa Zitto kuingiza CDM kwenye michezo hii ni kutengeneza mazingira ya kuinyongonyeza CDM kisayansi,hivyo wanachedema kwa kuwa lengo ni ukombozi someone should stop this kind of game,manke watu wazima ambao imewachukua karibu miaka ishirini na ushee kusimamisha chama leo ambacho kinainyima CCM usingizi kisha wanaibuka vijana kuanza mbwembwe zisizo na nidhamu na maadili hata kama ujana ni maji ya moto heshima nayo ni mlango wa adabu.

CDM wafike sehemu wasitishe kama si kuondoa kabisa tabia hii ya kuvuluga nguvu ya umoja wa wanachama na wapenzi wa CDM kukaa kama wamoja kwenye maswala muhimu na matokeo yake kuanza kugawana wanachama na wapenzi as if sio chama bali ni group la makinda wasiojua wanachokitaka.Hadhi ya CDM sasa ni KITAIFA hivyo tuondoleeni tabia ya kuendesha mambo ya style ya baadhi kuona CDM bila wao HAKUNA KINACHOWEZEKANA.Vinginevyo HAKUNA sababu ya kuwa na CDM kama wamecopy na kupaste style ya KUJISIFIA SIFIA MABARABARANI baada ya kutumia muda huo kukijenga chama na kutangaza sera za chama popote pale wanapopata nafasi ya kuwepo,ili kuwaambia watanzania kuwa wawe na imani nao na kuwa wanauwezo wa kuwaletea maendeleo na maisha bora vizazi kwa vizazi bila hofu.

TO MUCH OF ANYTHING IS HARMFULL,TIMIZENI WAJIBU NA MALIZENI HII TABIA,VINGINEVYO MSIUE WATU KWA KUWAAMINISHA WAWAPE SUPPORT HUKU, MNA MITABIA MICHAFU KULIKO CCM,HIVYO ISIJE KUWA NI MALA MIA YA CCM,KULIKO KUWA NA WATU AMBAO MKIWATAZAMA MNAULIZANA KWELI HAWA .........???????????????????????
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom