Zitto: Ndio ninautaka urais

Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
Zitto anafaa walau kuanzia 2025 atakuwa amepikwa na kukomaa vizuri.Kwa hivi sasa ni nafasi ya Dr Slaa.Dr Slaa kwa sasa hana mbadala ndani ya CDM.Ni kujilisha upepo kudhani kuna mtu mwingine atapitishwa kugombea Urais zaidi ya Dr wa ukweli walau kwa sasa.CDM ina vijana wengi na hakika huko Mbeleni kina Zitto na Mnyika na wengine ni hazina kubwa ya chama

Hatutaki wazee sisi, na mkimuweka Slaa mjue mmeisha shindwa tayari. Msitake kule mambo ya Senegal hapa
 
Ndio tatizo lenu watu wa kaskazini mnalazimisha Slaa 2015 agombee urais ili hali atakuwa mzee na hatufai tena. Na isitoshe mzee hana jipya kwa sasa, awaachie vijana wakina Zitto. Kuhusu umri katiba ijayo tunalirekebisha hilo na Zitto ambae ni chaguo la CDM wengi ata qualify.

kijana kikwete mliyemchagua alisaidia nini taifa?ameshindwa mpaka na wazee kina mwaikibaki!! :crazy:
 
sitampa kura yangu na wala hatutampitisha.

Nakupa 5 Angel Msoffe,hata mimi hawezi pata kura yangu!puppet mwenye uchu na madaraka,si ajabu wana c.c.m wengi kumpigia chapuo kwa kua wanajua atadhoofisha upinzani/chadema
 
Kwa katiba la Tz la kuwa Rais on 10 years bases.. Mtu mwenye miaka 35 akiukwaa urais given kwenye 45 atalazimika kuwekwa kando Kama sio 40. Na Kwa umri huu ndio Wa ujana Lakini unapachikwa Jina la mstaafu.

Ni wazi sehemu ya maisha yako itakuwa kula kulala. Mara nyingi kwenye nchi ambazo hawana democracy hata mtoto anaweza kuwa mtawala but he/she will be there hadi anazeeka.. Na ikitokea nchi ya kidokrasia yenye mafungu ya kuongaza Kwa miaka kadhaa Na ikatokea kiongozi kijana.. Lazima atafanya jitihada za kuchakachua katiba ili ajinemeshee miaka zaidi.

Vijana wengi wa kwetu ni wakirupukaji, wabi nafsi Na wasaliti. Hang'ang'ania vyeo Na nafasi za juu sana za uongozi bila kufikiria after uongozi kuisha itakuwaje.. Mtu hata familia Hana, hajajua house management and children care ikovipi Leo anag'ang'ana kuwa Rais. Ni kukurupuka sana.

Sisemi Rais lazima awe Ameoa ila Kwa utanzania wetu Na maisha Haya, familia ni uongozi kamili na ukishindwa kimanage fimilia sahau kiwamanage wananchi.. Kama huamini Njoo huku CCM, Angalia Kati ya wabunge wote, nani mwenye historia nzuri ya ndoa yake.. Hamna, naskia alikuwa warioba tu, njoo Kwa wabunge wanawake, orodhesha wenye ndoa... Kapa.. Kama ipo ya kuunga sana Kwa vijiti. Sasa Kama viongozi hawa weledi tu wa family care ulishawashinda saa ngapi wataweza kuliongoza Taifa.
 
na kwa cdm huyu ndio mtu anae faa kuwa rais. Wengine wote wakina m & s company wana tamaa tu za madaraka. Nawaomba wana cdm muungeni mkono zitto na apitishwe na chama

ganga yako,ya magamba hayaeleweki waparamia ya wengine.acha kimbele mbele tulia njaa,unanuka kwa ufisadi.
 
Zitto atapata kura chini ya laki tano.wewe unadhani kupendwa na watanzania ni kazi ndogo na unafiki wake.mimi sitampigia kura !Watu wanaangaika kupigania chama mpaka wanafungwa,yeye atujamuona kwenye hata maandamano.na nani atapush hoja ya kupunguza miaka kuwa 35?...hahaha.
 
kijana kikwete mliyemchagua alisaidia nini taifa?ameshindwa mpaka na wazee kina mwaikibaki!! :crazy:

Mkimuweka Slaa kura utampigia ww na familia yako ! watanzania hatuko tayari kutawaliwa na Slaa na uzee wake
 
Ndugu zangu. Naomba msome makala nzima kabla ya kuchangia. Msichangie kwa kusoma kichwa cha habari tu. Hii ni makala nimeandika kama majibu kwa makala ya mwanazuoni mmoja kuhusu umri wa Urais.

Nimesema wazi, kuutaka Urais na kuupata ni mambo mawili tofauti. Kwanza lazima chama changu kiniteue. Kama chama kikiona bado lazima nikubaliane na chama. Kama chama kikiona kuna mwanachama mwingine ana uwezo zaidi yangu lazima nimwunge mkono huyo. Hata kama chama kikiniteua lakini wananchi lazima wakubali. Kwa hiyo unaweza kuutaka Urais lakini usiupate!

Pili nimejibu hoja za ubaguzi, hatari na matabaka za mwanazuoni huyo. Ni vizuri MoD akachukua makala hiyo na kuiweka juu kabisa ili watu wachangie jambo walilolisoma.

Miye nitaweka makala hiyo kwenye blog yangu zittokabwe.com
 
chadema tunaipenda,chadema ndo mkombozi wa Tanzania,SLAA for presidency 2015, zitto asubiri...
 
Mkimuweka Slaa kura utampigia ww na familia yako ! watanzania hatuko tayari kutawaliwa na Slaa na uzee wake

ndo umeulizwa huyo kikwete wenu mnayemuita kijana amefanya nini??????
 
Hatutaki wazee sisi, na mkimuweka Slaa mjue mmeisha shindwa tayari. Msitake kule mambo ya Senegal hapa

Wenye akili mgando ndio wenye mawazo hayo,watu makini uangalia yule atakaeleta chachu ya maendeleo katika nchi,suala la uzee au ukijana si tija!angalia zambia au Germany,marais wao wana umri gani?ukirudi Kenya je?mfano wako wa Senegal ni mfano mfu kabisa,Wa Senegal wanachompinga Wade ni kukiuka kwake katiba na si kwa ajili ya uzee wake!changamsha ubongo!
 
chadema kama inataka kuopekua huu mpasuko unaowakabili mgombea ni huyu..........
 
Hatutaki wazee sisi, na mkimuweka Slaa mjue mmeisha shindwa tayari. Msitake kule mambo ya Senegal hapa

Mkuu utatoka povu sana lakini siwezi kuficha hisia zangu wala ninachoamini.Dr Slaa atakuwa Rais bora mwaka 2015 kuliko mtu yeyote ndani ya CD M.Huu ni mtazamo wa wengi ndani ya CDM kwa sasa.Slaa anaungwa mkono na wazee na vijana ndani ya chama.Huu ndio ukweli.Kina Mbowe,Zitto na Lissu tunawahitaji wawe wabunge ili Slaa apate serikali imara.Mimi siwezi kuficha ninachoamini.Anayeibuka sasa kubishana na Slaa anapoteza muda wake na anataka kujiangamiza kisiasa mwenyewe.
 
Kwani kuna ubaya kwa Zitto kugombea urais? ni haki yake kikatiba, na chadema ni chama cha kidemocrasia ilani ya chama chetu haimzuii Zitto kufanya hivyo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom