Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
Wakati huo CHADEMA kilikuwa chama ambacho watu wanakikimbia isipokuwa watu wa Kigoma na Kilimanjaro, Shinyanga, Karatu na Ukerewe. Vijana walikuwa wanajipambanua na CCM zaidi ama CUF au TLP kuliko hiki chama cha mabwanyenye. Huu ni mwaka 2001, muongo mmoja tu uliopita. Mimi na Freeman Mbowe ndio tumefanya mabadiliko yote yanayoonekana CHADEMA. Tumeingiza watu wapya, tumeandika Katiba upya. Ilipofika mwaka 2005 tukasema Freeman Mbowe nenda kwenye Urais, tulijuwa tunashindwa lakini tulitaka kujenga chama chetu. Tukapata Wabunge. Wabunge Wakafanya kazi. Tukaingia mwaka 2010 katika uchaguzi kama chama imara tunachokwenda kuchukua dola.

cc Mwigamba , Kitila , msajili wa vyama
 
Huu ni mwaka 2001,
muongo mmoja tu uliopita. Mimi na Freeman
Mbowe ndio tumefanya mabadiliko yote
yanayoonekana CHADEMA. Tumeingiza watu
wapya, tumeandika Katiba upya. Ilipofika
mwaka 2005 tukasema Freeman Mbowe nenda
kwenye Urais

Leo hii kuna Vimisukule vinamtukana Zitto wakati 2001 vingine vikikuwa chekechekea na kuna baadhi ya makamanda walikuwa wanakula good time CCM
 
Last edited by a moderator:
usione watu wamefanikiwa, wametoka mbali sana, tatizo la watanzania tumekaa kupondea watu tu ili hali sisi wenyewd hatuna hata zuri moja la kukumbukwa, wasikukatishe tamaa, fanya mambo yako kadiri mungu akuwezeshavyo binadam hawana jema, hata humu wapo na muda si mrefu watakuja na majibu yao ya hovyo, wamejaa chuki tu hawana hoja yoyote ya maana
 
Nimeipenda sana hii sehemu
Hata hivyo kazi hii hata kama naitaka ni lazima
wenye nchi waamue kunipa kazi hii. Ni lazima kwanza Chama changu kiseme wewe ndio mwanachama unaestahili kuifanya kazi hii. Ni lazima Watanzania wengi waseme wewe ndio mwananchi mwenzetu unayeweza kuchukua jukumu hili. Kuitaka tu haitoshi. Ni lazima wananchi wakuamini na kukupa jukumu hili. Sasa kama wananchi watasema huyu Zitto anapaswa kubeba jukumu hili mwaka 2015 tuache iwe. Kama watasema hapana wewe bado mpaka mwaka 2020 au hata 2025 tuache iwe hivyo. Pia Kama hawataki kabisa tuache iwe hivyo
Mimi nimeipenda sehemu hii hasa kwenye red.
Huu ni mwaka 2001, muongo mmoja tu uliopita. Mimi na Freeman Mbowe ndio tumefanya mabadiliko yote yanayoonekana CHADEMA. Tumeingiza watu wapya, tumeandika Katiba upya. Ilipofika mwaka 2005 tukasema Freeman Mbowe nenda kwenye Urais,
 
Mimi nimeipenda sehemu hii hasa kwenye red.

Mkuu hiyo red wameshaisaliti na sasa wapo busy na kupaza sauti kwa kutumia spika za CCM na allowance ya hapo Lumumba,reje mjadala wa katikati ya wiki wa Star tv ndani wakipewa collable wakina Mchange,Mwampamba na Yona wa TEMEKE huku mabosi wao wa usaliti wakiwatumia madesa kwa msgs!!!
 
Mkuu hiyo red wameshaisaliti na sasa wapo busy na kupaza sauti kwa kutumia spika za CCM na allowance ya hapo Lumumba,reje mjadala wa katikati ya wiki wa Star tv ndani wakipewa collable wakina Mchange,Mwampamba na Yona wa TEMEKE huku mabosi wao wa usaliti wakiwatumia madesa kwa msgs!!!

hivi una uhakika au ndo unatoka povu tu, eti buku 7 za lumumba na ninyi mnalipwa sh. ngapi?
 
Leo hii kuna Vimisukule vinamtukana Zitto wakati 2001 vingine vikikuwa chekechekea na kuna baadhi ya makamanda walikuwa wanakula good time CCM

-CCM imetumia Sh bilioni 3,659,000,000/ Kumpa ZITTO ili AIHUJUMU CHADEMA. Ebu fikiria Ikiwa kujenga DARASA 1 ina gharimu Tsh Milioni 10 vingejengwa vyumba vya Madarasa 365, sawa na Shule 45. Kama zahanati 1 Itagharimu Tsh milioni 20 ingejenga Zahanati 182. Ikiwa Kuchimba Kisima kimoja ni Tsh million 10 vingechimbwa visima 365.Vocha 1 ya kilimo ina ghalimu Tsh 100,000/ Wakulima 36,590 wangepata vocha. Kwa hali hii kweli ZITTO ni Mzalendo kwa nchi? je anafaa kuwa CHADEMA? TAFAKARI! Tuma Ujumbe huu kwa Watu wengi wasiopungua MIA Utakuwa MZALENDO HALISI.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom