Huyu kaka anamapungufu. Nasikia eti hajaoa!!!!. Hii post ni ya wababa, kijana kama huyu hajatulia, wachumba watamsumbua, Ikulu itajaa vichupi so badala ya ku deal na issue atadeal na vichupi
Na wewe tangu lini ukawa mshauri wa Chadema?
Huyu kaka anamapungufu. Nasikia eti hajaoa!!!!. Hii post ni ya wababa, kijana kama huyu hajatulia, wachumba watamsumbua, Ikulu itajaa vichupi so badala ya ku deal na issue atadeal na vichupi
Basi akagombee chama kingine lakini sio chadema. Lazima chama kiwe na malengo. dr.Slaa alishapiga jaramba 2010 kilichobaki ni kuingia uwanjani(ikulu). Zitto bado anao mda wa kujipanga na umri unaruhusu. hatutaki kupoteza nguvu kazi kama Slaa ipotee hivihivi. Inabidi dr.Slaa atoe mchango wake kwa taifa lake nasi tumfaidi.
Mkuu Nyange, Rais Khama wa Botswana hajaoa lakini anachapa kazi vizuri sana. Kwangu mimi cha muhimu ni kumpata mtu anayeelewa matatizo ya nchii na aoneshe nia, dhamira na uthubutu wa kuyatatua. And if takes mpenda vichupi to fix this country mimi binafsi sioni shida. Kwani vichupi wamelazimishwa? Si unaona hawa wenye ndoa lakini?
Na wewe tangu lini ukawa mshauri wa Chadema?
Na kwa cdm huyu ndio mtu anae faa kuwa Rais. Wengine wote wakina M & S Company wana tamaa tu za madaraka. Nawaomba wana cdm muungeni mkono zitto na apitishwe na chama
Matola,
1.Ati Alliance na coalition zitanipeleka pabaya?pabaya ni imagination tu,ni wapi huko? Acha kunitisha,sitishiki!
2.Kama nataka kujifunza siasa ili nifike mbali?Mbali ni wapi mkuu? Naona huu ni mwendelezo wa siasa za ubinaqfsi/unafiki.Unamanisha nijikite kwenye siasa za kujineemesha?huku ndiko unakopaita mbali? Sihitaji kujifunza siasa ya aina hii.
Kuhusu kufuata nyayo za mtu,mimi siyo aina hiyo ya copy and paste.siasa za copy and paste ndizo zilizotufikisha hapa.nina misiammo yangu na nina principles zinazoniongoza kwenye siasa na uongozi hata kama ni nje ya siasa.
Kuhusu kufuata Nyayo za Mnyika nimeshakujibu hapo juu,huyu ni kiongozi wangu ni rafiki na huwa tunashauriana mambo mengi na tunaheshimiana ila usinichagulie kitu cha kufanya/kufuata
3.kuhusu akina sugu sijui wamefanyaje,hayo ni yao.Kila mtu ana historia yake.Kuhusu kugombea ubunge Mungu akipenda nikifika salama 2015 nitagombea hilo halina mjadala.Hata 2010 ilikuwa nigombee lakini nilikuwa nje nikimalizia mitihani yangu ya Masters.Nilipokuja mchakato ulikuwa umefika mbali,hivyo niliamua kutogombea na nikaelekeza nguvu kukisaidia chama changu hasa Rafiki yangu John mnyika,Halima mdee,Regia Mtema (R.I.P) na majimbo ya Moshi mjini na jimbo la Rombo ambako waliamini kwamba mramba hawezi kushindwa uchaguzi.
Ati kama najiamini?Ndiyo ninajiamini sana.....!
4.Kuhusu kusimama kwa miguu yangu miwili: Hata sasa nasimama kwa miguu yangu miwili,nina kazi na ninafanya kazi kwa bidii.
Kwenye siasa sitegemei kubebwa,siamini katika siasa za kubebabana labda tubebane katika msimamo na vision basi.Naamini katika principles.Niligombea uchaguzi wa BAVICHA sikubebwa zaidi ya kutarajia kubebwa na wapiaga kura ambao wangekubaliana na kile nilichokuwa ninaamini.Ninaamini katika maamuzi ya ballot box,siamini katika remote control.
Watu wa kubebwa wanajulikana,cowards wasiojiamini na kusiamamia wanachoamini wanajulikana.Mkuu hapa utanitaka radhi
Ndio tatizo lenu watu wa kaskazini mnalazimisha Slaa 2015 agombee urais ili hali atakuwa mzee na hatufai tena. Na isitoshe mzee hana jipya kwa sasa, awaachie vijana wakina Zitto. Kuhusu umri katiba ijayo tunalirekebisha hilo na Zitto ambae ni chaguo la CDM wengi ata qualify.
Na wewe bana..acha uoga wa kijinga na kutishwa na so called usalama..wazungu wanakupenda wewe? mbona hujiulizi hilo swali kabla ya kumtwisha Ben mzigo huo?
Chadema msipomdhibiti huyu mtatuandalia bomu.
Huu ushirika wako Ben saanane na akina Zitto huko mbele utazaa uasi wa kutisha siyo ndani ya chama tu hata usalama wa nchi. Naona kila dalili za uasi wa vijana dhidi ya wazee.
Usalama wa taifa sasa inabidi ufanye kazi kushughulikia hizi mbegu mapema. Kwa bahati mbaya huyu ni mtu wa visasi na hata sasa nilishaongelea kuhusu chuki yake dhidi ya wazungu na wakenya, tunaandaa akina Julius Malema au akina Adolf Hitler bila kujijua.
Kujiamini najua unajiamini sana sijui ni kitu gani kinakupa jeuri kiasi hicho; hata balozi Eva Nzavo kipindi kile baada ya kikao cha jumuiya ya watanzania alichomshutumu balozi kwamba anagawa watanzania kwa misingi ya chama balozi alisikitika sana na kuuliza huyu mwenzenu jeuri hii anaitoa wapi hasa. Kama hapendezwi na mimi balozi kufungua matawi ya CCM huku ughaibuni ni kwa nini na yeye asifungue ya chadema?
Tatizo wagonjwa ndo wanautamani urais, matokea wakiupata wanapoteza muda mwingi kujitibu badala ya kufanya yale waliyoyahidi e.g Mkwe.reKama mtanzania mwenye sifa, ana haki ya kutangaza nia yake.
Siyo dhambi Zitto kusema anataka urais
Mkuu,Chadema msipomdhibiti huyu mtatuandalia bomu.
Huu ushirika wako Ben saanane na akina Zitto huko mbele utazaa uasi wa kutisha siyo ndani ya chama tu hata usalama wa nchi. Naona kila dalili za uasi wa vijana dhidi ya wazee.
Usalama wa taifa sasa inabidi ufanye kazi kushughulikia hizi mbegu mapema. Kwa bahati mbaya huyu ni mtu wa visasi na hata sasa nilishaongelea kuhusu chuki yake dhidi ya wazungu na wakenya, tunaandaa akina Julius Malema au akina Adolf Hitler bila kujijua.
Kujiamini najua unajiamini sana sijui ni kitu gani kinakupa jeuri kiasi hicho; hata balozi Eva Nzavo kipindi kile baada ya kikao cha jumuiya ya watanzania alichomshutumu balozi kwamba anagawa watanzania kwa misingi ya chama balozi alisikitika sana na kuuliza huyu mwenzenu jeuri hii anaitoa wapi hasa. Kama hapendezwi na mimi balozi kufungua matawi ya CCM huku ughaibuni ni kwa nini na yeye asifungue ya chadema?