Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
Namuona mheshimiwa yumo ndani ya nyumba

1.eti mhe yasemwayo yana ukweli?
2.je ni kweli kwenye chama hakuna mtu mwingine ila slaa peke yake?
3.je Dr akisema hagombei hamtaweka mgombea urais 2015? kumbuka kila kitu kinawezekana as we are human beings and not machines/angels.
 
Haya bwana minyukano ndani ya chama itakapo anza hapo amini usiamini.Wako watu ndani ya chama ambao hawataki kabisa kumsikia huyu jamaa na kundi lake
 
Mkuu nimeachana naye nadhani huyu G.Brain hakumaliza drs la saba.

Afadhali mkuu,dawa ya mjinga ni kumpuuzia ajione ujinga wake hakuna mwingine anaye uchangia,maana ukianza ku argue nae,pia na yeye atajiona kumbe ana + ideas!
 
Kuchangia kuhusu Zitto na mwenzake January kugombea urais 2015 ni kupoteza muda kwani katiba haitawaruhusu kufanya hivyo kutokana na umri wao. Kinachotakiwa kufanyika ni kubadili katiba kwanza, kitu ambacho itakuwa ni vigumu kufanyika.

Hawa vijana inawezekana wana dhamira lakini bado hawajajua jinsi ya kufanikisha malengo yao ya kisiasa. Ili waweze kubadili umri wa kugombea ni lazima wapitie bungeni, ambapo majority ya wabunge wana umri zaidi ya miaka 40. Sasa kitendo cha kusema ni kijana hatakayeweza kukabili challenge za urais, kiasi fulani kitawaudhi wabunge ambao sio vijana na hawataupigia kura huo mswada ukiwasilishwa.

Hawa watu wangetafuta njia itakayofanya hoja yao iwe na mshiko bila ya kudharau upande mwingine. Na kwa kiasi fulani hii inaonyesha ni jinsi gani ambavyo bado hawajaiva katika siasa...
 
habari za kuaminika kutoka ndani ya vikao vya ccm zinadai kuwa CCM INATARAJIA KUMSIMAMISHA WASSIRA a.k.a TYSON kugombea urais kutokana na kuwa na mvuto wa kisiasa hasa katika kampeni za Arumeru mashariki. Souce: Tingatinga
 
Kwa nini mnanchukia Zitto, Atafaa muda muafaka kama yeye alivyosema.

Ni makosa makubwa kumchukia Zitto kama Zitto.Huyu na vijana wengine ni hazina kubwa ndani ya chama miaka ijayo.Anachopaswa kufanya Zitto ni kuwa mtiifu kwa viongozi wake na kukijenga chama kuanzia vijijini. Zitto anapaswa kujiweka mbali na makundi ya wapuuzi wanaochochea migawanyiko ndani ya chama na kujaribu kuwachafua viongozi kupitia mitandao ya kijamii.Binafsi ninaamini nguvu ya CDM kwa sasa pia Zitto ana mchango mkubwa.Zitto anafaa lakini bado anahitaji kupikwa zaidi ndani ya chama.
 
Ndugu zangu. Naomba msome makala nzima kabla ya kuchangia. Msichangie kwa kusoma kichwa cha habari tu. Hii ni makala nimeandika kama majibu kwa makala ya mwanazuoni mmoja kuhusu umri wa Urais.

Nimesema wazi, kuutaka Urais na kuupata ni mambo mawili tofauti. Kwanza lazima chama changu kiniteue. Kama chama kikiona bado lazima nikubaliane na chama. Kama chama kikiona kuna mwanachama mwingine ana uwezo zaidi yangu lazima nimwunge mkono huyo. Hata kama chama kikiniteua lakini wananchi lazima wakubali. Kwa hiyo unaweza kuutaka Urais lakini usiupate!

Pili nimejibu hoja za ubaguzi, hatari na matabaka za mwanazuoni huyo. Ni vizuri MoD akachukua makala hiyo na kuiweka juu kabisa ili watu wachangie jambo walilolisoma.

Miye nitaweka makala hiyo kwenye blog yangu zittokabwe.com

Shukrani kwa ufafanuzi huo, nimesoma makala yako kwa usahihi sana na nimeielewa.

Fanya kazi kwa bidii kwani taifa letu lina changamoto nyingi sana fanyia kazi hizo changamoto kwa nguvu zako zote, naamini tumeshaona bidii yako na tunahitaji ufanye zaidi; wakati ukifika hutakuwa na mpinzani mkuu.

Kuhusu hili swala la ajira kwa vijana naomba uandae forum ya kulijadili na uishauri serikali iliweza kutenga maeneo kwa ajili ya EPZ kwa kila wilaya, itenge tena maeneo kwa ajili ya shughuli za kiuchumi kwa vijana kila wilaya kulingana na mahitaji na eneo kama maeneo ya kilimo, holticulture, matunda, mkonge, korosho, viwanda vidogo vidogo. Anza kwa kuondoa changamoto hii.
 
Labda Zitto wa 2007, lakini Zitto wa 2012 - siungi mkono.

nimepoteza imani na zito ambayo nilikuwa kabla. Huyu na mwenzake wamekaa na mwenzake wanaplani kuwaminya watu waliojenga nyumba na kupangisha,eti itaongeza mapato! Wafanyabiashara kibao wanakwepa kodi,madini yetu, samaki wetu, ardhi yetu wanaacha vinabebwa na wazungu. Wanyama wetu,magogo yetu vyote vinaibiwa, kwa nini umuumize mpangaji? Hawajui kwamba ni kutuumiza sie wapangaji? No matter why walikuwa wanadai umri upunguzwe.
 
habari za kuaminika kutoka ndani ya vikao vya ccm zinadai kuwa CCM INATARAJIA KUMSIMAMISHA WASSIRA a.k.a TYSON kugombea urais kutokana na kuwa na mvuto wa kisiasa hasa katika kampeni za Arumeru mashariki. Souce: Tingatinga

na pia sura yake inauzika, na kwamba ccm wanampango kutumia wingi wao bungeni kuishinikiza serikali ichapishe sura ya rais kwenye noti zetu. Jambo hili litafanya SURA YA WASSIRA ITOKEE KWENYE NOTI PINDI ATAKAPOKUWA RAIS
 
Heshima kwako Zitto,

Nimesoma makala yako kwa kweli imetulia sana na imenivutia kiasi nakosa neno sahihi la kuelezea jinsi nilivyovutiwa na hoja zako.Kuna jambo moja nashindwa kukuamini/kukuelewa ni msimamo wako kuelekea shirikisho la EAC, nakumbuka michango yako ndani bunge letu ulishindwa kutetea maslahi ya Tanzania huku wabunge wengi wakipinga suala la ardhi na ajira kuingizwa katika mkataba wa EAC. Naomba unijuze bado msimamo wako ni uleule na kwanini au umebadilika kwanini ?
Ndugu zangu. Naomba msome makala nzima kabla ya kuchangia. Msichangie kwa kusoma kichwa cha habari tu. Hii ni makala nimeandika kama majibu kwa makala ya mwanazuoni mmoja kuhusu umri wa Urais.

Nimesema wazi, kuutaka Urais na kuupata ni mambo mawili tofauti. Kwanza lazima chama changu kiniteue. Kama chama kikiona bado lazima nikubaliane na chama. Kama chama kikiona kuna mwanachama mwingine ana uwezo zaidi yangu lazima nimwunge mkono huyo. Hata kama chama kikiniteua lakini wananchi lazima wakubali. Kwa hiyo unaweza kuutaka Urais lakini usiupate!

Pili nimejibu hoja za ubaguzi, hatari na matabaka za mwanazuoni huyo. Ni vizuri MoD akachukua makala hiyo na kuiweka juu kabisa ili watu wachangie jambo walilolisoma.

Miye nitaweka makala hiyo kwenye blog yangu zittokabwe.com
 
habari za kuaminika kutoka ndani ya vikao vya ccm zinadai kuwa CCM INATARAJIA KUMSIMAMISHA WASSIRA a.k.a TYSON kugombea urais kutokana na kuwa na mvuto wa kisiasa hasa katika kampeni za Arumeru mashariki. Souce: Tingatinga

Kwa kweli watakuwa wamefanya la maana sana, maana yeye ni taswira ya CCM kabisa.
 
Nashangaa hapa Tz kila mtu anataka kuwa RAIS!! mpaka mzito kabwela nae anautaka urais!! anashinikiza umri wa urais uwe miaka 35!! Bado naaamini Dr slaa au Dr salim Ahmed Salim wanaweza kutuongoza vizuri.
Nawakiulisha.:bump2:
 
zitto ni kijana mpambanaji na jasiri lakini kuna tatizo alilonalo linalomkosesha imani mbele za Watanzania, pamoja na umaarufu wake wote alionao lakini kwa sasa hafai kuwa rais wa Tz,
 
nimepoteza imani na zito ambayo nilikuwa kabla. Huyu na mwenzake wamekaa na mwenzake wanaplani kuwaminya watu waliojenga nyumba na kupangisha,eti itaongeza mapato! Wafanyabiashara kibao wanakwepa kodi,madini yetu, samaki wetu, ardhi yetu wanaacha vinabebwa na wazungu. Wanyama wetu,magogo yetu vyote vinaibiwa, kwa nini umuumize mpangaji? Hawajui kwamba ni kutuumiza sie wapangaji? No matter why walikuwa wanadai umri upunguzwe.

Mkuu wangu huu upuuzi wa kuweka sheria ya kodi kwa wenye nyumba ni hoja hovyo kabisa ya January Makamba.Hakika hiki ni kitanzi kwa vijana wote mijini wanaoishi nyumba za kupanga.Hivi ni mwenye nyumba gani ataacha kupandisha kodi kufidia hasara atakayopata? Ninaomba CDM waongoze maandamano ya kulaani sheria hii haramu.CDM fahamuni nguzo kuu yenu ni Vijana na sisi ndio tutaumia kwa sheria hii ya hovyo isiyojali umasikini wetu.Nimuulize swali January hivi haoni kila serikali inapopandisha kodi vitu vinapanda bei? Sasa anadhani kodi ya kwenye nyumba atabeba mwenye nyumba au mpangaji? Nitalia na Mungu na hii sheria ya hovyo ya kuwaangamiza vijana mpaka siku Mungu atakapojibu maombi yangu.
 
Status
Not open for further replies.
33 Reactions
Reply
Back
Top Bottom