Mimi namkubali Zito kuwa kiongozi mwenye umakini wa hali ya juu, lakini dhana inayojengeka hivi sasa ya kudhani kila kiongozi mzuri ni lazima awe katika ngazi ya urais siiungi mkono! Mtazamo wangu kiongozi mwenye kuleta mabadiriko anatakiwa kutoka katika chama chenye dhamira ya kufanya mabadiriko, ambamo wabunge wake, madiwani, pamoja na wafuasi wake wote wataamua kuyaendea mabadiriko. Na wala si msimamo wa mtu mmoja. Tunayashuhudia yanayotosha kuwa mafundisho. Kiongozi anakuwa na dhamira ya kufanikisha jambo lakini anakosa uungwaji mkono wa kutosha kutoka kwa wahafidhina wa kwenye chama chake au jamii. Katika mazingira kama hayo ni rahisi sana Rais kugeuka DIKITETA. Ninaipenda mno kazi anayoifanya Zito hivi sasa ya kuipa challenge Serikali kwa kuukosoa utendaji usiofaa wa Serikali na kutoa shule pana kwa uma kuujua udhaifu wa serikali kwa upana wake katika sekta mbalimbali.
Hilo ndilo linalomjengea Heshima hivi sasa na kumpa umaarufu. Sitashangaa umaarufu huo ukipungua sana baada ya kuupata urais. Umaarufu aliokuwa nao JK kabla ya urais si huu alionao leo!