Mjumbe anapokuwa kwenye kikao ni ruhusa kabisa kupinga jambo wakati wa majadiliano lakini jambo hilo likihitimishwa kwa kura na ikionekana wengi ndiyo wanaounga mkono basi huo ndiyo unakuwa msimamo wa chama na kila mwanachama anapaswa kuutetea. Sasa kama Mhe. Zitto bado anaendelea kuupinga nje ya kikao, basi huo utakuwa ni utovu wa nidhamu na lazima akemewe na chama kupitia vikao vyake halali. Alichopaswa kueleza Zitto (kama ilikuwa ni lazima aeleze) ni kusema kwamba wakati wa kikao alikuwa na msimamo tofauti lakini uamuzi wa kikao ndiyo anaouheshimu na kuutetea. Hiyo ndiyo GHARAMA ya demokrasia.
Mkuu umeongea vizuri sana, Chadema hawakuona umuhimu wa kukurupuka kwa hili jambo, ilibidi watumie demokrasia ya kupiga kura na maana ya kupiga kura ni kuwa kulikuwa na misimamao tofauti, kwa waliokubali na wasiokubali hiyo move ilikuwa ni haki yao kidemokrasia, na tukumbuke kuwa hilo zoezi lilikuwa ni la siri, lilikuwa ni la wabunge tu labda na viongozi wengine wa juu
Swali la kujiuliza ilikuwaje Zitto aende kwenye vyombo vya habari kuliongelea hilo suala ambalo ahlikuwa la Public, hapa Zitto anatuonyesha yafuatayo:
1) Zitto anataka kuonyesha kwa baadhi ya "
watu wake (Rafiki zake)" kuwa yeye hakuhusika, lakini swali linakuja watajuaje kuwa yeye hakuusika na zoezi lilikuwa ni la siri? jibu ni lazima aende kwenye vyombo vya habari
2) Zitto anajionyesha kuwa yeye yupo juu ya kila mtu kwenye Chama, kama chama kina viongozi wa juu kuliko yeye na labda ndio wangepaswa kulizungumzia hilo swala kwa nini yeye ndio alichukua uamuzi wa kuelezea kilichotokea? je aliutaarifu uongozi kuwa anaenda press kuongelea hilo swala?
3) Zitto anazidi kujitoa uaminifu wake na imani yake katika Chama, inatia hofu sana, kama siri za Chama zinafikia point ya kuwa published, watu watamwamini vipi Zitto?, je kweli anaweza kutunza siri za chama za ndani zaidi?