Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Niliisha wahi andika huko nyuma Zito hana maturity kisiasa! Hivi angekaa kimya ingekuwaje? ama anajitafutia cheap popularity? Nadhani kuna msemaji wa CHADEMA. Binafsi huwa namwangalia kwa jicho la pili mh Zito.

Mch Masa K
 
Wewe usitufanye sisi wote watanzania mazezeta maendeleo gani yatakuja wakati tuna katiba kandamizi unadhani Jaji Nyalali alikuwa mwehu kusema lazima Katiba ibadilishwe ili nchi iweza kusonga mbele

Nataka uniambie kisayansi katiba yetu inahusiana vipi na uchumi wetu?? hayo ni mawazo duni ya kufanya Katiba ndio national priority. Mbona rwanda wanakimbia ki-uchumi, umesikia ni kwa sababu ya kubadili katiba?? Mimi binafsi hua sikubaliani ni mawazo ya wanasheria (hasa wa tanzania) kwa sababu hayaendi kisayansi wala kimahesababu (nadhani ni kwa sababu wengi husoma HKL, HGL na that means hesabu hakuna.
 
kwa siasa za Zitto sidhani kama chama kinaweza kufanikiwa katika adhima yake ya kufikia malengo ya katiba mpya na tume mpya si vizuri kuwa-let down wenzio

huyu bwa mdogo ana skendo zake nzito ndani ya chama...alishapewa baraka zote za kuhama chama..kama si msimamo thabiti wa chama,angewasumbua sana...hakutakiwa kuzungumza mambo ya kupiga...anamfurahsha nani wakati watu wamenuna kwa kura zao kutupwa kapuni...angeita basi press conference kabla hawajapiga hizo kura awaeleze...sijaipenda hiyo...
 
Usiweke maneno kwenye mdomo wa Zitto alisema walijadili walipopishana wakaamua kupiga kura sasa yeye anajua wengi wape ndio ukweli wenyewe humdanganyi mtu hakuna kitu kinaitwa wmenyekiti kumwambia nani swala ni kuwa mwamuzi alikuwa ni kura usipindishe ukweli kwa sababu umetumwa

Nimekuwepo hapa kijiweni kwa mwaka wa 4 sasa, na mara nyingi watu wenye jazba na mitazamo mifupi huishia kuita wenzao wametumwa as if huu ni mtandao wa CHADEMA.. Lazima ukue na uwe unafikiria mbali zaidi ya hapo, haya sasa wamegoma then what?? walikua wanamtumia messege nani?? kueni
 
Zitto Kabwe ameeleza kuwa ni kweli walipiga kura na kukubaliana watoke wakati Rais akizungumza, lakini wao walipinga na ndiyo maana aliamua bora asiingie ndani ya Bunge, amesema kuwa yeye kama Zitto na wenzake aliona ni bora kutoingia kuliko kuingia na kutoka wakati Rais ambaye ndiye alama ya Bunge na Amiri jeshi mkuu akiongeaa.

Kwa vile kutoka ulikuwa msimamo wa chama, basi yeye na wenzake wamekosea na hilo ni swala la Chama kwani wanaweza kuadhibiwa na chama kwa vile kura za kukubaliana kutoka ilishinda.

Zitto alisema kuwa wanasubiria hatma yake katika chama na kusema kuwa hiyo ndiyo gharama ya Demokrasia. Ila amekanusha kuwa jambo hilo lisifikiliwe ni mgawanyiko bali mtazamo tofauti wa mawazo.

Source: TBC 1 News Bulletin

mtazamo wangu mwishoni mwa 2015 zito atajitoa chadema na kujiunga na nccr ili agombe araisi alishawahaidi wapiga kura wake.kipindi kingine hatafika km mgombea ubunge ila uraisi.

Ninachokiona mpaka sasa zito bado anakinyongo na uongozi bada ya kubaniwa wakati wa kutafuta uweneyekiti.hivyo wazo lolote linatolewa na uongozi halimwingi akilini hata liwe zuri vipi.

Wito wangu kwa zito ni bora akajitoa mapena kabla hajasababsha mazara kwa chama.vyama vipo vingi
 
Safi Zitto kwa kua mkweli, demokrasia sio kuburuzwa kwa maamuzi ajabuajabu tu. Palipo na wazo kwa wasomi hoja lazima ichambuliwe na kila mmoja kua na hoja na maoni tofauti na wenzake.

Kwa hoja zilitolewa kundi la zito ni sahihi ila kundi la pili wanajua sheria ila walitenda dharau kwa katiba iliyowaweka bungeni.Mimi sina chama kwa kua bado sijaamua kujiunga na chama chochote na kura naangalia mtu anayefaa na kuweza kuleta maendeleo.

Mi nawaomba washabiki wa chadema kuacha kulazimisha watu kufuata misimamo yenu kwa kua kila mtu anaouwezo wa kutafakali.Najua wale waliopata elimu kwa njia za kifisadi kwa kua baba na mama zao wanafanya kazi serikalini na kubenefit majasho ya baba zetu na mama zetu wanaohangaika na umachinga ili tusome, hao ndo wanaongoza kutoa comment za bendera fuata upepo.

IF YOU ARE A REALY GREAT THINKER COME UP WITH NEW IDEA AND DON'T BE A DOGMA.

Nani alikwambia watu wote lazima wawe Chadema,ccm au cuf?si lazima. CHANGE YES WE CAN lakini kwa hoja za kushawishi watu! YES Slaa anashawishi, huu muda si wakulumbana ni kuhakikisha hii miaka mitano upinzani hakuna kulala ni kijiji hadi kijiji kampeni mfulululizo na mwisho ni ushindi. Hakuna aishiye milele hata ccm itakuja kufa!
 
Alichofanya zito ni kawaida,co rahisi watu wote kuwa na maono sawa ingawa ccm wanaweza kuitumia kama mtaji wa kuisambaratisha cdm kama wasipokuwa makini

sawa mnaweza wote msiwe na maono sawa lakini kama ilivyosemekana palifanyika upigaji wa kura, hivyo ilipaswa upande ulioshinda uungwe mkono kama vile CCM walivyo wamoja katika maamuzi yao sio kutoka na kuropoka kwenye vyombo vya habari wakati si msemaji mkuu wa chama
 
Niliisha wahi andika huko nyuma Zito hana maturity kisiasa! Hivi angekaa kimya ingekuwaje? ama anajitafutia cheap popularity? Nadhani kuna msemaji wa CHADEMA. Binafsi huwa namwangalia kwa jicho la pili mh Zito.

Mch Masa K
Miye humwangalia kwa jicho la tatu.
 
Nataka uniambie kisayansi katiba yetu inahusiana vipi na uchumi wetu?? hayo ni mawazo duni ya kufanya Katiba ndio national priority. Mbona rwanda wanakimbia ki-uchumi, umesikia ni kwa sababu ya kubadili katiba?? Mimi binafsi hua sikubaliani ni mawazo ya wanasheria (hasa wa tanzania) kwa sababu hayaendi kisayansi wala kimahesababu (nadhani ni kwa sababu wengi husoma HKL, HGL na that means hesabu hakuna.

Labda uwe na matatizo ya uelewa utafurahiaje katiba mbovu ulasema eti ndio kitu kinachofaa ukweli wenyewe Ruanda wameshaingia kwenye mchakato wa white paper ili kurekebisha katiba yao tunahitaki katiba mpya ili kufuta haya majizi na mabakaji ya demokrasia peleka salamu waamie watanzania wote sio chadema tuu tumeamua wakati wa mabadiliko ni sasa
 
Nimekuwepo hapa kijiweni kwa mwaka wa 4 sasa, na mara nyingi watu wenye jazba na mitazamo mifupi huishia kuita wenzao wametumwa as if huu ni mtandao wa CHADEMA.. Lazima ukue na uwe unafikiria mbali zaidi ya hapo, haya sasa wamegoma then what?? walikua wanamtumia messege nani?? kueni
Kuwa JF miaka mingi si kuwa una busara, mtu gani unasema hatuna haraka na katiba wakati wanasheria na majaji wenyewe wameshaona katiba ina kasoro.
 
mtazamo wangu mwishoni mwa 2015 zito atajitoa chadema na kujiunga na nccr ili agombe araisi alishawahaidi wapiga kura wake.kipindi kingine hatafika km mgombea ubunge ila uraisi.

Ninachokiona mpaka sasa zito bado anakinyongo na uongozi bada ya kubaniwa wakati wa kutafuta uweneyekiti.hivyo wazo lolote linatolewa na uongozi halimwingi akilini hata liwe zuri vipi.

Wito wangu kwa zito ni bora akajitoa mapena kabla hajasababsha mazara kwa chama.vyama vipo vingi

Itakula kwake anaheshima kubwa sana akiwa chadema lakini hatutashangaa
 
zitoo ni nani katika chama mpaka apingane na wakuu wake hakuna demokrasia katika hili huyu ni msaliti na chama kichukue hatua dhidi yake faster au wananchi tuchukue hatua???????msaliti na auawe uchi na aibu imrudie mamaake.;;;

Hiyo ndiyo sera ya Chadema?

Hon Zito ameng'amua kuwa uongozi wa Chadema umewehuka na mafanikio waliyoyapata, sasa ni kukurupuka kwa kwenda mbele.

Hon, If I may give an advice;
....achana na wasanii wa kisiasa. Mungu amekujalia talanta ya uongozi na tunakujua kuwa una uchungu wa dhati kwa nchi yako. You are our potential next president.

So go for real serious politics!

CCM is one of the living examples in that domain.
 
Nataka uniambie kisayansi katiba yetu inahusiana vipi na uchumi wetu?? hayo ni mawazo duni ya kufanya Katiba ndio national priority. Mbona rwanda wanakimbia ki-uchumi, umesikia ni kwa sababu ya kubadili katiba?? Mimi binafsi hua sikubaliani ni mawazo ya wanasheria (hasa wa tanzania) kwa sababu hayaendi kisayansi wala kimahesababu (nadhani ni kwa sababu wengi husoma HKL, HGL na that means hesabu hakuna.
Kwa hiyo ungependelea na sisi Tanzania tuwe na utawala wa mtu mmoja dikteta kama Rwanda au? Katiba itasaidia kutuondolea watawala wabovu kama hawa tulio nao sasa hivi ndani ya CCM. Hii ni hatua ya kwanza kuleta maendeleo endelevu. Sasa hivi CCM wanasema (Makamba) kwamba lazima wao washibe kwanza ndio waanze kufikiria matatizo ya wananchi. Tanzania hatuna Kagame, katiba itatusaidia kuweka mfumo wa kuwapata watawala bora na kuwaondoa mamlakani wanapoboronga. Bila hiyo tutaendelea kusikiliza ngonjera tu za akina Makamba.
 
Zitto Kabwe ameeleza kuwa ni kweli walipiga kura na kukubaliana watoke wakati Rais akizungumza, lakini wao walipinga na ndiyo maana aliamua bora asiingie ndani ya Bunge, amesema kuwa yeye kama Zitto na wenzake aliona ni bora kutoingia kuliko kuingia na kutoka wakati Rais ambaye ndiye alama ya Bunge na Amiri jeshi mkuu akiongeaa.

Kwa vile kutoka ulikuwa msimamo wa chama, basi yeye na wenzake wamekosea na hilo ni swala la Chama kwani wanaweza kuadhibiwa na chama kwa vile kura za kukubaliana kutoka ilishinda.

Zitto alisema kuwa wanasubiria hatma yake katika chama na kusema kuwa hiyo ndiyo gharama ya Demokrasia. Ila amekanusha kuwa jambo hilo lisifikiliwe ni mgawanyiko bali mtazamo tofauti wa mawazo.

Source: TBC 1 News Bulletin
Normally, Zitto has got two contrasting traits:

1. the content of his message/purpose is always near perfect;

BUT

2. he's second to none in terms of "poorest" art of delivery

So he needs some counselling (an intensive one if I have to be emphatic) on item 2 above to be close to what we could call a good leader.
 
Nimekuwepo hapa kijiweni kwa mwaka wa 4 sasa, na mara nyingi watu wenye jazba na mitazamo mifupi huishia kuita wenzao wametumwa as if huu ni mtandao wa CHADEMA.. Lazima ukue na uwe unafikiria mbali zaidi ya hapo, haya sasa wamegoma then what?? walikua wanamtumia messege nani?? kueni

Ni kwa sababu ya mawazo yako ambayo unasema katiba ni karatasi ndio maana nikasema kama kweli ni mawazo ya aina hiyo uyakuwa umetumwa na dhamira potofu katiba ya nchi kama si kitu kwa nini wanasiasa wakiteuliwa wanaapa kuilinda katiba,unapovunja katiba utakuwa na maendeleo gani kutumwa kwa dhamira potofu kama yako ndiko kumeliangamiza taifa letu nikatoa mfano ambao jaji Nyalali aliona kulikuwa na sheria zaidi ya 40 ambazo zingeweza kudumaza kabisa maendeleo yetu na kuiweka nchi yetu katika hali tete miaka 20 iliyopita na kweli leo tunayaona katiba mbovu tunasogelea kwenye hatari ya kuparurana wenyewe
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), walikaa chini na wakafanya demokrasia ya uamuzi kwa kupiga kura, hayo yote sisi hatukuyajua na yalikuwa ni siri ya Chama, kama hayakuwa siri, Katibu ama mwenyekiti wa Chama angetueleza (Kupitia vyombo vya Habari),

lakini kitendo cha Zitto kwenda kwenye vyombo vya habari na kuiongea hiyo siri ya vikao vyao ni USALITI, MIMI hapa simpingi Zitto kwa uamuzi wake aliochukua wa kutokubaliana na hilo la kutoingia bungeni kabisa, hiyo ni Demokrasia na ndio maana Chadema walipiga kura, ninachomlaumu na kumwona Zitto kuwa msaliti iweje aende kwenye vyombo vya HAbari na Kuropoka, Chama kitamwamini vipi tena katika siri zingine za kichama,

Zitto inampasa kuelewa kuwa Chama kina viongozi na kuna wasemaji, Mwenendo wa Zitrto ndani ya Chadema ni wakutia mashaka sana, kwa nini anapenda kwenda kwenye vyombo vya habari bila baraka za viongozi wake, Angalia issue kama ya mwenyekiti wa kambi ya upinzani bungeni, nadhani kwake ilikuwa ni busara kusubiri maamuzi ya chama kupitia vikao vyao ili wapendekeze jina, lakini alikurupuka na kutangaza atagombea hiyo nafasi,

Ushauri kwa Zitto
ki ukweli kabisa siasa zako haziendani na Chadema kabisa, uko fast sana, una siasa za kipekeyako, za kibinafsi na sio za kichama, kama ukiwa kwenye Chama cha muhimu ni kufuata chama kinataka na kinasema nini, aina za Chama zinazokufaa ni kama TLP na NCCR, kwamba kila mtu anasema lwake
Very tru ....ht mm zitto naona haamininiki siku hz.
 
Itakula kwake anaheshima kubwa sana akiwa chadema lakini hatutashangaa
Huyu jamaa ingawa ni kiongozi wetu lakini akiamua kutoka leo nitafurahi sana, ninachoomba Chadema iende naye taratibu wasimpe cheo kikubwa wala wasimfukuze ajiondoe mwenyewe, walikuwapo kina Kabouru enzi chama hakina mvuto atakuwa Zitto wakati chama kina vichwa vya uhakika, kwa busara za uongozi huwezi mlinganisha Zitto na Lissu.
 
Labda uwe na matatizo ya uelewa utafurahiaje katiba mbovu ulasema eti ndio kitu kinachofaa ukweli wenyewe Ruanda wameshaingia kwenye mchakato wa white paper ili kurekebisha katiba yao tunahitaki katiba mpya ili kufuta haya majizi na mabakaji ya demokrasia peleka salamu waamie watanzania wote sio chadema tuu tumeamua wakati wa mabadiliko ni sasa

Nashukur kwamba umeprove huna uwezo wa kunihakikishia ni kwa nini Katiba ndio iwe national Priority yetu badala ya maendeleo? Na umeshindwa kunihakikishia ni jinsi gani katiba yetu inachangia kua nyuma kimaendeleo?? Umenidhihirishia ninaongea na mtu mwenye vidato vingapi. Ni wakati wa kuacha kuota, ni wakati wa kudiscuss vitu in reality. Si TZ tu, Africa kwa ujumla. Katiba ya tanzania haipo Msumbiji, Malawi, Zambia, Namibia, Congo, n.k. Nchi zote hizo ni maskini, unataka kuniambia na Africa nzima ni masikini kwa sababu ya CCM na katiba ya Tanzania?? Think further my friend.

Lazima tubadilike, badala ya kua tunadiscuss ndoto, tudiscuss vitu vya kutuondoa kwenye umaskini. Tushikamane kwa pamoja kwa ajili ya kizazi kijacho. Nikuhakikishie kwamba mie sina tatizo la uelewa hata kidogo, ndio maana nimekataa kunyweshwa sumu na waroho wa madaraka na wafanya biashara ya Ruzuku. Hiyo analysis yako ndio hiyo hiyo nimekua nikiiona kwenye gazeti la tanzania daima. Think more than that, Katiba, katiba, utafikiri hiyo ndio inasimamia kilimo, viwanda, na uzalishaji kwa ujumla. Katiba ni guide tu, kinachotakiwa ni strategies na mapendekezo mazuri ya kujenga. Sio kugoma kama watoto
 
Kuwa JF miaka mingi si kuwa una busara, mtu gani unasema hatuna haraka na katiba wakati wanasheria na majaji wenyewe wameshaona katiba ina kasoro.

Wewe wala usijaribu kudandia treni kwa mbele,, Kasoro kasoro, nataka unitajia priority zetu 20 kwa sasa hapa nyumbani, ukianza na Afya, Elimu, barabara, maji, n.k ukishaorodheshwa vyote, naomba uniambie Katiba umeiweka namba ngapi. Thats my point, katiba ni maelekezo tu yaliyo kwenye vitabu, katiba haiendi viwandani au kwenye mashamba kuongeza kilimo. Fikiria zaidi ya hapo mdogo wangu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom