Njilembera
JF-Expert Member
- May 10, 2008
- 1,496
- 610
Siku zote nasema namkumbuka Zito toka Daruso, hajabadilika, sidhani kama atabadilika. Huyo ndio Zito.
Kama kura ilipigwa na wengi wakashinda, basi uamuzi huo unawabana wote, na ni lazima kila mmoja ashiriki! Hainiingii akilini kuwa uamuzi wa demokrasia unatekelezwa na baadhi na wengine kuacha. Collective responsibility bana! Zito sijui ni utoto au ni nini! Tena hakupaswa kwenda kwenye vyombo vya habari kueleza yaliyojiri na msimamo wake binafsi. Yeye ni Kaimu Katibu Mkuu, maamuzi ya chama ni ya wote, na hata hakubaliani nayo, ambalo ni jambo la kawaida, hana budi kuelezea msimamo wa wengi na kuacha haya ya ubinafsi.
Zito anafahamu yeye ni target number one, when it comes to partisan politics kati ya CCM na Chadema. He has to be careful in his statements as the CCM wata-manipulate hizo statements and in the end kufifisha nguvu za Chadema. Ni aibu huyu kijana hafikirii matokeo ya statements na vitendo vyake! Akumbuke ameshakua sasa, sio kila kitu anachokiona kinafanywa na Baba na Mama anakiweka hadharani!