Kuanza kutofautiana mapema ni dalili mbaya sana kwa chama makini kama CHADEMA, ambacho kimeaminiwa na wananchi kwa imani kubwa sana. Ukichukulia hali ya kutokuwa na msemaji mkuu wa chama, kama Zitto anaweza akaenda kwenye media na kuongelea mambo ya ndani ya Chama ni hatari sana kwa chama kilicho makini. Chama cha CHADEMA niliamini ni chama makini kisicho hata na doa ya kukosa uadilifu na kuaminiana.
Kauli ya zitto kwa media kuongelea mambo ya chama kwamba waligawanyika katika msimamo wa kutoka nje wakati rais anaongea lina faida kwa nani? Na kusudi lake ni nini? Kwani nini maana ya demokrasia pale kura zinapoamu?, Je kuna haja ya kugoma kufuata maamuzio ya kura? Je Hio ni demokrasia gani? Hakuna tofauti ya kupinga demokrasia huku ukiubili Demokrasia.
Hapa CHADEMA wanajikoroga tena sana tu. Hakuna haja ya kuwa Mwanachama wa chama kisicho kuwa makini kama CHADEMA. Nimekuwa mwanachama wa muda mrefu wa Chadema, Nimeihubiri CHADEMA lakini kwa haya ya akina zitto ni bora kujiweka pembeni.
Hapa tusifanye tunatetea kwa maoni ya kutifautiana kwa mtazamo na kimawazo. Hapa ukweli watu tunaujua kuwa Umakini ndani ya CHADEMA umepotea, Kwa mitazamo hii Tutarajie kusambaratika kwa CHADEMA.
Mimi binafsi naomba kujiondoa Kabisa kuwa mwanachama hai wa CHADEMA mpaka hapo tutakapo kuwa tumekomaa kisiasa. Nahisi kwa vijana makini kujiunga na CHADEMA ni uamuzi wa kurisk mno, kwani uchanga wa chama na kuwa na watu waoga kama Zitto, Mtu ambaye hawezi kuheshimu demokrasia ndani ya chama ni hatari isiyovumilika na watu makini. Hivyo mimi kama mtu makini nahisi kabisa nilikosea kujiunga na CHADEMA ni heri kuwa mtu asiye na CHAMA kiliko kuwa mwanachama wa CHAMA chochote kwa Tanzania yetu hii.
Kwa hili CHADEMA wapoteza tumaini langu kwao.